28/02/2023
Mambo vipi? Mchana huu tumekuandalia machache kati ya mengi tuliyokuandalia na mtandaoni utakuwa nami Elisante Kivuyo , na hizi ni baadhi ya taarifa utakazozisikia:
📍Uingereza na Umoja wa Ulaya zimetangaza "ukurasa mpya" katika uhusiano baada ya miaka mingi ya mvutano wa Brexit, huku wakikubaliana kuhusu marekebisho ya sheria za biashara huko Ireland Kaskazini
🎧Ukraine imesema kuwa vikosi vyake vipo chini ya shinikizo katika mji wa Bakhmut, ambao umeharibiwa vibaya katika jimbo la mashariki la Donetsk, ambalo Urusi imekuwa ikijaribu kulikamata kwa miezi kadhaa
✔ Umoja wa Mataifa umesema zaidi ya nchi 30 zimeahidi kutoa msaada wa kiutu wa takribani dola bilioni 1.2 kwa ajili ya mamilioni ya watu wa Yemen
✍ Matokeo ya awali katika uchaguzi wa Nigeria uliofanyika mwishoni mwa wiki yanaonesha Bola Tinubu kutoka chama tawala akiwa kileleni.
:DW