05/09/2021
Katika biashara kuna kitu kinaitwa (Scalling).
Biashara yako inaweza ikawa inafanya scalling kwa mifumo tofauti, kutegemeana na aina ya biashara unayofanya.
Kwa mfano;
K**a mwaka huu umehudumia wateja 10, hakikisha mwaka kesho unahudumia wateja 15. Kadiri miaka inavyosogea, na idadi ya wateja wako iwe inaongezeka.
K**a mwaka huu ulifuga ng'ombe wawili, basi mwakani hakikisha wamefika ng'ombe saba.
Mwaka huu ukifungua duka moja, basi baada ya miaka 3, uwe umeongeza duka la pili, au mengi zaidi.
nyingine ni ile ya kubaki na "unit" ile ile moja, lakini ukaiboresha zaidi.
Kwa mfano; Ukianza kwa kumiliki mgahawa mmoja, baada ya miezi kadhaa unaongeza idadi ya vyakula unavyopika, na ukubwa wa eneo la mgahawa wako.
Unakua bado uko na mgahawa ule ule mmoja, lakini umeuboresha zaidi.
Scalling inaweza kufanyika kwa njia mbalimbali kadiri wewe mwenyewe unavyoona.
Miaka michache iliyopita Kampuni ya VUNJABEI ilikua inamiliki duka moja pekee jijini Dar es Salaam, maeneo ya Sinza Madukani.
Mwaka huu, 2021, VUNJABEI inamiliki maduka 8 katika mikoa 6 tofauti hapa Tanzania.
Huu ni ukuaji wa kasi sana. Fast Scalling.
VUNJABEI inayo maduka katika mikoa ya; Mwanza, Dodoma, Arusha, Mbeya, Iringa, na Dar es Salaam ambapo yapo maduka matatu.
Mwaka huu, timu ya SIMBA iliingia mkataba na VUNJABEI wenye thamani ya Tshs 2billioni, kwa kipindi cha miaka miwili.
Hii inamaanisha kwamba, Vunjabei atailipa Simba Tshs 2billioni, huku yeye akiruhusiwa kutengeneza na kuuza vifaa vyote vya timu ya Simba.
Kazi tayari imeanza.
Wiki hii, Vunjabei ameanza kuuza jezi, kofia, skafu, soksi, na vifaa vinginevyo vya michezo vya timu ya Simba. Mzigo unapatikana katika maduka yote 8 ya VUNJABEI nchi nzima.
Katika suala la , VUNJABEI ni kitabu kizuri sana ambacho kinatakiwa kisomwe na vijana wote walioko katika biashara, hasa zile za rejareja (Retail).
Kwa mtazamo wangu, huu mkataba wa miaka miwili baina ya Vunjabei na Simba, umetumika tu k**a majaribio.
Timu ya Simba wanataka kupima uwezo wa VUNJABEI katika utengenezaji na usambazaji wa vifaa vya michezo.
Mkataba huu utakapoisha, tutegemee dili la pesa kubwa zaidi na la muda mrefu zaidi baina ya pande hizo mbili.
Kitaalamu, kila biashara hua ina kitu kinaitwa "Breakthrough point".
Hii ni ile fursa inayokuja na kukukuta tayari umejiandaa, na unapoitumia basi kila kitu kinabadilika ghafla. A game changer Opportunity.
Hili Dili la Simba, ni "Breakthrough point" ya Kampuni ya VUNJABEI.
Je, katika kipindi cha miaka 5 ijayo, unafikiri VUNJABEI atakua anayo maduka mangapi nchi nzima ??
Binafsi, makadirio yangu ni kwamba yatazidi maduka 20.
Tuachane na hayo. Kwa hivi sasa, tuendelee kununua jezi zetu katika maduka ya VUNJABEI.
; Umati wa watu ukiwa umepanga foleni kununua jezi za Simba SC, katika moja ya duka la VUNJABEI.