Sauti ya Mtaa

Sauti ya Mtaa "Karibu kwenye [Fundikira Marriale]! 🌟 Hapa tunakuletea tarifa mbalimbali taarifa za kuelimisha, furaha ya kila siku, au safari za mafanikio].

Jiunge nasi katika safari hii.

KUNA BUNDI DHIDI YA UPEPO NA TAARIFA ZISIZOTHIBITISHWA KUHUSU AFYA YA 'Tundu Lissu';Askofu wa Chadema Tanzania, Tarehe 1...
20/05/2026

KUNA BUNDI DHIDI YA UPEPO NA TAARIFA ZISIZOTHIBITISHWA KUHUSU AFYA YA 'Tundu Lissu';
Askofu wa Chadema Tanzania, Tarehe 18 May 2026 saa 07:30hrs akiwa Itunge Dar Es Salaam kwenye account ya Facebook Emmaus Bandekile Mwamakula, Alichapisha taarifa yenye kichwa 'ASKOFU ATOA KAULI JUU YA AFYA YA LISSU!').
Nipo tofauti na Askofu, kwani Katika nyakati ambazo jamii inahitaji utulivu, busara na ukweli, baadhi ya watu k**a Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula, John Heche nk! wameendelea kutumia majukwaa yao kueneza simulizi za hofu, taharuki na mashaka bila ushahidi wa moja kwa moja na kufanya sisi jamii tujielekeze kwenye Maswali. Kauli ya Emmaus Bandekile Mwamakula kuhusu afya ya Tundu Lissu imeibua maswali mengi kuliko majibu.

Swali kubwa ambalo jamii inapaswa kujiuliza ni hili:
Ni kwa nini taarifa nyeti k**a hizi zitolewe kwa hisia kali, tuhuma nzito na lugha ya kuashiria njama kabla ya kuthibitishwa rasmi na madaktari au mamlaka husika?
Kwa mujibu wa simulizi hiyo, John Heche anadai mbele ya jukwaa kupigiwa simu na ndugu wa Lissu aitwaye Vicent Lissu kuhusu maumivu ya tumbo 'Hakutaja alipiwa tarehe ngapi! mwezi gani! Mwaka gani! Saa ngapi?. Lakini ghafla, bila ripoti ya kitabibu, bila uchunguzi wa daktari, bila ushahidi wa maabara simulizi linaanza kugeuzwa kuwa “Sumu”, “Njama”, na mazingira ya kisiasa. (Hawa wanataka kuaminisha nini na kwa maslahi gani?.

Hapa ndipo jamii inapaswa kuwa makini.
Maumivu ya tumbo si ushahidi wa sumu. Binadamu anaweza kuumwa kwa sababu nyingi za kawaida kabisa. Lakini unapochukua taarifa ambayo haijathibitishwa kisha ukaijenga kwa lugha ya hofu, machozi, taharuki na lawama za kisiasa, unakuwa hutafuti ukweli tena unatengeneza huruma ya kuchochea hisia kwa jamii.

Kinachoshangaza zaidi ni namna kauli hiyo ilivyojaa, lawama za mapema na hukumu kabla ya uthibitisho. Mdomo huponza kichwa; Hii ndiyo mbinu inayotumika mara nyingi kwenye propaganda za kisiasa; kuanzisha hisia kwanza, ushahidi baadaye. 'Kwanza watu waogope' Kwanza jamii ichukie. 'Kwanza wananchi waamini kuna “mkono wa siri”. Halafu baadaye ukweli uje ukiwa umechelewa.

Hata hivyo jamii tunao ushahidi wa Post za askofu huyuhuyu 'Kushadadia asiyo yajua' aliyoongea baada ya tukio la mwanafunzi wa IFM Kukatwa kichwa! lakini baada ya watuhumiwa kuk**atwa aibu anajisikia yeye mbele ya jamii. Mzee 'mdomo huponza kichwa' wapo watu wanayakusema lakini kwa busara zao hunyamaza! kwakuwa wewe umeumbwa kusema sema mambo yenye mantiki,udhibitisho wakimamlaka.

Watanzania wanapaswa kuelewa kuwa taasisi k**a Jeshi la Magereza Tanzania zina wajibu wa kisheria wa kuhakikisha usalama wa mahabusu na wafungwa. Tuhuma nzito k**a “kupewa sumu” haziwezi kutolewa kwa hisia, kwa presha za kisiasa au kwa maneno ya kusisimua mitandao bila ushahidi wa kitaalamu. Emmaus Bandekile Mwamakula

SIASA ZA KUCHOKOZA VYOMBO VYA DOLA AU MKAKATI WA KUTAFUTA HURUMA YA KISIASA?Kuna maswali mengi ya kujiuliza baada ya baa...
19/05/2026

SIASA ZA KUCHOKOZA VYOMBO VYA DOLA AU MKAKATI WA KUTAFUTA HURUMA YA KISIASA?
Kuna maswali mengi ya kujiuliza baada ya baadhi ya wanachama wa Chama Chadema Tanzania kwenda kuweka bendera ya chama nje ya kituo cha Polisi huku wakijua wazi mazingira ya kiusalama na taratibu za maeneo hayo nyeti. Je, hili lilikuwa tukio la kawaida la kisiasa, au kulikuwa na dhamira iliyojificha nyuma yake?

Kwa nini mtu aamue kufanya tukio la kisiasa eneo ambalo ni wazi linaweza kusababisha tahadhari au hatua za kiusalama? Je, walikuwa wanatafuta makabiliano ya makusudi ili baadaye wajenge simulizi ya kisiasa kuwa wameonewa? Haya ni maswali ambayo wananchi wengi wanaanza kujiuliza.

Inawezekana kabisa huu ukawa mkakati wa kutengeneza “kick” za kisiasa kupitia matukio ya kuvutana na vyombo vya dola. Katika siasa za kisasa, baadhi ya makundi huamini kuwa kuk**atwa au kuzuiwa huweza kuwajengea umaarufu, huruma ya wananchi, au ajenda mpya kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari. Je, hili ndilo lililokuwa linatafutwa?

Swali jingine la msingi ni hili; nani anafadhili aina hii ya siasa za uchokozi? Kwa sababu si rahisi kufanya matukio yenye viashiria vya kuvuruga utulivu bila kuwa na malengo makubwa ya kisiasa nyuma yake. Je, kuna watu wanaotaka kuona hali ya taharuki ikiongezeka ili wapate nafasi ya kuhamasisha maandamano au migogoro ya kisiasa?

Wananchi wengi wanahitaji siasa za hoja, sera na ushindani wa kistaarabu, si siasa za kujaribu kuchokoza mamlaka ili kutengeneza taharuki. Tanzania imejijenga katika misingi ya amani, na ni wajibu wa kila chama cha siasa kuhakikisha hakitumii mbinu zinazoweza kuleta taharuki au kuigawa jamii kwa manufaa ya kisiasa.

Mwisho wa yote, maswali yataendelea kubaki: Je, hili lilikuwa tukio la kawaida la kisiasa, au ilikuwa ni njia ya kutengeneza mazingira ya migongano kwa maslahi ya kisiasa? Wananchi wanatazama, wanachambua, na wanahitaji majibu ya kweli.

🚨 CHADEMA MNAJIFIFISHA WENYEWE:  AFRIKA INAHITAJI MAENDELEO YA VITENDO, SI DEMOKRASIA YA KELELE 🚨CHADEMA; Majukwaa yenu ...
09/05/2026

🚨 CHADEMA MNAJIFIFISHA WENYEWE: AFRIKA INAHITAJI MAENDELEO YA VITENDO, SI DEMOKRASIA YA KELELE 🚨
CHADEMA; Majukwaa yenu haya akisi maisha halisi ya Mtanzania,alivyozaliwa kwenye ardhi hii alivyolelewa na aina ya matendo aliyofundishwa ki asili kwa Makuzi ya mazingira yetu; Kwanini nasema hivi Mikutano yenu inafanya mtoto anayekuwa leo asielewe maana halisi ya Demokrasia halisi ya maeneo yake, bali afikiri Demokrasia ya huko ulimwengu mwingine ndio yetu! 'Msituletee mambo yasiyo kwenye utamaduni wetu'

Nchi yetu! tumelelewa katika kuweka mbele nidhamu, mipango ya muda mrefu na maendeleo kuliko siasa za kelele zisizo na tija,zenye vurugu, kejeli,Matusi,ushawishi,Uchonganishi na chuki.

CHADEMA; Nawakumbusha kuwa, CHINA hawakujenga uchumi mkubwa duniani kwa vurugu za kisiasa kila siku, bali kwa sera za taifa zinazodumu kwa miongo. Dubai nayo imeonyesha kuwa uongozi wenye maamuzi na dira unaweza kuifanya nchi kuwa kitovu cha dunia kwa biashara na maendeleo. Wanufaika ni wapinzani na wasio wapinzani sasa nyie Chadema kusudi lenu ni lipi!

Afrika haiwezi kuendelea kwa maandamano yasiyoisha, matusi ya kisiasa na migogoro ya kila uchaguzi. Tunahitaji siasa za kazi, uzalishaji, nidhamu na viongozi wenye maamuzi ya maendeleo.

Ukiangalia mikutano mingi ya chadema, maneno yao nchi nzima yanafanana, ni free Tundu lissu na michango je? hakuna hoja za Msingi “Taifa halijengwi kwa kelele nyingi, linajengwa kwa dira, nidhamu na utekelezaji.” Vijana wa Afrika waweke mbele elimu, uchumi, teknolojia na uzalishaji kuliko siasa za migawanyiko zisizo na mwisho.









📌
📌
📌
📌

IGP Camilius Wambura Ahimiza Mazoezi kwa Askari na Ushirikiano wa Jamii Katika Kupambana na Uhalifu.Mkuu wa Jeshi la Pol...
07/05/2026

IGP Camilius Wambura Ahimiza Mazoezi kwa Askari na Ushirikiano wa Jamii Katika Kupambana na Uhalifu.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Camilius Wambura, ametoa msisitizo kwa askari wa Jeshi la Polisi kuimarisha mazoezi ya mwili k**a sehemu ya msingi ya utendaji wao wa kila siku, akibainisha kuwa afya bora na stamina imara ni nguzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu yao.

Amesema kuwa askari wenye afya njema wana uwezo mkubwa wa kukabiliana na changamoto zozote zikiwepo pia hata katika Maisha binafsi, hususan katika mazingira yanayohitaji wepesi wa kimwili, umakini na uvumilivu wa hali ya juu. Amesisitiza kuwa mazoezi siyo tu kwa ajili ya mwili, bali pia ni njia ya kujenga nidhamu, uthabiti wa kisaikolojia na moyo wa kizalendo.

Aidha, ametoa wito kwa askari kuimarisha ushirikiano wa karibu na jamii, akieleza kuwa mapambano dhidi ya uhalifu hayawezi kufanikiwa bila wananchi kushiriki kikamilifu. Amesema polisi wanapaswa kuwa karibu na wananchi, kusikiliza changamoto zao na kujenga nao nia Moja ya kutekeleza uzalendo wao na shughuli zao zinazowapatia vipato vya kila siku.

🔴 LARRY MADOVO,MANGE KIMAMBI,MARIA SARUNGI, HAWAPO TANZANIA: Kuna mstari ambao jamii hatupaswi kuuvuka, Mstari wa kulind...
17/04/2026

🔴 LARRY MADOVO,MANGE KIMAMBI,MARIA SARUNGI, HAWAPO TANZANIA: Kuna mstari ambao jamii hatupaswi kuuvuka, Mstari wa kulinda mshik**ano wa taifa letu 🇹anzania, sisi wenyewe tusihadaiwe na waliopo mbali nasi. Nimeona post ya LARRY MADOVO, Mjaluo wa Kenya asili yake Magharibi mwa Ziwa Victoria, akiwa na MANGE KIMAMBI Huyu ni Mtanzania Mpare mwenye asili ya Mwanga-Kilimanjaro, Lakini yupo mafichoni Marekani: Post ile iko na kejeli na maneno ya dhihaka: Hawa wana ajenda zisizonjema, Sio kila anayezungumza kwa sauti kubwa kuhusu maendeleo yenu na mamlaka zetu ana nia njema, Ni kuongeza mgawanyiko, hasira na chuki miongoni mwa wananchi, tusiwaache watupande kichwani hawa.
Larry Madowo na Maria Sarungi kuna mahusiano ya urafiki na kabila luo Tanzani na Luo Kenya na kwasasa Maria Sarungi anaishi Kenya nchi ya kina Larry Madovo; Maria Sarungi Kenya yupo mafichoni Ikiwa yeye ni Mtanzania, Ila Larry Madovo anaingia Tanzania kwa kutokea Kenya alipo Maria Sarungi, hata hivyo Mange Kimambi yupo Marekani ambako anakutana pia na Larry Madovo ambae anatokea Kenya.
Neno ni moja tu sisi tunapenda utulivu na amani tufanye kazi zetu bila vurugu na migawanyiko, nyie hamko Tanzania sisi tupo huku na wala hamuwezi kuwa na huruma na sisi, msituletee umamluki kwenye Masikio yetu. Tanzania imejengwa juu ya misingi ya umoja, heshima na amani. Haya siyo maneno tu,ni urithi wetu.

CHADEMA: ACHENI KUJARIBU SERKALI NA KU SHINIKIZA HATUA ZA MAHAKAMA: John Heche, Golugwa! Chadema ni Chama kilichopo ndan...
12/04/2026

CHADEMA: ACHENI KUJARIBU SERKALI NA KU SHINIKIZA HATUA ZA MAHAKAMA:
John Heche, Golugwa! Chadema ni Chama kilichopo ndani ya nchi yenye Misingi yake!; Eleweni hii si siasa ni sheria TUNDU LISSU kuwepo hadi leo Mahabusu sio takwa la mtu ni sheria ('MSIDANGANYE WATU,MSITUPOTOSHE',). Zipo kanuni na taratibu zinazolinda nchi, Serikali inaongoza kwa sheria, si kwa huruma ya kisiasa wala umaarufu wa mtu, ndiyo maana tuna amani hadi leo.

LISSU: Aonewe huruma kwa lipi? Kwani yupo Gerezani kwa fumanizi au bahati Mbaya? Si yupo kwa Makusudi yake ya kujipa umwamba na kujaribu kuruka kanuni,taratibu na sheria zilizopo!!! Mahak**a si ndio inaamua, Sasa nyie Chadema wakina nani nyie ni mahak**a au Mungu?. Why Lissu pekee!! Je unawazungumzia je, Mahabusu wengine waliopo gerezani wasio maarufu, wagonjwa wa Kansa,Ukimwi,Tb,Ulemavu,Stroke ? Acheni ubinafsi wa kutaka sheria iwe na upendeleo;

Au huruma ni kwa anayejulikana tu? Hapo haki iko wapi, kwa wote au kwa wachache? K**a kila kiongozi akishinikiza watu wake waachiwe, mfumo wa sheria utabaki wapi? Heche muwe mnawaza, maswali ya msingi unayopaswa kuyajibu kabla ya kuhamasisha watu kuvunja taratibu.

Lissu ni mtuhumiwa k**a watuhumiwa wengine tofauti yake ni umaarufu, sio hadhi mbele ya sheria. Kumuweka juu ya mfumo wa sheria ni kuleta ubaguzi usiokubalika katika haki. Amani iliyopo leo ipo kwa sababu sheria inasimamiwa sio kwa sababu ya mashinikizo ya kisiasa. Chadema Acheni mahak**a ifanye kazi yake bila kuingiliwa, hiyo ndiyo njia pekee ya haki ya kweli.

🔴 TAHADHARI KUBWA: UTAPELI WA MITANDAONI 🔴NICODEMUS JULIAS LOYORE NAMBA 0791262588; Acha janja janja wengine born town k...
04/03/2026

🔴 TAHADHARI KUBWA: UTAPELI WA MITANDAONI 🔴
NICODEMUS JULIAS LOYORE NAMBA 0791262588; Acha janja janja wengine born town kitambo, acha kutaka pesa kirahisi na usiwe na masihara na fedha za walimwengu wanaotafuta fedha kwa jasho na mazingira mengine magumu! Umejitakia kwa kutaka umaarufu wa kijinga 'Kutukana, kushawishi, umetishia, umetia hofu jamii, kukejeli na kukebehi watu wasio na makosa na wewe'; Umeyafanya hayo wazi ulionywa na familia, Mke, Muajiri; Lakini hukutaka kuona hatari yake mbele sasa aibu inakukuta wewe mwenyewe; Mke kakukimbia, ajira umefukuzwa, jamaa na marafiki hawana time na wewe kwa kujitakia; Pambana na hali yako na ujinga wako.

Ni muhimu kuchukua tahadhari kubwa dhidi ya wimbi la utapeli linaloendelea kwenye mitandao ya kijamii. Kumekuwa na tabia hatari ya baadhi ya watu kueneza simulizi za kutaka huruma au msaada wa kifedha bila uthibitisho wowote wa ukweli. Wengine hufikia hatua ya kutengeneza au kukuza matatizo yao makusudi ili baadaye waombe msaada, jambo ambalo si tu ni udanganyifu bali pia ni kuchezea akili na hisia za watu wanaotafuta maisha kwa uhalali.

Ni vyema na lazima tukumbuke kuwa 'pesa ni ngumu sana kuipata. Haikubaliki mtu achukue fedha yako kirahisi kwa kutumia ushawishi wa kihisia au taarifa zisizo rasmi. Kabla hujatuma pesa kwa mtu yeyote uliyemkuta mtandaoni, jiulize: Je, taarifa hii imethibitishwa? Je, huyu mtu ni wa kuaminika? Kwa nini kuna haraka au shinikizo la kutuma pesa? Huyu alijitakia au yalimkuta ghafla? Nani wanashinikiza zaidi wana sifa gani kwetu au ni wale ambao nao wanataka kesho wachangiwe?

Aidha, ni vyema pia sisi jamii tukaacha kabisa tabia ya kutetea watu wanaojitakia matatizo na kuona kuna urahisi wa kupata fedha. kutengeneza matatizo ili kupata huruma au msaada wa kifedha. Vitendo hivi vina madhara makubwa, si tu kwa wahusika bali pia kwa familia zao na watu wanaowazunguka. Mwisho wa siku, mtu hujikuta amejiingiza kwenye matatizo makubwa zaidi kijamii, kifamilia na hata kisheria.
Tusikubali kudanganywa wala kutumiwa k**a njia ya watu wengine kujipatia fedha kwa njia zisizo halali.
🧠 Linda akili yako
🔍 Chunguza kabla ya kuamini
🚫 Usitume pesa bila uhakika

Mzee wa 'TFF VIPI TENA'  Ulionywa sana. Inaonekana sasa umebaki peke yako, kwa sababu jamii ilishakutambua na kuchukua t...
20/02/2026

Mzee wa 'TFF VIPI TENA' Ulionywa sana. Inaonekana sasa umebaki peke yako, kwa sababu jamii ilishakutambua na kuchukua tahadhari mapema kabla hata ya wale unaowapotosha hawajakurudia. Hii ni ishara tosha kuwa watu wameanza kuelewa mbinu zako na athari zake. Ni muhimu kutambua kuwa ushawishi hasi una mwisho wake, na mara nyingi huacha mtu akiwa amebeba lawama peke yake.

Acha ujinga. Sifa za kijinga siku zote huzaa majuto. Hiki ni kipindi cha vijana kujituma, kufanya kazi na kutafuta maendeleo yao halali sio kukaa mitandaoni kusikiliza upotoshaji usio na tija. K**a wanavyosema wana wa Elephant, “usiwauzie mbuzi kwenye gunia.” Ukweli unaonekana wazi, na vijana wengi hawapo tayari tena kudanganywa au kupotezewa muda wao wa kujenga maisha.

Kumbuka pia, ahadi hewa hazina msaada wa kweli. Yule unayedhani atakusaidia, kesho anaweza kuwa wa kwanza kukugeuka na kukudai ushahidi wa mateso yako. Huu si mchezo ni maisha halisi. Acha upotoshaji, acha uoropokaji, acha kutukana watu. Mwisho wa yote, utatubu tu kwa sababu ukweli haukwepeki. ✅

CHADEMA; Kesi za uhaini huwa na uzito wa kipekee kwa sababu zinagusa moja kwa moja dhana ya usalama wa taifa na uthabiti...
11/02/2026

CHADEMA; Kesi za uhaini huwa na uzito wa kipekee kwa sababu zinagusa moja kwa moja dhana ya usalama wa taifa na uthabiti wa dola. Ndiyo maana kila hatua ya mahak**a huchunguzwa kwa umakini mkubwa na jamii, wanasiasa na taasisi mbalimbali.

Kwa mtazamo wa nadharia za siasa, changamoto hujitokeza pale ambapo chama cha siasa kinahamisha mkazo kutoka siasa za taasisi kwenda siasa za harakati (movement politics). Siasa za harakati mara nyingi hutumia lugha kali, msisimko wa umma na mobilization ya kihisia k**a nyenzo ya kushinikiza mabadiliko. Tatizo linaanza pale ambapo kauli au mikakati hiyo inapotafsiriwa na dola k**a inayovuka mipaka ya ushindani wa kawaida wa kisiasa na kuingia katika eneo linalogusa utulivu wa jamii.

Katika mazingira ambayo jamii imejengwa katika misingi ya amani na utulivu, vyombo vya dola vina wajibu wa kikatiba wa kuzuia hali yoyote inayoweza kusababisha taharuki, migawanyiko au purukushani. Hivyo, matamshi ya viongozi wa kisiasa yanapokuwa na tafsiri tata au yenye ukali wa juu, taasisi za dola hujiona zinalazimika kuchukua tahadhari mapema.

Kwa mantiki hiyo, hatua za kisheria zinazoonekana leo zinaweza kutazamwa k**a sehemu ya mkakati mpana wa dola kulinda utulivu wa kijamii, hasa katika mazingira ambayo mijadala ya kisiasa imekuwa ya juu na yenye hisia kali. Kwa upande mwingine, hili pia linarejesha mjadala muhimu kuhusu mipaka kati ya uhuru wa kisiasa na wajibu wa kulinda amani ya umma.

Kwa hiyo, kinachoonekana si tu kesi ya mtu binafsi, bali ni mvutano wa kimfumo kati ya siasa za harakati na siasa za taasisi ambapo dola inasisitiza utaratibu na uthabiti, huku wanasiasa wakijaribu kusukuma ajenda zao kwa kasi ya juu.

Mwisho wa siku, mizani kati ya uhuru wa kisiasa na usalama wa jamii ndiyo itakayoamua mwelekeo wa mjadala huu mbele ya jamii inayothamini utulivu na ustaarabu.

12/01/2026

TUWE MAKINI NA UCHANGISHAJI WA FEDHA KIHOLELA MTANDAONI
Lipo wimbi la watu kusambaza ujumbe wa “tusimame na fulani” bila idhini ya mamlaka.
Hii ni hatari sana kwa sababu:

✔️ Asilimia 60%–80% ya michango ya mitandaoni isiyothibitishwa hutumika kwenye utapeli.
✔️ Hakuna anayethibitisha ukweli wa taarifa.
✔️ Namba za simu ni rahisi kuficha na matapeli hutoweka mara moja.
✔️ Wengine hutengeneza video za huruma ili kuchota fedha kwa kisingizio cha ukimbizi wa kisiasa.

📌 MIFANO“Tusimame na Cherry pamoja na mumewe… tuma mchango wako 0754930411 jina Nuru Masunga… wametoroka nchi kwa tishio la kuuawa…” Je!
Baadaye ikabainika kuwa mbinu ya kutengeneza kipato kwa kisingizio cha hatari ya kisiasa, nani wa kulaumiwa! Ikiwa ushachanga! Huyu anajulikana ni chama gani na anatoka wapi?

🚨 TURUDI NYUMA; Hiyo namba niyanani? Uhusiano wake na Mhusika upo je?. Ninachoweza kushauri kila mtu anapotoa shilingi kumi yako jiridhishe.
Mitandao imejaa watu wanaocheza na huruma za wananchi ili kutapeli.
Linda pesa zako. Linda usalama wako.

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sauti ya Mtaa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share