Athuman Tumuisha nabii Muhammad aliyo yafanya akiwa hai

02/04/2026
02/04/2026

Niliwaambia hawa DPP na serikali wamekimbilia kwa Jaji Mkuu 😁 - Lissu kawabana kila kona kweli! Wameishiwa legal arguments!
Yaani ni vituko 🙄
Na niwaambie the only solution ili Taifa itulie ni na
Mnachelewesha the inevitable! Na mtatekeleza tu haya!
Nasema

02/04/2026

Anaandika Wakili Dickson Matata kwamba bei hizi mpya za mafuta zinawahusu wapinzani hasa hasa CHADEMA,

"Kwa wote wenye kadi za CCM bei hii mpya ya mafuta haiwahusu,hii ni kwa wapinzani tu hasa hasa CHADEMA,ukifika petrol station onyesha kadi yako ya CCM na utauziwa mafuta kwa bei ya zamani TZS 2800 na sio TZS 3800,nchi ni yenu bwana lazima mtambe!"

02/04/2026

Kwangu mimi nadhani kabla ya maamuzi waliyokuja nayo CAF kwa kwenye fainali ya AFCON Senegal dhidi ya Morocco, wangeanza uchunguzi kwenye hii mechi ya Morocco dhidi ya Taifa Stars. Tanzania ilinyimwa penati ya wazi ambayo hata mwamuzi aligoma kwenda kuangalia marudio kwenye chumba cha VAR.

02/04/2026

Naomba tuwape maneno ya Baraka vijana Hawa wa Kanda ya Kusini kwa Kuusimamia Msiba wa Mhe Bwege. Wamefanya kazi nzuri sana kwa kushirikiana na Wananchi wa Kilwa🙏

02/04/2026
02/04/2026

KWAHERI NDUGU WILLIAM LUKUVI, LAKINI CHUMVI IKIPOTEZA LADHA YAKE ITATIWA NINI HATA IKOLEE?

Mwl. John Pambalu

Kwanza nitoe pole kwa wote walioguswa na msiba wa Mzee Lukuvi. Pamoja na yote, bado tunabaki kuwa binadamu. Tukifanya k**a waliyotufanyia, atakosekana mwenye utu. Usipolipa baya kwa baya, ndipo utu unapobaki. “Rudisheni upanga arani mwake.” Lukuvi amekwenda. Wacha nizungumze na “Lukuvi” waliobaki. K**a chumvi ikipoteza ladha yake, itatiwa nini hata ikolee?

Ameondoka mshauri wa ndugu Samia. Ametuacha katika taifa ambalo wale waliowahi kusherehekea mateso na mauaji ya raia wasio na hatia, kwa majina ya wahaini au wakosoaji, leo hii nao wanapokumbwa na mauti au matatizo, umma unashangilia.

Ujumbe k**a “Asante Mungu kwa hiki kidogo”, “Kifo ni kifo”, au “Mungu amejibu” baada ya kifo cha mshirika au kiongozi wa serikali, kadiri vinavyozidi kusambaa, vinaonyesha wazi mpasuko mkubwa kati ya watawala na wanaotawaliwa.

Lakini je, hii ni kulipiza kisasi kwa Mungu? Kiimani, hapana. Maana Mungu alisema magugu na ngano vitaachwa vikue pamoja, na siku ya mwisho ndipo magugu yatafungwa kwa ajili ya moto na ngano kwa ajili ya ghala. Wema hufa, na wabaya pia hufa. Wema na wabaya wote huzeeka pia.

Lakini je, hali hii inatufundisha nini? Inatufundisha kuwa taifa limepoteza upendo, umoja na mshik**ano?

Naiona hatari mbele, tena hatari kubwa sana. Wanaosherehekea kifo cha Lukuvi leo, kuna “Lukuvi” mwingine yupo mtaa wa Kanyerere Butimba Mwanza, anaweza kuwa mjumbe wa shina au balozi wa nyumba kumi na mwingine yuko Namtumbo au Songwe. Usiniambie wataishia kusherehekea kifo cha Lukuvi wa Isimani na wasisherehekee cha Lukuvi wa Kanyerere. Hilo ni hatari zaidi.

Chuki hii ikizidi, itafikia hatua ya kumsaidia Mungu “kuvuna” vilivyo vyake. Na hapo, aliyesherehekea kifo na aliyeumia kwa kifo cha Lukuvi, hakuna atakayekuwa salama.

Lakini tumefikaje hapa?

1. Mauaji ya wakosoaji wa serikali

2. Utekaji wa watu wenye mawazo tofauti

3. Kesi za uongo dhidi ya wakosoaji

4. Kuumizwa kwa viongozi wa dini wenye mawazo tofauti

5. Kufungiwa makanisa na watumishi wa Mungu wenye mitazamo mbadala

6. Wizi wa kura na kunyimwa haki ya kuchagua viongozi wanaowataka.

Haya na mengine mengi k**a haya yamelipasua taifa letu, lile tulilokuwa tunaimba, “Tazama ramani utaona nchi nzuri… Utumwa wa nchi Nyerere aliukomesha…”

Leo watu wamekuwa watumwa wa chuki, kutokana na uovu waliotendewa, waliosikia au walioshuhudia ukitendeka kwa ndugu zao umesababisha watu kujaa chuki. Nafikiri ni wakati wa kutafuta njia ya kutoka hapa tulipofika.

Nina ushauri muhimu kwa kila mwenye kulipenda taifa hili:

Futeni kesi za uongo. Lissu na Kaunya waachiwe huru. Fungulieni CHADEMA ifanye kazi zake. Ombeni radhi kwa yote yaliyotokea tangu 2015. Waliotesa, kuteka kuumiza na kuua watu wawajibishwe. Waliokimbia nchi warejee wakiwa na uhakika wa usalama na uhai wao.

Taifa liungane kuandika Katiba mpya yenye nguvu ya kudhibiti walafi na walevi wa madaraka. Hata Mungu atasema: “Wanangu wameamua kubadilika.”

Kila mmoja anaweza kuchagua kuwa chumvi. Chumvi huleta ladha, huzuia vitu kuharibika. Hata ikiwekwa kwenye kilichoanza kuharibika, hupunguza au kuzuia kuharibika zaidi.
Ninatamani kuona mtoto wa Mdude akicheza pamoja na mtoto wa Mchengerwa au Mwigulu. Lakini yote yanawezekana tu ikiwa kweli na haki vitarudi.

Mambo ya Mungu hayachunguziki. Unampiga risasi mtu. Unamnyima fedha za matibabu. Unamfunga kwa hila ili angalau afe kwa presha na hafi. Halafu anakufa anayekushauri kuyafanya au kutoyafanya unayoyafanya.

Mambo ya Mungu hayachunguziki jamani. Kifo ni mawaidha k**a ya Ramadhan na Kwaresma hayakutosha kuwaeleza acheni kuonea wasio na hatia. Wafungulieni mliowafungwa kwa hila. Ningetamani msome ule mfano wa Yesu juu ya yule mkulima aliyevuna vingi akaimbia nafsi yake ee nafsi yangu umepata vyote tunywe, tule na tufurahi. Yesu akaendelea kusema ee mpumbavu wewe ungejua leo wanaitaka roho yako.......

Ninasimama kwa zamu yangu kujenga palipobomoka. Wewe je?

Kwaheri Mzee Lukuvi. Ungesimama uone jinsi hata msiba wako haujatuunganisha bali umeongeza utengano. Kisha umshauri aliyekuteua ndipo uende. Lakini hilo haliwezekani tena.

Tumefika mahali ambapo hata mema machache uliyowahi kuyafanya leo hakuna yanayokumbukwa. Unakumbukwa kwa video zinazosambaa ambazo kwa upande wa ubinadamu wako ni kweli ulikosea kutamka maneno ya chuki dhidi ya waislamu wa Zanzibar na mzee Abuu wa Nela Mwanza?.

Kwamba mema uliyowahi kuyatenda, hakuna linalotrend hata moja. Tunayaona, tunayashuhudia na tunajiuliza tumefikaje huku?. Nenda Lukuvi tuliosalia bado tunayo nafasi ya kuwa chumvi au mwanga ili tuliponye taifa. Dua na sala yangu upate pumziko la amani.

“Nyinyi ni chumvi ya ulimwengu.”

Wasalamu,
John Pambalu
[email protected]

02/04/2026

Msanii wa nyimbo za injili kutoka Kisii nchini kenya, Mary Claire, anapigania uhai wake hospitalini baada ya kushambuliwa kikatili kwa kumwagiwa asidi na EX wake.

Kwa mujibu wa taarifa, mshukiwa mkuu wa tukio hilo anadaiwa kuwa ni mpenzi wake wa zamani, ambaye inasemekana alikuwa na mgogoro wa kimapenzi na Claire kwa muda.

Inaelezwa kuwa mwanaume huyo aliwahi kumsaidia Claire kifedha katika masomo yake (Kumsomesha) kwa makubaliano angeolewa k**a mke wa pili baada ya kukamilisha masomo., lakini mambo yalibadilika baada ya msanii huyo kuamua kuendelea na maisha yake na kuingia katika uhusiano na mwanaume mwingine.

Hata hivyo, baadhi ya taarifa kuhusu undani wa mahusiano yao bado hazijathibitishwa rasmi, huku uchunguzi ukiendelea kubaini ukweli kamili wa tukio hilo la kusikitisha.

Claire kwa sasa anaendelea kupatiwa matibabu huku wengi wakimuombea apone haraka.

💬 Maoni yako ni yapi kuhusu matukio ya ukatili wa mapenzi yanayoongezeka?
🙏 Tumuombee apone haraka


Endereço

São Paulo, SP

Notificações

Seja o primeiro recebendo as novidades e nos deixe lhe enviar um e-mail quando Athuman posta notícias e promoções. Seu endereço de e-mail não será usado com qualquer outro objetivo, e pode cancelar a inscrição em qualquer momento.

Compartilhar

Categoria