01/06/2021
JAZANDA.
Hii ni mbinu ya kulinganisha vitu viwili moja kwa moja bila kutumia viunganishi. Katika ukurasa wa 4 tunasoma; "Mwangeka alisema Ridhaa kupitia kwa sauti ya mawazoni mwake, kumbe wewe ni sawa na yule Mwangeka wa kihistoria ambaye kivuli chake kikitembea siku zote mbele yake, ambaye mwili wake ulikuwa kaka tu, roho yenyewe iliishi nje ya kaka hillkwa kutotaka kudhibitiwa? Umewezaje kunusurika? Kumbe wadhifa waliokupa wa kwenda kudumisha Amani katika mashirika ya kati umetokea kuwa wongovu wako?"
Hapa, Ridhaa anamlinganisha Mwangeka wa kisasa na yule Mwangeka wa kihistoria.
Katika ukurasa wa 6 tunasoma; "Basi niambie, baba, unatumia mantiki gani kusema kuwa sisi si watoto wa miaka hamsini? Je, miaka hamsini ya uhuru imetukuza kiuchumi au tumebaki kuwa wategemezi wa hao hao ambao walitupa uhuru?"
Hapa kuna ulinganishi kati ya miaka hamsini ya uhuru wa taifa, na miaka hamsini ya kuzaliwa kwa hawa watu ambao bado hawajajikomboa kutokana na ule ukolonio mambo leo.
Katika ukurasa wa 8 tunasoma; "Ardhi ya mzee Mwimo Msumbili ikawa haitoshi kuyalea madume yake ishirini "
Vijana wake Mzee Mwimo wanalinganishwa na madume ishirini.
Katika ukurasa wa 29 tunasoma; "Nilihisi kwamba ingekuwa bora k**a tungefia katika mazingira tuliyoyazoea; huenda hata tungepata wa kutuomboleza, kuliko kufia ugenini "Sasa umeanza kufikiria k**a wafuasi wa nabii Musa ambao baada ya kukosa chakula huko jangwani, walimshutumu kwa kuwatoa kule Misri. Walidai kuwa huko Misri wangekula matikitimaji yao pamoja na kuwa watumwa!"
Hapa, msemewa anafananishwa na wale wana wa Israeli waliOtamani kuwa ni heri wangekufia huko misri badala ya kupelekwa jangwani na Musa kufia huko.
2. TASHIHISI/UHUISHAJI.
Hii ni mbinu ya kupatia kitu kisicho uhai sifa za kiumbe mwenye uhai, au sifa za kibinadamu. Katika ukurasa wa 3 tunasoma; "Alijiona akiamka asubuhi ambayo ilizaa usiku wa jana, usiku ambao ulitandaza kiza katika maisha yake "
Usiku unapewa sifa za kuwa na uhai na ku