11/04/2026
KIBALI MBELE ZA MUNGU
Na
Marry Malack
+255759984391
Kibali ,ni hatua ya kukubalika kwa Mungu ,mtu ,kazini,family na jamii kwa ujumla
Unapokuwa na kibali ndipo huwa unakuwa na ruhusa ya kufanya jambo ,ama kuomba jambo sehemu uliyojipatia kibali
Unapaswa kujua hali uliyo nayo sasa inakuruhusu kuomba kibali ?
Ni hatua ya kuingia ndani zaidi na kukaa ,kusikiliza na kujifunza zaidi
Napo ni baada ya Mungu kukupa kibali
Unapopata kibali kwa Mungu hutuketisha mazungumzoni na kuanza kutupa maelekezo zaidi nini twapaswa kufanya na ni kwa wakati ngani
Ili upate kibali na mazungumzo na Mungu yakupasa uwe msafi yaani kujitakasa
1 Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu.
Kutoka 3:1
2 Malaika wa Bwana akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea.
Kutoka 3:2
3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei.
Kutoka 3:3
4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.
Kutoka 3:4
5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.
Kutoka 3:5
6 Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu.
Kutoka 3:6