12/04/2022
MAKUNDI YA WALIOPO SOKONI
Je wajua sokoni hakuna adui bali kuna mshindani wa kibiashara?
Na je wajua kuwepo kwa mshindani wa kibiashara ni fursa?
Katika biashara nyingi kuna watu walishakuwepo kwenye biashara hiyo kabla au baada ya wewe kuanza kuifanya.
Tupate taswira ya kile ambacho leo nahitaji kukushirikisha kupitia makundi haya;
Market Leader
Ni wale ambao wana mauzo makubwa sokoni na ndio walioshika soko kwa bidhaa husika. Hawa ni wale ambao jina lao la biashara au bidhaa au huduma huja vichwani mwa wateja haraka pale ambapo bidhaa au huduma ya namna hiyo ikihitajika.
Mfano, Katika huduma za ushehereshaji MC Gara B ni market leader katika eneo hilo la huduma. Kutokana na takwimu za mwaka 2021 Vodacom ndio market leader katika sekta hiyo ya biashara ya mawasiliano.
Market Challengers
Ni wale ambao hukuza mauzo yao sokoni kwa kujiwekeza katika ushindani wa kibiashara na washindani wao. Hawa kwa kiwango kikubwa huwa wapo chini ya market leader, hivyo harakati na mikakati yao yote hujiwekeza katika kumshinda market leader wa soko au bidhaa husika.
Mfano mzuri wa Market Challengers ni Maji ya Viwandani k**a vile Uhai au Afya yakipambana na Maji ya Kilimanjaro sokoni.
Market Follower
Ni wale ambao hufuata au hukopi kile afanyacho market leader. Huwa haonyeshi hushindani kwa market leader ila hukopi mikakati yote yenye mafanikio kutoka kwa market leader. Hutambua namna ya kuwashikilia na kuwatunza wateja alionao. Hawa huwa hawana maamuzi yoyote kwenye bei, ubora wala mauzo.
Mfano wa market followers ni wafanyabiashara wanaojihusisha na uwakala wa fedha mtandaoni uwe ule wa benki au mitandao ya simu, au wasajili laini za mitandao ya simu n.k.
Market Nicher
Ni soko ambalo hutumika kuuza bidhaa maalum, ni soko ambalo huuza bidhaa zinazotosheleza mahitaji maalum ya soko fulani, kiwango maalum cha bei ya bidhaa, ubora wa uzalishaji na jamii iliyokusudiwa. Si kila bidhaa inaweza kutafsiliwa na Market niche. Mfano King’amuzi cha DSTV ina market niche ya wateja ambao hufuatilia ligi ya Uingereza kwa nchi ya Tanzania. Hii ni tofauti na wateja wa King’amuzi cha AZAM ambao wateja wake kadhaa ukipenda kwa ajili ya ligi kuu ya nchi hiyo ya Tanzania.
Baada ya kutambua makundi hayo, tuna maswali ya kujiuliza k**a wafanyabiashara;
1. Je kati ya hayo makundi tupo kundi lipi ?
2. Je twataka kuwa kundi lipi kati ya hayo kwa bidhaa au huduma tuiuzayo sokoni?
3. Je napaswa kuwa na nini au kufanya nini ili nifikie kundi ninalolitamani?
NB: Usikose kipindi kijacho tutakachotazama mbinu za kuingia sokoni kwa kundi fulani.
Imeandaliwa na;
BE Consult Ltd
Tel: +255 713 706 562
Watsup: +255 786 670 237
Facebook: Be Consult Co. Ltd
Instagram: beconsult_co
E-mail: [email protected] / [email protected]