04/10/2025
Ee mtu upendwaye sana, usiogope; amani na iwe kwako, uwe na nguvu, naam, uwe na nguvu.
Tazama mpendwa uliyepewa neema ya Mungu na amani ya wetu Yesu,nakuuliza na kukuomba u some maandiko haya ujue Mungu you pamoja nawe ili akusaidie na kukuokoa na kukukomboa ndio maana mara nyingi imeandikwa usiogope.
❝Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema Bwana, ili nikuokoe.❞(Yeremia 1: 19)
❝Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza.❞
—Isaya 43: 2)
Yeremia 15 (²⁰ Nami nitakufanya kuwa k**a ukuta wa boma la shaba juu ya watu hawa; nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, ili nikuokoe, na kukuponya, asema Bwana.
²¹ Nami nitakuokoa na mkono wa watu wabaya, nami nitakukomboa katika mkono wao wenye kutisha.
❝Kaa wewe pamoja nami, usiogope; kwa maana yeye atafutaye roho yangu, ndiye atafutaye na roho yako; nawe utakaa kwangu salama.❞(1 Samweli 22: 23)
❝Usiogope kwa sababu ya hao maana mimi nipo pamoja nawe nikuokoe, asema Bwana.❞
—Yeremia 1: 8)
❝Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.❞(2 Wafalme 6: 16)
Mithali 3 (²³ Ndipo utakapokwenda katika njia yako salama, Wala mguu wako hautakwaa. ²⁴ Ulalapo hutaona hofu; Naam, utalala na usingizi wako utakuwa mtamu. ²⁵ Usiogope hofu ya ghafula, Wala uharibifu wa waovu utakapofika.
²⁶ Kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako, Naye atakulinda mguu wako usinaswe.
❝Utafichwa na mapigo ya ulimi; Wala usiogope maangamizo yatakapokuja.❞(Ayubu 5: 21)
❝Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.❞
—Yoshua 1: 9)
❝Naye Bwana, yeye ndiye atakayekutangulia, atakuwa pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha; usiogope wala usifadhaike.❞(Kumbukumbu 31: 8)
❝Nami nitawapa amani katika nchi, tena mtalala wala hapana atakayewatia hofu; nami nitawakomesha wanyama wabaya katika nchi yenu, wala hautapita upanga katika nchi yenu.❞(Walawi 26: 6)
Isaya 41 (¹⁰ usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu. ¹¹ Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia. ¹² Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa k**a kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako. ¹³ Kwa maana mimi, Bwana, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia.
Warumi 8 (²⁸ Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.
²⁹ Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. ³⁰ Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza. ³¹ Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu?
2 Wakorintho 4 (⁶ Kwa kuwa Mungu, aliyesema, Nuru itang'aa toka gizani, ndiye aliyeng'aa mioyoni mwetu, atupe nuru ya elimu ya utukufu wa Mungu katika uso wa Yesu Kristo.
¹⁵ Kwa maana mambo yote ni kwa ajili yenu, ili neema hiyo ikiongezwa sana, kwa hao walio wengi shukrani izidishwe, na Mungu atukuzwe. ¹⁶ Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku.