11/01/2024
Mara ngapi unafanya vitu kwa ajili ya watu wengine? Na kujisahau wewe?
Yaani kila kitu unachokifanya unafanya kwa ajili ya watu wengine kuna wakati unadiliki hata kujinyima ili kuwafurahisha wengine, unakopa, unadhalilika ili tu wengine wafurahi
Unashindwa kwenda sehemu unazozipenda au kufanya vitu unavyovipenda na kukupa furaha ukiogopa watu watasema nini, sijui nitaonekanaje?
Unajua uko kwenye utumwa wa kujitakia? Unawezaje kujikomboa?
1. Jifikilie kwanza wewe kabla ya mtu mwingine, yaani utagawaje upendo kwa watu wengine akati wewe mwenyewe hujipendi? Hujijali?
2. Mwanadamu anakupenda na kukuheshimu ikiwa unafaida kwake faida ikiisha atakukimbia asikusaidie hata kidogo ukitaka kuamini siku moja waambie yaani nimepokea barua ya kuachishwa kazi na sina hata pa kuanzia ndo najitafuta naomba unikopeshe hela nianzishe biashara harafu utakuja kutupa majibu hapa wangapi watakuwa tayari kukusaidia
Je wao wamefanys nini/ au wanafanya juhudi gani kukufurahisha?
3. Wanadamu hawana shukurani wala kumbu kumbu hivyo fanya unapokuwa na nafasi k**a huna nafasi acha.
4. Kila mtu anakosea hivyo usiogope kumkosea mwanadamu
5. Sisi wote tulikuja duniani kwa njia moja na tutaondoka hivyo hivyo so usimuogope mtu
Sisemi watu msifanye vitu kwa ajili ya watu wengine lakini namaanisha fanya kulingana na uwezo wako usijikamue
Fanya vith kwa ajili yako kwanza na vyenye manufaa kwako moja kwa moja