08/08/2026
Kwa pamoja tunasema Moyo wetu umejaa shukrani zisizo na kifani kwa kila mmoja wenu mliochukua muda kututakia heri ya ndoa,Hadi harusi Kila ujumbe, kila simu, kila dua na kila neno la upendo mlilonitumia liligusa nafsi zetu kwa namna ya kipekee.
Sikuhii haingekuwa na maana k**a isingepambwa na hisia zenu za upendo, moyo wenu wa ukaribu, na baraka mlizonitamkia.
Tumejiona wenye bahati kubwa kuwa na watu wa thamani k**a ninyi maishani mwetu
Kwa upendo wenu, mmetufanya tutabasamu zaidi. Kwa maneno yenu, mmetupa nguvu mpya. Na kwa dua zenu, naamini ndoa yetu mbele itaangazwa.
Asanteni sana kutoka moyoni. Mungu awazidishie baraka na furaha k**a ile mlotuletea Jana .
Leo Mr & Mrs JUMANNE tunatambua kwa moyo wa dhati kuwa siku ya Harusi yetu isingekuwa ya kipekee k**a isingekuwa ninyi. Mmesimama nasi mmetubeba pale tulipochoka, mkatufariji pale tulipokuwa na hofu, mkatoa muda, nguvu, mawazo na mali zenu bila kutarajia malipo yoyote.Nimegundua kuwa utajiri wa kweli si fedha wala mali, bali ni kuwa na watu wenye mioyo ya upendo k**a ninyi. Kila hatua mliyopiga kwa ajili yetu imeacha alama isiyofutika moyoni kwetu Mmefanya ndoto zetu iwe uhalisia, na hilo hatutaweza kulisahau maishani. K**a Mimi na mke wangu tungekuwa na uwezo wa kuwalipa kwa kila jema mlilotutendea, bado nisingeweza kufikia thamani ya upendo wenu. Ninachoweza kufanya ni kusema asanteni, lakini najua neno hilo ni dogo mno kulinganisha na ukubwa wa wema wenu.
Namuomba Mungu, ambaye huona hata jambo dogo lililofanywa kwa upendo, awafungulie milango ambayo hakuna mwanadamu atakayeifunga.* Awabariki katika familia zenu, biashara zenu, kazi zenu na ndoto zenu. K**a vyeo vyenu vya juu kazini viipo mbali basi namwomba Mungu awasogezee karibu na K**a ridhi zenu ziko mbali Allah awasogezee siku zote msipungukiwe na chochote,kuanzia furaha , aman,afya,mafanikio,Ridhiki. Machozi ya furaha mlotufanya tutoe Jana , Mungu ayabadilishe kuwa vicheko na ushindi usioisha katika maisha yenu.🤲🙏