26/09/2025
K**A UNAMPENDA SANA MAMA YAKO BASI SOMA HAPA!
Hamisi alikua anampenda sana Mama yake, pamoja na kwamba alikua ameoa lakini alikua akitumia muda mwingi sana nyumbani kwao na Mama yake, alikua akimsaidia Mama yake kazi, alikua akimnunulia Mama yake zawadi na vitu vya gharama sana. Pamoja na kumnunulia lakini Mama yake hakuvivaa aliviweka tu na alipomuuliza Mama yake alimjibu yeye kashazeeka havihitaji. Hamisi hakujali aliendelea kumdekeza na kumhudumia Mama yake.
Pamoja na Baba yake kuwa na pesa lakini Mama yake alikua hana furaha, Baba yake alikua akimnyanyasa, hamnunulii nguo nzuri, hamsikilizi na anamdharau sana. Hali ile ilimfanya Hamisi kumchukia Baba yake na kuapa kuwa atampa Mama yake kila kitu ilia ngalau awe na furaha kwani zamani hakufurahia pesa za Baba yake. Siku moja Mama yake alimuomba Hamisi amuandalie Sherehe, hakujua ni ya nini lakini kwakua alimpenda basi alimuandalia Sherehe kubwa.
Mama yake alimuambia katika sherehe aje na mke wake, Hamisi alikuja naye, katikati ya Sherehe Mama yake alisimama na kumuambia DJ kupiga wimbo wa “Happy Birthday” Huku kila mmoja akishangaa ilikua ni siku ya nani ya kuzaliwa Mama yake alimsimamisha mke wa Hamisi. Watu walishangaa hata yeye mwenyewe alishangaa, alishasahau k**a ni siku yake ya kuzaliwa, wakiwa katika ule mshangao waliingia vijana watano wakiwa na mabegi makubwa makubwa.
Mama Hamisi aliyafungua, yalikua na nguo nyingi, nguo zote ambazo Hamisi alikua akimpelekea Mama yake zilikua pale, Mama Hamisi alimpa mke wa Hamisi na kumumbia. “Chukua wewe ndiyo unastahili hizi zawadi sio mimi…” Kila mtu alishangaa, Mama alimuita Hamisi na kumuambia. “Najua unanipenda sana ndiyo maana umenipa hivi vitu, lakini nakupenda sana mwanangu hivyo sitaki ufanye kosa k**a alilolifanya Baba yako, sitaki wanao waje kukuchukia k**a unavyomchukia Baba yako.
Baba yako alimpenda Mama yake kuliko alivyokua ananipenda, akamsikiliza yeye zaidi, akamruhusu kutupangia maisha, alikua hanijali aliniona k**a takataka, nyie mliona mamboa liyokua ananifanyia mkamchukia na kunipenda mimi kwakua mlijua naonewa. Sasa anajua yote haya unayafanya kwa upendo lakini nikuulize mwanangu vipi mke wako, leo ni siku yake ya kuzaliwa je umeikumbuka? Lini ulishamnunulia nguo ya maana k**a zawadi? Lini umewahi kurudi nyumbani ukakaa na kula na mke wako zaidi ya kuja kula kwangu?”
Hamisi alibaki kimya hakua na jibu Mama yake alimuambia “Nenda kampende mkeo, sasa hivi huna watoto ila wakizaliwa na kuona namna unavyomtesa Mama yao watakuchukia k**a wewe unavyomchukia Baba yako na kumpenda mkeo, nakupenda sana mwanangu sitaki hayo yakutokee.” Alimaliza kuongea, Hamisi alikua anatokwa na machozi hakujua k**a matendo yake yanamfanya mkewe kukosa furaha na kumfanya yeye kuwa k**a Baba yake ambaye ni k**a aliwatelekeza, alimpigia mkewe magoti kumuomba msamaha, mkewe alimsamehe. Hamisi akaahidi kumpenda Mama yake pamoja na Mkewe.
nauza laptop aina zote tupo ilala machinga complex bei kuanzia 250,000 mkoani tunatuma kwa usalama na uaminifu mkubwa 0685916070