13/03/2022
*Ugonjwa wa Kisukari wa Figo*
*Ugonjwa wa figo unaoletwa na kisukari*
Idadi ya wagonjwa wa kisukari(diabetes)inaongezeka kwa kasi mno,ulimwenguni kote.Tatizo kuu ni ongezeko la ugonjwa wa figo unaosababishwa na ugonjwa wa kisukari. Ugonjwa wa figo unaoletwa na kisukari ni moja ya matokeo mabaya sana ya kisukari na huleta vifo vingi.
Ugonjwa wa figo wa kisukari ni upi?
vya figo kuharibika.Vinapoharibika, protini hupotea kwenye mkojo. Hali hii nayo husababisha shinikizo la damu (hypertension) , mwili kuvimba na figo kuanza kudhoofika. Mwisho figo hushindwa kufanya kazi (ESKD). Huu ndio ugonjwa wa figo wa kisukari (Diabetic nephropathy).
Kwa nini ni muhimu kujua kuhusu ugonjwa wa figo unaotokana na kisukari?
• Ugonjwa wa kisukari unaongezeka kwa kasi kubwa mno duniani kote.
• Ugonjwa huu ndio chanzo kikuu cha ugonjwa sugu wa figo.
• Wagonjwa k**a asilimia arobaini hadi hamsini walio katika kipindi cha mwisho cha ugonjwa wa figo(ESKD) ni wagonjwa wa kisukari.
• Ugonjwa wa figo unahitaji tiba ya gharama kubwa kutibiwa na watu wengi katika nchi zinazoendelea hawawezi kugharamia.
• Utambuzi na matibabu ya mapema yanaweza kuzuia ugonjwa wa figo. Kwa wenye kisukari ambao wana ugonjwa sugu wa figo, matibabu ya mapema huhairisha haja ya dayalisisi au kupatiwa figo.
• Ugonjwa wa figo wa kisukari huongeza hatari ya kufa kutokana na matatizo ya moyo.
• Hivyo utambuzi wa mapema wa ugonjwa huu wa figo unaotokana na kisukari ni muhimu sana.
Ugonjwa wa kisukari ndio mara nyingi husababisha ugonjwa sugu wa figo.
Ni wagonjwa wangapi wa kisukari hupata ugonjwa wa figo?
Ugonjwa wa kisukari ni wa aina mbili. Lakini kila aina ina hatari yake ya kusababisha ugonjwa wa figo.
Aina ya ugonjwa wa kisukari unaohitaji dawa ya insulin (Aina 1)
Aina ya kwanza (Type -1) huanza mtu akiwa na umri mdogo na huhitaji dawa ili kuuthibiti . Aslimia 30 - 35 ya walio na aina hii hupata ugonjwa wa figo.
Aina ya ugonjwa wa kisukari usiotegemea insulin (Aina 2)
Aina ya -2 ya kisukari sana sana huwapata watu wazima na mara nyingine huweza kuthibitiwa bila insulin. Asilimia 10- 40 ya wagonjwa wa aina hii ya kisukari huenda wakapata ugonjwa wa figo.Aina hii ya pili ndio chanzo kikuu cha ugonjwa wa figo usiopona. Mtu mmoja kati ya wagonjwa wapya watatu hupata shida hii.
Ni mgonjwa yupi wa kisukari anaweza kupata ugonjwa wa figo?
Ni vigumu kujua mgonjwa yupi aliye katika hatari zaidi ya kuupata ugonjwa wa figo,ingawaje kuna ishara zinazoashiria k**a:
Kisukari ni chanzo kikuu cha ugonjwa wa figo ulio katika hatua ya mwisho, mgonjwa mmoja kati ya watatu huwa na shida hiyo.
• Mtu kapata aina ya kwanza ya kisukari kabla ya kufikisha umri wa miaka ishirini.
• Ugonjwa wa kisukari usiotibiwa vizuri.( kiasi cha juu cha HbA1c)
• Shinikizo la damu lisilotibiwa/lisilodhibitiwa vizuri.
• Historia ya kisukari kwenye familia na hasa ikiambatana na ugonjwa sugu wa figo.
• Matatizo ya macho.(diabetic retinopathy), au uaribifu /tatizo la neve kwa sababu ya kisukari (diabetic neuropathy).
• Protini kwenye mkojo,uzito mkubwa,uvutaji wa sigara na ongezeko la mafuta kwenye damu.
Ugonjwa wa figo huanza lini kwa mgonjwa wa kisukari?
Ugonjwa sugu wa figo huchukua muda mrefu kwa hiyo ni vigumu kuupata katika miaka kumi ya kwanza ya kisukari. Dalili huonekana k**a miaka kumi na mitano hadi ishirini baada ya aina ya kwanza ya kisukari kuanza.
Iwapo mgonjwa wa kisukari hajapata ugonjwa wa figo baada ya miaka ishirini na mitano,basi hatari ya kuupata hupungua.
Je ni lini mgonjwa wa kisukari anaweza kuwa na ugonjwa wa figo:
• Anapokojoa mkojo wenye povu au kuna protini kwenye mkojo akipimwa.
• Anapopata shinikizo la damu au k**a alikuwa na shinikizo la damu basi hali hiyo kuzidi kuwa mbaya.
• Vifundo vya miguu, miguu na uso kuvimba, mkojo kupungua na uzito wa mwili kuongezeka.
Dalili za madhara ya kisukari huwa ni protini kwenye mkojo unapopimwa, shinikizo la damu na kuvimba mwili.
• Kupungua mahitaji ya dawa ya insulin na dawa nyingine zinazotumika kutibu kisukari.
• Mgonjwa ambaye ghafla anakuwa na historia ya kuhitaji kipimo cha dawa kidogo kuiweka sukari yake kuwa chini.
• Historia ya mgonjwa kuwa na matukio ya kisukari mwilini kushuka. Aidha kusaidiwa na dawa za kisukari ambazo hapo awali zilikuwa hazimsaidii.
• Mgonjwa kujihisi vyema hata bila kutumia dawa.Wagonjwa wengi hufurahi kupona kisukari lakini ukweli ni kwamba figo za mgonjwa sasa huwa zinazidi kudhoofika.
• Dalili za ugonjwa sugu wa figo huanza kuonekana; k**a vile uchovu/kuchoka, kukosa hamu ya chakula, kichefuchefu, kutapika, kujikuna, kuonekana mgonjwa mgonjwa, na kushindwa kupumua.Hizi ni dalili ambazo huonekana ugonjwa ukiwa umeendelea zaidi.
• Vipimo vya kreatinini na yurea huwa juu katika damu.
Je,ugonjwa wa figo unaoletwa na kisukari hujulikanaje na ni uchunguzi upi unaweza kuutambua mapema?
Vipimo viwili ambavyo ni muhimu sana ni kile cha protini kwenye mkojo na kreatinini kwenye damu. Kipimo cha kwanza ambacho huweza kutambua ugonjwa huu wa figo,mapema ni kile kinachoweza kuonyesha kiasi kidogo kabisa cha albumin kwenye mkojo. Albumini ni aina ya protini k**a ile inayopatikana katika uteyai.
Kipimo kingine ni kile cha kawaida kinachoonyesha uwepo wa albumin nyingi kwenye mkojo.
Kipimo cha kreatinini ndicho huonyesha kazi inayofanywa na figo. Kiasi cha kreatinini huongezeka kwenye damu katika kipindi cha mwisho, yaani ugonjwa ukiwa umekomaa sana.
ONYO:K**a sukari katika damu inashuka mara kwa mara au kisukari kinajidhibiti bila dawa, ni muhimu ufikirie uwepo wa ugonjwa wa figo
What's up call/ 0755467415
au bonyeza link kuja whatsap
https://wa.me/255755467415