Kwale Press Club

Kwale Press Club Professional journalists in Kwale County sharing credible news and nurturing talent.

MWANI WA KWALE WASAFIRISHWA CHILE Tani 43 za Mwani zimesafirishwa kutoka kwa kundi la wakulima wa Mwani wa Kibuyuni huko...
06/08/2026

MWANI WA KWALE WASAFIRISHWA CHILE

Tani 43 za Mwani zimesafirishwa kutoka kwa kundi la wakulima wa Mwani wa Kibuyuni huko Lungalunga kaunti ya Kwale hadi nchi ya Chile.

Hii ni mara ya kwanza kwa wakulima hao kupata soko kubwa la kimataifa kwa zao lao.

Akizungumza wakati wa kuaga shehena hiyo, naibu gavana wa Kwale Chirema Kombo amesema serikali ya kaunti inawekeza kwenye sekta za kilimo na uchumi wa baharini ili kukuza uchumi na kuboresha maisha ya wenyeji.

Profesa Hamadi Boga: Lazima vijana tupige kura tofauti, kwa sababu inaashiria kwamba wale ambao wamekua mamlakani miaka ...
06/08/2026

Profesa Hamadi Boga: Lazima vijana tupige kura tofauti, kwa sababu inaashiria kwamba wale ambao wamekua mamlakani miaka yote hiyo wameshindwa kubuni ajira za kutosha. Hawajui jinsi ya kubuni ajira.

05/08/2026

MASKWOTA WA NIKAPHU WAKATAA KUPEWA ROBO EKARI

Wakazi wa kijiji cha Nikaphu katika eneo bunge la Lungalunga, kaunti ya Kwale, wamepinga mpango wa serikali wa kuwagawia maskwota ardhi ya robo ekari kwa kila familia.

Wanasema zoezi la kugawa ekari 270 zinazokusudiwa kunufaisha familia 137 limeratibiwa kufanywa bila kuwahusisha ipasavyo, jambo ambalo limeibua wasiwasi kwamba baadhi ya watu wasiostahili wanaweza kujumuishwa miongoni mwa wanufaika.

Wakazi hao wanataka ugavi wa ardhi uzingatie ukubwa wa mashamba ambayo kila familia imekuwa ikitumia kwa muda mrefu.

Wanasisitiza kuwa hawako tayari kupokea maeneo madogo kuliko yale ambayo wamekuwa wakiyamiliki na kuyatumia kwa miaka mingi.

WATU 40 waliokolewa salama baada ya boti ya MV Siri Ya Mafanikio kupinduka katika eneo la Mkondoni, Shimoni kaunti ya Kw...
02/08/2026

WATU 40 waliokolewa salama baada ya boti ya MV Siri Ya Mafanikio kupinduka katika eneo la Mkondoni, Shimoni kaunti ya Kwale.

Operesheni hiyo ya uokoaji ilifanywa jana na maafisa wa kituo cha Shimoni cha Kenya Coast Guard (KCGS) baada ya kupokea taarifa ya dharura kuhusu ajali hiyo ya baharini.

Kwa mujibu wa KCGS, chombo hicho kiliondoka Shimoni saa mbili asubuhi kikielekea Pemba kikiwa na wahudumu 10 na abiria 30.

Kilipinduka kutokana na upepo mkali na mawimbi makubwa yaliyokikumba katika eneo la bahari ya Mkondoni.

Mabaki ya chombo hicho yalivutwa hadi Bandari ya Shimoni kwa uchunguzi zaidi kuhusu chanzo cha ajali hiyo.

02/08/2026

Fatuma Achani: Mimi ni simba jike, usione ajabu wanaume wameungana kushindana na mimi.

02/08/2026

Mangale Chiforomodo: Tolwa si matusi endeni mwambie uyo mzee k**a amechoka awachane na siasa. Tunataka vitambulisho vitolewe burebure haraka haraka.

02/08/2026

Fatuma Achani: Tunashukuru EACC kwa kuturudishia kipande hiki cha ardhi cha beach.

02/08/2026

EACC yarejesha barabara ya umma ya kuelekea ufukweni iliyonyakuliwa Diani

Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) imerejesha barabara ya umma ya kuelekea ufuoni iliyokuwa imenyakuliwa katika eneo la Diani, Kaunti ya Kwale, hatua inayorejesha njia muhimu ya umma ya kufikia Bahari ya Hindi.

Barabara hiyo yenye urefu wa mita 300, inayounganisha Barabara ya Diani Links na ufukwe katika eneo la Absa na Swahili beach, ni muhimu kwa wakazi pamoja na watalii.

Hata hivyo, juhudi za kuiendeleza zilikwama baada ya ardhi hiyo kutwaliwa kinyume cha sheria na watu binafsi.

Kiwanja kilichorejeshwa kina ukubwa wa takriban ekari 1.14 na kinakadiriwa kuwa na thamani ya shilingi milioni 45.

Mkurugenzi Mkuu wa EACC, Abdi Mohamud, alisema tume ilifanikiwa kurejesha ardhi hiyo baada ya kushinda kesi mahak**ani dhidi ya waliokuwa wameinyakua.

Aliongeza kuwa EACC itaendelea na juhudi za kurejesha ardhi nyingine za umma zilizonyakuliwa isivyo halali katika Kaunti ya Kwale, ikiwemo eneo lililokaliwa na Msikiti wa kihistoria wa Kongo.

02/08/2026

Watumiaji wa barabara ya Kwale kinango wataka daraja kurekebishwa

Watumiaji wa barabara ya Kinango-Kwale wanaita Mamlaka ya Barabara Kuu Kenya (KeNHA) kuanza na kukamilisha mara moja ukarabati wa Daraja la Marere linalounganisha Kinango na Kwale baada ya kukatika jumapili iliyopita.

Usafiri katika Barabara hiyo ulitatizika kwa muda baada ya daraja hilo la zamani kuvunjika na kusababisha gari moja kuanguka.

Wasafiri wanaotumia barabara hiyo wanasema njia ya muda iliyotengenezwa ni nyembamba na wanaitaka idara husika ya barabara kushughulikia daraja hilo ili kurejesha usafiri wa kawaida.

Wanasema mkandarasi anayejenga daraja la kisasa na Barabara ya Kwale–Kinango anakumbana na wakati mgumu kuendelea na kazi kutokana na kuvunjika kwa daraja hilo.

Jaindi Kisero, Independent Economics and Business Journalist: The government should approach procurement of global minin...
01/08/2026

Jaindi Kisero, Independent Economics and Business Journalist: The government should approach procurement of global mining companies and developers for Kwale County's niobium and rare earths projects at Mrima Hills with more transparency.

Address

Kwale
80405

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kwale Press Club posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kwale Press Club:

Shortcuts

Share