02/03/2022
Changamoto hii inawakumba sana wafugaji wa kuku.
Sababu zinazopelekea changamoto hii ni k**a zifuatazo.
1. Ukosefu wa maji ya kutosha kwa ajili ya kunywa.
2. Wadudu k**a vile E.coli hivyo hakikisha maranda yanakuwa makavu muda wote. Matumizi ya Glucose kwa muda mrefu huchochea changamoto hii kukua kwa kasi zaidi. Ikumbukwe glucose ni chakula kizuri cha wadudu wa magonjwa, hivyo inashauriwa kuwapa kwa maji safi na salama.
3. Joto kuzidi bandani. Joto likizidi husababisha kuku kukaukiwa maji na hatimaye kusababisha kinyesi kuwa kigumu sana.
4. Ukubwa wa punje za chakula. Ikiwa punje za chakula zitakuwa kubwa hivyo baada ya kumeng'enywa kuku hupata shida kuzitoa k**a kinyesi. Mfano, usimlishe kifaranga wa siku moja Growers mash.
5. Weka vyombo vya maji mbali na chanzo cha joto ili kuzuia maji kuchemka kupitiliza na kufanya kuku washindwe kunywa.
Ahsante.