22/05/2015
MCHANGO WA FAMILIA KATIKA PROJECT ZAKO.
Familia ina mchango mkubwa sana katika kufanikisha mradi unao uiendesha uwe ni kilimo, ufugaji au hata biashara za kawaida, mafanikio hapa hutegemea familia.
Familia inategemewa katika maeneo kadhaa k**a vile
1. Kutoa sapoti ya fedha
2. Kutoa sapoti ya man power
3. Kutoa saport ya kukutia moyo wewe initiator wa Idea
4. Kuja kuwa wasimamizin wa mradi wapo endapo, utakuwa uko mbali, unaumwa au hata kufariki dunia.
WANAO TAKIWA KUTOA SAPOTI.
MAMA/BABA
Mara nyingi tumekuwa tunaendesha miradi pekee yetu, either utakuta ni Mama ana mradi wake wa Ng'ombe au kuku au mbuzi au Nguruwe au hata shamba na Baba hana time na wala hana hoby hizo kabisa, yaani mama hoby yake ni kufuga mzee hobby yake ni magari, na upande wa pili wa hivyo hivyo.
Mke/mme ni lazima awe bega kwa bega na project ya mwenzake na kuhakikisha kwamba project inasonga mbele,
Kwa staili hii mafanikio huwa ni vigumu sana kupatikana.
WATOTO
Watoto ni lazima wawe wanatoa sapoti ya kutosha hasa sapoti ya man power,
Unaweza kuta mzee ni mkulima au ni mfugaji mzuri sana wa Nguruwe au kuku au Ng'ombe na watoto ndo kabisa hawana habari kwanza hata kuona kinyesi cha ng'ombe kwao ni kinyaa cha hari ya juu.
Unaamka asubuhi kuingia kwenye banda la Ng'ombe au kuku watoto wanaachwa wamelala au wako bise kucheza game,
Unaenda shambani, asubuhi huku nyuma unaacha watoto wakiwa wamelala au wanacheza,
Ni makosa makubwa sana yanafanyika ukizania unawapenda watoto wako,
NI LAZIMA WATOTO WAKO WAJUE HAYA.
1. Wajue kuendesha shughuri zako ziwe ni za kilimo au ufugaji au duka,
2. Wajue madawa yote unayo tumia kutibu
3. Wajue wateja wako/marafiki wa mradi wako
4. Ukienda shamba au bandani lazima wawepo hata kwa nusu saa kuona mambo yanavyo enda.
5. Lazima uwape hamasa kwamba watakapo maliza masomo yao basi wanatakiwa kuja kuendeleza kile unacho fanya wewe
MADHARA YA KUKOMAA NA PROJECT PEKE YAKO NI K**A HAYA.
1. Endapo una project yako ya kuku/mbuzi/shamba/hoteli/ng'ombe au nguruwe na ukaugua muda mrefu na hapo nyumbani hakuna anaye jua hata yai linaokotwa vipi, itakuwa ni shida sana na matokea yake ni mradi wako kufa
2. Ukiwa hauko duniani na mradi wako utakufuata huko huko since walio bakia hakuna anaye jua chochote kile, ndo ile huwa unaona mzee kafa na baada ya mwezi biashara nayo haipo tena hii ni kwa sababu hakuna sapoti alio kuwa anapata toka kwa familia yake yeye alikuwa na spiri ya biashara huku famuilia ikiwa na hoby nyingine kabisa.