Dafu Wellness

Dafu Wellness Tunawasaidia Wanawake kutatua matatizo ya uzazi kirahisi kabisa.

Kabla hujakata tamaa, nakuongezea mambo muhimu ya kuzingatia ili kuhakikisha mirija ya uzazi iko safi muda wote.Kwa kuku...
11/02/2022

Kabla hujakata tamaa, nakuongezea mambo muhimu ya kuzingatia ili kuhakikisha mirija ya uzazi iko safi muda wote.

Kwa kukumbusha ni kwamba mirija ya uzazi husaidia yai kusafiri kutoka kwenye ovari mpaka kwenye fuko la uzazi, hivyo mirija ya uzazi ikiziba yai la mwanamke huwa vigumu kusafiri kutoka kwenye ovari mpaka kwenye mji wa uzazi mimba inapotungwa...

Mirija inaweza kuziba iwapo k**a itashambuliwa na fangasi au bakteria na kupelekea kuziba kwa kujaa maji au kuvimba, au iwapo k**a kuna uvimbe wa fibroid kwenye mji wa uzazi.....

Pia k**a umewahi kuharibu mimba na kusafishwa kwa vyuma inaweza kupelekea vidonda au makovu ndani ya mirija ambayo huweza kusababisha mirija kuziba kwa sababu ya kuwepo kwa makovu
Wakati ukiendelea kutafuta dawa bora ya kukusaidia, jitahidi kuweka mazingatio ambayo yatakusaidia kukupa matokeo haraka kukuepusha na oparesheni
1. kwa sababu mirija inaweza kuziba kutokana na matatizo ya bakteria/fangasi, jitahidi kutibu magonjwa ya kaswende, U.T.I. sugu na matatizo ya P.I.D kwa kuzingatia usafi na matumizi ya vyakula vya kukusaidia kusafisha kizazi k**a tangawizi, tufaha (apple), kitunguu saumu, binzari ya manjano, maziwa mtindi, karafuu n.k
Weka mbali vyakula ambavyo si rafiki kwa afya yako k**a vyakula vya kukobolewa, soda, vyakula vya makopo na vile vya kutiwa mafuta mengi (natumaini unakumbuka)
2. Kwa sababu mirija inaweza kuziba kwa sababu ya uvimbe na makovu ni muhimu sana kupendelea kutumia vyakula vyenye kuondoa vivimbe ndani ya mwili na kubalansi homoni, vyakula hivi ni pamoja na Limao, Mdalasini, Machungwa, Mboga za Majani, Pilipili hoho, Kotimiri, Iliki n.k
3. Punguza stress, jitahidi kujiwekea mazingira ambayo yatakusaidia kuwa na furaha, msongo wa mawazo ni chanzo cha homoni kuvurugika, na mvurugiko wa homoni ni chanzo cha vivimbe kuongezeka ukubwa, usipothibiti stress unaweza kujikuta unazidi kuongeza tatizo badala ya kumaliza tatizo
4. Pendelea kufanya masaji ya maeneo ya nyonga na chini tumbo kwa kutumia mafuta ya mnyonyo...
5. Punguza uzito, hakikisha una uzito unaoendana na kimo chako
6. Fanya mazoezi ya Yoga... K**a ni mpenzi wa Mazoezi ya Kunyoosha Mwili wako basi fanya mazoezi ya yoga muda wowote utaoamua kufanya... Unaweza kuingia youtube kujifunza, zipo aina mbalimbali za kufanya yoga.... Unaweza kupitia intro kidogo ya video niliyoweka youtube
Bofya https://youtu.be/jd4W0DUKn5I

K**a una changamoto za uzazi k**a uvimbe, mirija kuziba, P.I.D, Hedhi Haieleweki na Unatamani Kuzitibu Changamoto hizi kwa pamoja nakushauri kuchukua huku ukiendelea kuzingatia kanuni zako bora za uzazi.

Wasiliana nami kwa simu au kwa kutuma ujumbe inbox 0678634046

Hedhi yako imevurugika na unawaza ni kwa namna gani utaweza kuiweka sawa....!Unatumia dawa zipi kwa sasa kurekebisha hom...
10/02/2022

Hedhi yako imevurugika na unawaza ni kwa namna gani utaweza kuiweka sawa....!

Unatumia dawa zipi kwa sasa kurekebisha homoni au ndo umekataa tamaa kuhusiana na mambo ya uzazi....!

Today i have some tips for you..!
Wakati ukiendelea kutafuta ufumbuzi wa tatizo lako nakusisitiza kufanya mabadiliko katika vyako vya;
Haijalishi unaishi mazingira yapi au uchumi wako ukoje, jitahidi kuweka ulazima wa
👇🏼
• Kula parachichi zima 1 kila siku k**a huwezi walau kipande kimoja cha parachichi
• Tumia vyakula vya wanga kwa kiwango kidogo, vyakula k**a Mahindi, Ugali na Dona, Viazi, Mihogo, Ndizi, Tambi n.k, ila ongeza wingi wa mboga za majani na matunda k**a spinach, bamia, msusa, parachichi, ndizi mbivu n.k ni vizuri sana kwenye kuimarisha homoni zako
• Epuka kahawa, chai ya rangi, soda nyeusi na vinywaji vingine vyote vyenye kiwango kingi cha kafeina ndani yake
• Achana na msongo wa mawazo (stress) na upate usingizi wa kutosha kila siku, k**a hupati usingizi jitahidi kunywa glass ya maziwa fresh yaliyotiwa mdalasini na vijiko kadhaa vya asali mbichi, inaleta usingizi kuliko kumeza pilitoni
• Usitumie dawa za uzazi wa mpango k**a unahitaji kuweka homoni zako
• Kuna vyakula tunafosi kivitumia ila havina ulazima wowote wala havina faida mwili, vyakula k**a chipsi, chapati, vinywaji k**a soda.... Usishindane na utandawazi, kula kawaida uijenge Afya yako
• Kunywa chai yako yenye tangawizi, mdalasini, iliki na mchaichai
K**a utaweza kupata Unga Wa Mbegu Ya Parachichi utumie.
Weka kijiko kimoja cha unga wa mbegu ya parachichi kwenye kikombe cha chai, unasaidia kuondoa tindikali mwilini kwa ndugu zangu ambao mmetumia au mnatumia sana uzazi wa mpango, sindano, p2, vidonge n.k
Weka nia, chukua hatua ndani ya wiki 3 hadi 4 uje na mrejesho wako

👉🏻 Ni changamoto gani ya uzazi ambayo mpaka sasa inakuwazisha sana na unapenda nikusaidie..? [niandikie katika comment]

K**a unasumbuliwa na changamoto za ukavu ukeni, kukosa hisia za mapenzi, kukosa ute wa uzazi, kupata dalili za mimba ila ukipima haionekani, hedhi yako kukosa mpangilio mzuri, hedhi kutoka kidogo, yenye mabonge au utelezi n.k nina Kirutubisho kizuri cha asili kinachoweza kukusaidia kuondoa changamoto hizo, kusafisha fuko la uzazi na kurekebisha mzunguko hedhi.

Nipigie Simu / WhatsApp namba 0678634046
Jifunze na Kuchukua Hatua bila Kukata Tamaa utazishinda nyakati ngumu.....

Ute wa mimba ni ute unaovutika, ni ute muhimu sana linapokuja suala la kutungwa kwa ujauzito.Ute huu ambao huvutika mith...
07/02/2022

Ute wa mimba ni ute unaovutika, ni ute muhimu sana linapokuja suala la kutungwa kwa ujauzito.

Ute huu ambao huvutika mithili ya yai husaidia mbegu kuogelea na kupenya kwenye mlango wa kizazi na kwenda kulirutubisha yai kwenye mirija.
Baadhi ya njia za uzazi wa mpango zinapelekea kukosa ute wa mimba ili usishike mimba isiyotarajiwa.

Tatizo la kukosa ute wa mimba linachangia pia uchelewe kupata ujauzito. Baadhi ya wanawake watahitaji kutumia kwanza dawa za kuongeza ute ili kushika mimba.

Ute ute laini unaovutika ni wa mhimu ili kuweka mazingira mazuri ya kushika ujauzito.

Siku chache kabla ya mimba kutungwa ute ute laini unaovutika huanza kuzalishwa kwa wingi kwenye mlango wa kizazi.

Katika ulaini wake ute huu unaleta mazingira mazuri kwa mbegu za mwanaume kuogelea kupenya mlango wa kizazi.

Changamoto yoyote kwenye ute maana yake mbegu haitapenya na mimba haitatungwa.

Tupigie tukusaidie leo 0678634046

Utafiti wa Chama Cha Madaktari Bingwa wa Akina Mama (FIGO) mwaka 1990 ulionesha kuwa sababu kuu ya mwanamke kutoshika mi...
05/02/2022

Utafiti wa Chama Cha Madaktari Bingwa wa Akina Mama (FIGO) mwaka 1990 ulionesha kuwa sababu kuu ya mwanamke kutoshika mimba ni hitilafu katika mirija ambayo kitaalam huitwa Tubal Factor ambapo asilimia 25-35 hutokana na magonjwa ya mirija ya uzazi.

Katika utafiti huo, iligundulika kuwa asilimia 30-40 husababishwa na hitilafu ya kupevuka mayai kitaalam huitwa Ovulatory Factor.

Sababu nyingine zilielezwa kuwa ni hitilafu za ukuta wa uzazi, yaani Endometriosis au mwanamke kuwa na uvimbe kwenye mji wa uzazi.

Ile sababu ya matatizo yanayosababishwa na kupevuka kwa mayai au kutotolewa kwa mayai au kutoka kidogo sana, hutokea baada ya vichocheo vinavyoitwa, Hormone ya "Godotrophins Relising Hormone" kutoka sehemu ya tezi la kwenye ubongo Ijulikanayo k**a Hythalamus kunakosababishwa na tezi kutofanya kazi vizuri.

Kwa sababu hiyo, mayai hutolewa kidogo au kutotoka kabisa na kusababisha baadhi ya wanawake kutoenda kwenye siku zao za hedhi wakati muda wa kufanya hivyo haujafika.
Sababu nyingine zinazofanya mwanamke kushindwa kushika mimba huwa ni kuziba au kuwa na upenyo mdogo wa kusafirisha mayai kutoka kwenye tezi la mfuko wa uzazi, lijulikanalo kitaalam kwa jina la O***y.

Hali hiyo ya kuwa na upenyo mdogo husababishwa na maambukizi ya bakteria kwenye mirija pamoja na mji wa mimba na tatizo hilo kitaalam huitwa Pelvic Infections au PID yanayoambatana na kutokwa na uchafu
Mwanamke akiwa na tatizo hili atajisikia maumivu makali wakati wa kufanya tendo la ndoa.
Wanawake wengine hushindwa kupata mimba kutokana na kuwa na hitilafu kwenye mji wa mimba, k**a vile kuwa na uvimbe kwenye kizazi au vinyama kuota kwenye mji huo wa uzazi Endometritis au kuwa na matatizo ya kuzaliwa nayo ya mji wa uzazi kuwa mdogo sana.
Tatizo lingine ni mwanamke kuwa na hitilafu kwenye shingo au mlango wa uzazi kitaalam huitwa Cervical Factors, k**a vile maumbile yasiyo ya kawaida, jambo ambalo husababisha usumbufu mji wa kizazi kuwa mbali na uke,
HIVYO kusababisha ucheleweshaji wa kusafirisha mbegu za kiume Sperms.
Tatizo lingine ni kuwa, kwenye mlango wa uzazi, huzalishwa utelezi mwingi ambao unaweza kuleta hitilafu katika kufanya kazi.

Kwa Mawasiliano zaidi juu ya upatikanaji wa huduma zetu tafadhali tupigie
0678634046

KARIBU

Hii Kitaalamu huitwa HYPOMENORRHEA.Usingahike na jina lake   kikubwa ujue tiba yakeAnyway, tuendelee na somoKawaida kati...
01/02/2022

Hii Kitaalamu huitwa HYPOMENORRHEA.
Usingahike na jina lake kikubwa ujue tiba yake

Anyway, tuendelee na somo
Kawaida katika mzunguko wa mwanamke hutokwa na damu ya hedhi ujazo wastani wa 30-80 mililita
Mwanamke unayepata damu ya hedhi chini ya siku 3 yani unaona hedhi kitone tu au unapata hedhi kwa siku moja tu au unaiona leo na kesho huoni mpaka kesho kutwa hilo tunasema ni tatizo
Wakati mwingine tatizo hili linaweza kukupelekea mwanamke kukosa kubeba mimba japokuwa tatizo hili sio la kukupa hofu sana lakini ni vyema kuchunguzwa na kupatiwa tiba ili kuzuia madhara makubwa yanayoweza kujitokeza baadae

SABABU ZA KUTOKWA NA DAMU CHACHE.
• KURITHI
Magonjwa au matatizo huwa yanatokana na sababu tofauti, yapo ya kuambukizwa na yapo ya kurithi, tatizo hili pia ni miongoni mwa tatizo la kurithi, endapo kwenye familia au ukoo kuna historia ya kuwa na hali hii basi vizazi vijavyo kuna uwezekano wa baadhi ya watu wakarithi, lakini mara nyingi kwa upande huu huwa haina madhara sana kiasi cha kukufanya kukosa watoto.

• Sababu ya pili ni KUKOSEKANA KWA USAWA WA HOMONI (HOMONI IMBALANSI)
Hii ndio sababu kubwa sana kwa wanawake wengi na ndio huwafanya wengi kuwa na changamoto za kukosa kubeba mimba.....Mzunguko wa hedhi wa mwanamke hutegemea homoni mbili, homoni ya estrogeni na progesterone. endapo kutakosekana usawa katika homoni hizi mbili, mwanamke huweza kuingia kwenye tatizo la mzunguko wake wa hedhi.
Progestrone hutumika kutengeneza ukuta wa ndani wa mfuko wa uzazi au mji wa mimba (uterus) ambao k**a yai lililoanguliwa na mwanamke halijakutana na mbegu za kiume, ukuta huu hubomoka na damu ya hedhi kutoka, endapo kiwango cha homoni hii kitapungua na damu ya hedhi pia hupungua. kutokana ukuta utakaotengezwa unakuwa mwembamba.
Vilevile hata homoni ya testosterone inayotolewa na mwanaume, ikiwa nyingi, huchangia kwenye tatizo hili.
• Sababu ya tatu ni Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango za kumeza ambazo huleta tatizo kwenye ukuta wa mji wa mimba na kusababisha mvurugiko wa homoni
•Hypothyroidism, ni hali ambayo tezi ya thyroid inakuwa haizalishi homoni za kutosha, hali ni miongoni mwa sababu zinazopelekea homoni kutokuwa sawa, hali hii hutokea pindi tezi kuu ya pitiutali inakuwa haifanyi kazi kisawasawa na kushindwa kuzalisha homoni ya FSH, hali hiyo husababisha mwanamke kutopata siku za kuangua mayai na kuleta hali ya kupata damu chache wakati wa hedhi.

• MATATIZO KWENYE MJI WA MIMBA,
Ujazo au utengenezwaji wa ukuta wa mimba hubadishiri kiasi cha damu ya hedhi itakayotoka, endapo sehemu hiyo ikawa na tatizo au maambukizi, upasuaji au magonjwa mengine hupelekea mtu kutokwa na damu chache ya hedhi.

• KUFANYA MAZOEZI KUPITA KIASI.
Mwanamke kufanya mazoezi kupita kiasi huweza kumsababishia hali hii, hasa wanawake wanene ambao hufanya mazoezi kwaajili ya kupunguza uzito na mafuta, mafuta yanatoka hutoka kwa hali isiyo ya kawaida, na kupelekea kusababisha au kusumbua mfumo wa uzalishaji wa homoni ambao unapelekea hali ya kutokwa na damu chache kutokea.

• MAWAZO / STRESS
Mawazo huathiri vitu vingi kwenye mfumo wetu wa maisha, mimba na hata katika mzunguko wa hedhi, mawazo ya muda mrefu huenda kuzuia uzalishwaji wa homoni ya luteinizing.

MATIBABU.
Matitabu ya tatizo hili hutegemea na kilichosababisha, hivyo kwenda hospitali na kufanya vipimo mapema ni jambo jema zaidi ili kuweza kujua tatizo kwa kina na kutibiwa k**a litahitaji tiba. kumbuka magonjwa mengi ya uzazi na ovari kwa ujumla huweza kupelekea tatizo hili kwa asilimia kubwa.

Hapa chini nakukumbusha TIBA RAHISI YA KUTIBU TATIZO LA MVURUGIKO WA HOMONI/HEDHI
K**a unapitia changamoto za kukosa hisia, kukosa ute wa uzazi, kuwa mkavu sana wakati wa tendo, hedhi kutoka ikiwa na utelezi au mabonge, maziwa kujaa, hedhi kukosa mpangilio....Nenda maduka ya dawa za asili (lishe)...Chukua
• Unga wa Mrehani [basil leaves powder] robo kilo
• Unga wa habat sawda (black seed), robo kilo
• Unga wa mbegu za uwatu (fenugreek) robo kilo na Unga wa mizizi ya Mkunde pori robo kilo.
Utachanganya kwa pamoja dawa hizi kwenye bakuli moja, uwe unatumia unga wa mchanganyiko wa dawa hizi kijiko kidogo kimoja kwenye chai, uji, au maji moto tumia mara tatu kwa siku, kwa wiki 3 mpk 4 utapona changamoto za homoni
Ni hayo nilokuandalia kwa leo...

K**a bado una changamoto yoyote ya uzazi tunayo tiba ya uhakika na utapona kabisa piga simu 0678634046

K**a unatibu U.T.I au Fangasi ila baada ya kushiriki tendo na mume unapata dalili tena za miwasho na U.T.I inawezekana t...
31/01/2022

K**a unatibu U.T.I au Fangasi ila baada ya kushiriki tendo na mume unapata dalili tena za miwasho na U.T.I inawezekana tatizo likawa linaanzia kwa mwenzio.

Jitahidi kumuandalia dawa ya kumuondolea U.T.I pia, it is very simple
Unachukua kijiko kidogo cha baking soda unatia kwenye kikombe cha maji, kisha unakamulia limao.... Anakunywa kila siku kwa siku 7 infection inamuisha kabisa
K**a kwako Fangasi na P.I.D limekuwa tatizo sugu fanya hivi

ANDAA
• unga wa maganda ya parachichi vijiko 2
• unga wa mbegu za mlonge vijiko 2
• unga wa maganda ya ndizi [mbichi/mbivu] vijiko 2
• unga wa habat soda vijiko 2
• unga wa kitunguu swaumu vijiko 2
• unga wa uwatu vijiko 2 [vitu hivi unaweza kuandaa mwenyewe au kuvitafuta katika maduka ya tiba asili]
Utachanganya dawa hizi kwa pamoja kwenye sufuria au kontena kisha mimina ASALI taratibu huku ukikoroga mpaka lita nzima iishe k**a una blenda unaweza kutumia ili ikusaidie kuikoroga vizuri

* MATUMIZI
Utalamba vijiko viwili vya dawa asubuhi, mchana na jioni k**a huna muda mchana basi tumia vijiko vitatu asubuhi na vijiko vitatu usiku…. Mfululizo kwa siku 14 mpaka 21 utakuja kunipa mrejesho wako

Ikiwa Bado unahangaika na Fangasi sugu, miwasho sugu, pamoja na UTI basi usihangaike sana tupigie simu sasa hivi 0678634046 tutakupa tiba na utapona kabisa.

Inakadiriwa asilimia 70 mpaka 80 ya wanawake wanaweza kupatwa na ugonjwa huu katika safari yao ya kuishi.Vile vile si kw...
30/01/2022

Inakadiriwa asilimia 70 mpaka 80 ya wanawake wanaweza kupatwa na ugonjwa huu katika safari yao ya kuishi.

Vile vile si kweli kwamba ni upasuwaji tu ndiyo njia pekee ya uhakika ya kutibu uvimbe kwenye kizazi.

Zipo dawa rafiki zinazoweza kutumika na ukapona bila kulazimika kufanya upasuwaji.

Fanya mambo haya ujikinge na tatizo hili.
1. Weka sawa homoni zako
Ili kuepuka kupata uvimbe kwenye mji wako wa uzazi unahitajika kuhakikisha homozi zako zipo sawa kila mara.
2. Dhibiti uzito wako

Tabia zifuatazo zitakusaidia kupunguza uzito wako;
• Kupunguza kiasi cha chakula unachokula,
• Kufunga kula mara kwa mara,
• Kupunguza kukaa chini au kwenye kiti masaa mengi, na
• Mazoezi ya viungo ya mara kwa mara

3. Acha baadhi ya vipodozi
Losheni, krimu na vipodozi vingi vya dukani vina kemikali ambazo zinaweza kuuingia mwili wako kirahisi kupitia ngozi yako na kukuletea wewe usawa usio sawa wa homoni (endocrine imbalance) na uwezekano mkubwa wa kupatwa na uvimbe kwenye kizazi.

4. Weka sawa shinikizo lako la juu la damu

Tafiti nyingi zinathibitisha kwamba wanawake wanaoumwa shinikizo la juu la damu wanapatwa kirahisi zaidi pia tatizo la uvimbe kwenye kizazi.

5. Utaacha kula nyama nyekundu ikiwemo nyama choma na mishikaki

6. Utaacha pia vilevi vyote

TUNAKUSAIDIAJE?
K**a una uvimbe kwenye kizazi tunayo tiba na uvimbe utaisha Tupigie simu 0678634046

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dafu Wellness posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share