05/05/2023
Fahamu sababu zinazoweza kupelekea kufa kwa biashara yako.
- HAUNA MIPANGO YA BIASHARA(Business Plan)
Hujui umetoka wapi, unaenda wapi na utafikaje, hauna mpango wowote bali unafanya biashara kwa mazoea ni unaamka tu na kuuza bidhaa/huduma, wateja wakinunua ni sawa na hata wasiponunua wewe hauna mpango.Biashara Bila Mipango Ni Ishara Ya Kwamba Sio Muda Mrefu Biashara Yako Inakaribia Kufa.
- HAUELEWI TABIA ZA WATEJA WAKO wateja wanatofautiana hivyo ni lazima uwaelewe vizuri wateja wako kuanzia mahitaji yao na hata tabia zao za manunuzi. Mfano; Unauza bidhaa Masaki halafu wateja wengi wanataka kukulipa kwa kadi za benki lakini wewe hauna njia ya kupokea malipo kwa benki matokeo yake unawalazimisha wakulipe kwa simu(mobile money), lazima utashindwa tu na biashara itafeli.
- MAHESABU MABOVU YA MZIGO(INVENTORY)
Hauna hesabu nzuri za biashara yako. Haufahamu mzigo wako kiasi gani uliingia, kiasi gani umeuza, kiasi gani umeingia hasara na kiasi gani umepata Faida.
- KUANZA KUITANUA BIASHARA MAPEMA; mfano, unauza nguo hata bado biashara haijachangaya tayari umehamia kwenye furniture na bidhaa zingine, kwa ufupi unakuwa na papara, kitu ambacho hakitakiwi kwenye biashara.Focus kwanza na kitu cha aina moja.
- KUKOSA MAUZO; biashara yako wateja wanaanza kupungua ila wewe haushtuki wala kuchukua hatua za kuwarudisha au kujua shida nini mwisho wa siku unakosa mauzo, unakosa kodi ya duka, unakosa mtaji halafu mwisho biashara inakufa.
- UNATAKA KUFANYA KILA KITU WEWE; wewe ndio unajua na kufanya kila kitu kwenye biashara yako, hata ikitokea unaumwa biashara inasimama, kwa style hii biashara hiyo kufa ni swala la muda tu.