Vijana Wana Nguvu

Vijana Wana Nguvu To share the word of God
To help and reaching young men and women to battle of life
In business, politics and more

16/02/2026

Kwa mapenzi ya Mungu tumekombokewa kwa damu ya Yesu kristo.
Katika mapenzi hayo mmepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu.
Tumeokokewa kwa neema ya Mungu kwa njia ya Imani iliokatika kristo Yesu.
❝wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele.❞(Waebrania 9: 12)10:4❝Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.❞

15/02/2026

Damu ya kristo Yesu ndiyo damu ilioamriwa iwe ya agano jipya.
Malaki 2 (⁵ Agano langu naye lilikuwa agano la uhai na amani; nami nikampa ili aogope, naye akaniogopa, akalicha jina langu.
⁶ Sheria ya kweli ilikuwa kinywani mwake, wala udhalimu haukuonekana midomoni mwake; alikwenda pamoja nami katika amani na unyofu, na kuwageuza wengi hata wakaacha uovu.
⁷ Kwa maana yapasa midomo ya kuhani ihifadhi maarifa, tena yawapasa watu kuitafuta sheria kinywani mwake; kwa kuwa yeye ni mjumbe wa Bwana wa majeshi.

Hii ni damu ya agano mliloamriwa na Mungu.

❝kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.❞
—Mathayo 26: 28)
Zekaria 9 (¹¹ Na kwa habari zako wewe, kwa sababu ya damu ya agano lako, nimewatoa wafungwa wako katika shimo lile lisilo na maji. ¹² Irudieni ngome, enyi wafungwa wa tumaini; hata hivi leo nasema ya kwamba nitakurudishia maradufu.

24/01/2026

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi.❞

2 Wathesalonike 1 (¹¹ Kwa hiyo twawaombea ninyi sikuzote, ili Mungu wetu awahesabu kuwa mmekustahili kuitwa kwenu, akatimiza kila haja ya wema na kila kazi ya imani kwa nguvu; ¹² jina la Bwana wetu Yesu litukuzwe ndani yenu, nanyi ndani yake, kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.
Waefeso 6 (²³ Amani na iwe kwa ndugu, na pendo, pamoja na imani, zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Bwana Yesu Kristo.
²⁴ Neema na iwe pamoja na wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo katika hali ya kutokuharibika.

24/01/2026

Mmetengwa na Kristo, ninyi mtakao kuhesabiwa haki kwa sheria; mmeanguka na kutoka katika hali ya neema.
Maana sisi kwa Roho tunalitazamia tumaini la haki kwa njia ya imani.

❝Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu;❞
wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.
Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.(Waefeso 2: 8-10)

24/01/2026

Kusimama imara katika Bwana.
Wafilipi 4 (¹ Basi, ndugu zangu, wapendwa wangu, ninaowaonea shauku, furaha yangu, na taji yangu, hivyo simameni imara katika Bwana, wapenzi wangu.
⁴ Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.
⁵ Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
⁶ Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
⁷ Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
⁸ Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.
¹⁹ Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.
²⁰ Sasa atukuzwe Mungu, Baba yetu, milele na milele. Amina.

Wafilipi 1 (⁶ Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu;
¹⁰ mpate kuyakubali yaliyo mema; ili mpate kuwa na mioyo safi, bila kosa, mpaka siku ya Kristo;
¹¹ hali mmejazwa matunda ya haki, kwa njia ya Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa ya Mungu.
1 Wathesalonike 2 (¹² ili mwenende k**a ilivyo wajibu wenu kwa Mungu, mwenye kuwaita ninyi ili mwingie katika ufalme wake na utukufu wake. ¹³ Kwa sababu hiyo sisi nasi twamshukuru Mungu bila kukoma, kwa kuwa, mlipopata lile neno la ujumbe la Mungu mlilolisikia kwetu, mlilipokea si k**a neno la wanadamu, bali k**a neno la Mungu; na ndivyo lilivyo kweli kweli; litendalo kazi pia ndani yenu ninyi mnaoamini.

24/01/2026

❝Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.❞
2 Wakorintho 6 (¹ Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.
² (Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)

Kukirimiwa wingi wa neema na utajiri wa kristo.
2 Wakorintho 8 (⁷ Lakini k**a mlivyo na wingi wa mambo yote; imani, na usemi, na elimu, na bidii yote, na upendo wenu kwetu sisi; basi vivyo hivyo mpate wingi wa neema hii pia. ⁹ Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.

Kujazwa neema kwa wingi.
2 Wakorintho 9 (⁸ Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema; ⁹ k**a ilivyoandikwa, Ametapanya, amewapa maskini, Haki yake yakaa milele. ¹⁰ Na yeye ampaye mbegu mwenye kupanda, na mkate uwe chakula, atawapa mbegu za kupanda na kuzizidisha, naye atayaongeza mazao ya haki yenu;
¹¹ mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu.

Kupewa mambo yote na kuongezewa neema.
2 Wakorintho 4 (¹⁵ Kwa maana mambo yote ni kwa ajili yenu, ili neema hiyo ikiongezwa sana, kwa hao walio wengi shukrani izidishwe, na Mungu atukuzwe.
¹⁶ Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku. ¹⁷ Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana; ¹⁸ tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.

Kutajirishwa katika Kila jambo.
1 Wakorintho 1 (⁴ Namshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, kwa sababu ya neema ya Mungu mliyopewa katika Kristo Yesu; ⁵ kwa kuwa katika kila jambo mlitajirika katika yeye, katika

Address

Maua

Opening Hours

Monday 21:00 - 17:00
Tuesday 21:00 - 17:00
Wednesday 21:00 - 17:00
Thursday 21:00 - 17:00
Friday 21:00 - 17:00
Saturday 21:00 - 17:00

Telephone

+254742047413

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Vijana Wana Nguvu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share