12/03/2021
NIUZE NYANYA?
Ni miongoni mwa maswali wanayojiuliza watu wengi wakitaka kuonyesha wazi kwamba wanachoangalia siyo fursa zilizopo kwenye nyanya bali udhaifu na dharau utakazozipata kwa kuuza nyanya hizo.
Hebu twende taratibu. Chukulia mfano maembe, yana hatua za ukuuaji hadi kufikia mahali pa kutumika. Utaona wakati sahihi wa kuliwa ni pale yanapokomaa. Kuna usemi maarufu unaosema "Fursa ni k**a maembe, wakati unasubiri yaive wengine wanayala kwa chumvi" kadhalika na kila wazo la kuzalisha faida.
Mara nyingi siyo chache, watu wengi wangependa kupata kazi mahali ambapo kuna kila kitu; yaani kwa ufupi ukute viti vya kuzunguka, meza nzuri za heshima na viyoyozi. Mazingira k**a hayo yenye ushawishi kwa jamii utaona ni rahisi mtu kufurahia kazi ya namna hiyo yenye hadhi ambayo ataweza kupiga picha na kuwavutia wanaomfahamu na jamii kwa ujumla.
Jambo moja dhahiri ni kwamba uzuri wa kazi au biashara haupimwi kwa uzuri wa jengo la ofisi au samani (furniture). Linapokuja swala la kutengeneza biashara yenye manufaa basi bidhaa yoyote inaweza kufaa kulingana na uhitaji na faida inayoacha.
Ndiyo, siyo suala la nyanya tu, hata k**a ni manyoya ya kuku, samadi (vinyesi vya wanyama), mchanga, kokoto, nyasi hata k**a ni pumba. Kinacho angaliwa siyo uzuri wa bidhaa bali uwezo wa bidhaa hiyo kuhitajika sana sokoni.
Wakati wewe unashangaa juu ya nyanya kuna watu wao wanauza mkojo wa sungura na wanazalisha mpaka 200,000 kwa dumu la lita 20. Mkojo huu hutumika k**a mbolea maalum mashambani
Mambo ya muhimu ya kuzingatia ni kwamba:
1. Mfumo wa biashara (business system) ndiyo kitu pekee kitakacho kutofautisha na mkulima kule shambani. Bill Gate kwa mfano hakuanzisha Microsoft bali alinunua wazo kutoka kwa kikundi cha watu mtaani akajenga biashara na kuanza kuliuza wazo hilo. Miongoni mwa wateja waliomletea matokeo makubwa alikuwa IBM na yaliyofuata mpaka leo ni historia. Angalia namna bora ya usambazaji, jinsi ya kuwafikia wateja wengi na jinsi ya kutengeneza mfumo utakaowahudumia watu wengi zaidi (Hii ndiyo sehemu muhimu zaidi kuliko hata bidhaa au huduma unayotoa)
2. Anza taratibu (Humble beginning). Epuka kuanza kwa nguvu kubwa na kuokoa gharama za uendeshaji. Biashara nyingi kubwa hazikuanzia maghorofani bali kwenye karakana majumbani au nje ya miji. Fuatilia historia ya Google, Apple, Disney na Alibaba
3. Lenga kutatua changamoto zaidi na siyo kupata faida za haraka haraka. K**a unataka faida za haraka haraka siyo wazo sahihi maana inaweza ikakuchukua miaka mpaka kupata uelekeo sahahi. Hivyo unahitaji uvumilivu, na nguvu ya kuendelea kutoa huduma mfululizo bila kuacha ( | | | )
4. Badala ya kuona aibu kuwa utaonekanaje, ona aibu juu ya ugali na vitu vya bure unavyotumia hapo nyumbani. Ndiyo, pengine umri unaenda na wewe unasubiri kazi safi ambayo kila mtu atakusifu. Siyo wakati huu
5. Maarifa katika zama hizi yamejaa kila mahali na unaweza ukayapata bure au kwa gharama ndogo kabisa. Pia unaweza kujifunza moja kwa moja kwa watu wenye wazo sawa na la kwako. "Na k**a elimu ni ghari basi jaribu ujinga"
Ndiyo unaweza kuuza siyo nyanya tu bali huduma na bidhaa yoyote na ukafanikiwa. Unahitaji wazo sahihi, mahali sahihi na muda sahihi. Siyo kila wazo ni fursa mahali ulipo. Tafuta wapi linahitajika fanya majaribio kisha wekeza.
Kila la heri
Unaweza kutembelea www.zanobay.com
Ukipenda Like | share | Comment. Asante
Imeandaliwa na: Joseph Magweiga Marwa