Vijana Wana Nguvu

Vijana Wana Nguvu To share the word of God
To help and reaching young men and women to battle of life
In business, politics and more

24/01/2026

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi.❞

2 Wathesalonike 1 (¹¹ Kwa hiyo twawaombea ninyi sikuzote, ili Mungu wetu awahesabu kuwa mmekustahili kuitwa kwenu, akatimiza kila haja ya wema na kila kazi ya imani kwa nguvu; ¹² jina la Bwana wetu Yesu litukuzwe ndani yenu, nanyi ndani yake, kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.
Waefeso 6 (²³ Amani na iwe kwa ndugu, na pendo, pamoja na imani, zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Bwana Yesu Kristo.
²⁴ Neema na iwe pamoja na wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo katika hali ya kutokuharibika.

24/01/2026

Mmetengwa na Kristo, ninyi mtakao kuhesabiwa haki kwa sheria; mmeanguka na kutoka katika hali ya neema.
Maana sisi kwa Roho tunalitazamia tumaini la haki kwa njia ya imani.

❝Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu;❞
wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.
Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.(Waefeso 2: 8-10)

24/01/2026

Kusimama imara katika Bwana.
Wafilipi 4 (¹ Basi, ndugu zangu, wapendwa wangu, ninaowaonea shauku, furaha yangu, na taji yangu, hivyo simameni imara katika Bwana, wapenzi wangu.
⁴ Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.
⁵ Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
⁶ Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
⁷ Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
⁸ Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.
¹⁹ Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.
²⁰ Sasa atukuzwe Mungu, Baba yetu, milele na milele. Amina.

Wafilipi 1 (⁶ Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu;
¹⁰ mpate kuyakubali yaliyo mema; ili mpate kuwa na mioyo safi, bila kosa, mpaka siku ya Kristo;
¹¹ hali mmejazwa matunda ya haki, kwa njia ya Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa ya Mungu.
1 Wathesalonike 2 (¹² ili mwenende k**a ilivyo wajibu wenu kwa Mungu, mwenye kuwaita ninyi ili mwingie katika ufalme wake na utukufu wake. ¹³ Kwa sababu hiyo sisi nasi twamshukuru Mungu bila kukoma, kwa kuwa, mlipopata lile neno la ujumbe la Mungu mlilolisikia kwetu, mlilipokea si k**a neno la wanadamu, bali k**a neno la Mungu; na ndivyo lilivyo kweli kweli; litendalo kazi pia ndani yenu ninyi mnaoamini.

24/01/2026

❝Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.❞
2 Wakorintho 6 (¹ Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.
² (Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)

Kukirimiwa wingi wa neema na utajiri wa kristo.
2 Wakorintho 8 (⁷ Lakini k**a mlivyo na wingi wa mambo yote; imani, na usemi, na elimu, na bidii yote, na upendo wenu kwetu sisi; basi vivyo hivyo mpate wingi wa neema hii pia. ⁹ Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.

Kujazwa neema kwa wingi.
2 Wakorintho 9 (⁸ Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema; ⁹ k**a ilivyoandikwa, Ametapanya, amewapa maskini, Haki yake yakaa milele. ¹⁰ Na yeye ampaye mbegu mwenye kupanda, na mkate uwe chakula, atawapa mbegu za kupanda na kuzizidisha, naye atayaongeza mazao ya haki yenu;
¹¹ mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu.

Kupewa mambo yote na kuongezewa neema.
2 Wakorintho 4 (¹⁵ Kwa maana mambo yote ni kwa ajili yenu, ili neema hiyo ikiongezwa sana, kwa hao walio wengi shukrani izidishwe, na Mungu atukuzwe.
¹⁶ Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku. ¹⁷ Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana; ¹⁸ tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.

Kutajirishwa katika Kila jambo.
1 Wakorintho 1 (⁴ Namshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, kwa sababu ya neema ya Mungu mliyopewa katika Kristo Yesu; ⁵ kwa kuwa katika kila jambo mlitajirika katika yeye, katika

09/11/2025

Bwana na akujibu, Akuponye na hofu zako zote.

Zaburi 20 (⁴ Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako, Na kuyatimiza mashauri yako yote.
⁵ Na tuushangilie wokovu wako, Kwa jina la Mungu wetu tuzitweke bendera zetu. Bwana akutimizie matakwa yako yote.
⁶ Sasa najua kuwa Bwana amwokoa masihi wake;Atamjibu kutoka mbingu zake takatifu.

❝Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo, Na waliopondeka roho huwaokoa.❞(Zaburi 34: 18)
145 (¹⁸ Bwana yu karibu na wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu. ¹⁹ Atawafanyia wamchao matakwa yao, Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa.

Ee mtu upendwaye sana, usiogope; amani na iwe kwako, uwe na nguvu, naam, uwe na nguvu. Tazama mpendwa uliyepewa neema ya...
04/10/2025

Ee mtu upendwaye sana, usiogope; amani na iwe kwako, uwe na nguvu, naam, uwe na nguvu.

Tazama mpendwa uliyepewa neema ya Mungu na amani ya wetu Yesu,nakuuliza na kukuomba u some maandiko haya ujue Mungu you pamoja nawe ili akusaidie na kukuokoa na kukukomboa ndio maana mara nyingi imeandikwa usiogope.

❝Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema Bwana, ili nikuokoe.❞(Yeremia 1: 19)
❝Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza.❞
—Isaya 43: 2)
Yeremia 15 (²⁰ Nami nitakufanya kuwa k**a ukuta wa boma la shaba juu ya watu hawa; nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, ili nikuokoe, na kukuponya, asema Bwana.
²¹ Nami nitakuokoa na mkono wa watu wabaya, nami nitakukomboa katika mkono wao wenye kutisha.

❝Kaa wewe pamoja nami, usiogope; kwa maana yeye atafutaye roho yangu, ndiye atafutaye na roho yako; nawe utakaa kwangu salama.❞(1 Samweli 22: 23)
❝Usiogope kwa sababu ya hao maana mimi nipo pamoja nawe nikuokoe, asema Bwana.❞
—Yeremia 1: 8)
❝Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.❞(2 Wafalme 6: 16)
Mithali 3 (²³ Ndipo utakapokwenda katika njia yako salama, Wala mguu wako hautakwaa. ²⁴ Ulalapo hutaona hofu; Naam, utalala na usingizi wako utakuwa mtamu. ²⁵ Usiogope hofu ya ghafula, Wala uharibifu wa waovu utakapofika.
²⁶ Kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako, Naye atakulinda mguu wako usinaswe.

❝Utafichwa na mapigo ya ulimi; Wala usiogope maangamizo yatakapokuja.❞(Ayubu 5: 21)
❝Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.❞
—Yoshua 1: 9)
❝Naye Bwana, yeye ndiye atakayekutangulia, atakuwa pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha; usiogope wala usifadhaike.❞(Kumbukumbu 31: 8)
❝Nami nitawapa amani katika nchi, tena mtalala wala hapana atakayewatia hofu; nami nitawakomesha wanyama wabaya katika nchi yenu, wala hautapita upanga katika nchi yenu.❞(Walawi 26: 6)
Isaya 41 (¹⁰ usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu. ¹¹ Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia. ¹² Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa k**a kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako. ¹³ Kwa maana mimi, Bwana, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia.

Warumi 8 (²⁸ Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.
²⁹ Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. ³⁰ Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza. ³¹ Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu?

2 Wakorintho 4 (⁶ Kwa kuwa Mungu, aliyesema, Nuru itang'aa toka gizani, ndiye aliyeng'aa mioyoni mwetu, atupe nuru ya elimu ya utukufu wa Mungu katika uso wa Yesu Kristo.
¹⁵ Kwa maana mambo yote ni kwa ajili yenu, ili neema hiyo ikiongezwa sana, kwa hao walio wengi shukrani izidishwe, na Mungu atukuzwe. ¹⁶ Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku.

12/07/2024

Nakuuliza uje utendalo utatendewa Kwa hivyo tenda mema nawe utatendewa mema ukijua hata mawaziri waliodharau Gen z ruto aliwamwaga

27/06/2024

KUMBUKENI MITHALI HII .
Pasipo mashauri taifa huanguka; Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.(Mithali 11: 14)
Mithali 15 ²² Pasipo mashauri makusudi hubatilika; Bali kwa wingi wa washauri huthibithika.
²³ Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake; Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema k**a nini!
²⁴ Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu; Ili atoke katika kuzimu chini.

SIKILIZA MASHAURI.
Sikiliza mashauri, ukapokee mafundisho, Upate kuwa na hekima siku zako za mwisho.❞
—Mithali 19: 20)
❝Kila kusudi huthibitika kwa kushauriana; Na kwa shauri la akili fanya vita.(Mithali 20: 18)

Address

Maua

Opening Hours

Monday 21:00 - 17:00
Tuesday 21:00 - 17:00
Wednesday 21:00 - 17:00
Thursday 21:00 - 17:00
Friday 21:00 - 17:00
Saturday 21:00 - 17:00

Telephone

+254742047413

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Vijana Wana Nguvu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share