17/05/2025
BADILISHA WATU WANAOKUZUNGUKA INAWEZEKANA UNABEBA UOGA WAO!
Kuna watu wengi ambao wana uwezo wa kufanikiwa na wapo katika mazingira ya kufanikiwa lakini kila wanapoweka mawazo yao mezani yanakutana na maoni k**a huwezi kufanikiwa hapa watu ni wakabila sana, hapa hakuna mtu wa kununua kitu flani, unaona kila mtu anafungabiashara, ukianza tu TRA wanakumaliza, huwezi kufanikiwa mtu k**a wewe, ajira na Biashara wapi na wapi?
Lakini ukweli nikuwa wametumia muda wao mwingi katika kuwaza namna ya kushindwa, kuwaza watu walioshindwa kuliko kuwaza namna ya kuweza.
Hali hii huwajengea uoga na kujiona wanapata hasara kila wakati, wanazidumaza akili zao kwakushindwa kufikiria ni namna gani wanaweza kupambana na changamoto na kujikita katika kuacha kufanya kitu kabisa.
K**a uko katika hali hii basi SASA hembu badilisha aina ya watu wanaokuzunguka, badilisha watu wa kuwaambia malengo yao kwani kuna watu watakujaza uoga wao. Hata k**a ni mume wako, hata k**a ni mke wako k**a anaishia kukuambia tu kuwa huwezi bila kukuambia namna ya kuweza basi acha kumuambia.
BADILI MTAZAMO, KILA MTU ANAWEZA