03/04/2022
π°π°π°π°π°π°π°π°π°π°π°
*MSISITIZO WA MTUME Ψ΅ΩΩ Ψ§ΩΩΩ ΨΉΩΩΩ ΩΨ³ΩΩ
JUU YA KULA DAKU*
ΨΉΩ Ψ£ΩΨ³ Ψ¨Ω Ω
Ψ§ΩΩ Ψ±ΨΆΩ Ψ§ΩΩΩ ΨΉΩΩ ΩΨ§Ω
Kutoka kwa Anas Bin Maaliki ΨΆΩ Ψ§ΩΩΩ ΨΉΩΩ amesema
ΩΨ§Ω Ψ±Ψ³ΩΩ Ψ§ΩΩΩ Ψ΅ΩΩ Ψ§ΩΩΩ ΨΉΩΩΩ ΩΨ³ΩΩ
Amesema mtume Ψ΅ΩΩ Ψ§ΩΩΩ ΨΉΩΩΩ ΩΨ³ΩΩ
ΨͺΨ³ΨΨ±ΩΨ§ ΩΨ₯Ω ΩΩ Ψ§ΩΨ³ΨΩΨ± Ψ¨Ψ±ΩΨ©
Kuleni daku, kwa hakika katika(kula)daku kuna baraka
Al Bukhaariy namba 1923
Muslim namba 1095
*FAIDA ZA HADIYTHI HII*
*FAIDA YA KWANZA*
Amesema Ibn Hajar kula daku hupatikana kwa kichache zaidi ya anachojipatia mtu katika chakula au kinywaji,hadiythi hii imekharijiwa na (Imam )Ahmad kutoka katika hadiythi ya Abuu Sa'iyd Al Khudri kwa lafdh *"KULA DAKU NI BARAKA KWA HIVYO MSIACHE (KULA DAKU)JAPO MMOJA WENU ANYWE FUNDA LA MAJI,KWA HAKIKA ALLAAH NA MALAIKA WAKE WANAWASWALIA WANAOKULA DAKU"* Sa'iyd Bin Mansuur amepokea kwa isnad nyingine ambayo ni mursal: *"KULENI DAKU JAPO NI KWA TONGE MOJA*
Marejeo:FAT-HUL-BAARIY
*FAIDA YA PILI*
Amesema Imam Nawawiy Allaah amrehem,hapa kunamsisitizo juu ya kula daku,ulamaa wamewafikiana kuwa ni sunna wala si wajibu,Ama baraka iliyomo humo,iko wazi kwa sababu daku hutilia nguvu saumu,na hutilia nishati na hupatikana kwa sababu yake Raghba(shauku)ya kuzidi kufunga,kutokana na wepesi wa takhilifu kwa aliye kula daku,huu ndiyo usawa unaotegemewa katika maana yake,na imesemwa ni kwa sababu hujumuisha mtu kuamka,kufanya dhikr na kuomba dua na istighfari(kuomba msamaha)na pengine mlaji daku huenda akatawadha na akaswali au kuchukua mandarizi ya swala mpaka alfajiri itokezapo
Marejeo:SHARHU MUSLIM YA AL IMAAM AN-NAWAWIY
πβοΈ By Al Akhy Abuu 'Uthaymiyn Haarun Ibnul Raashid Assalafiyyu Almaalikiyyu Allaah amuhifadhi
DAARU SSALAFIYYAH MEDIA*
Sasa tunapatikanwa katika mitandao ya kijamii mbali mbali, kwa link zifuatazo:
YouTube π
https://youtube.com/channel/UCx_RKDo3ZKtvrYxfa5F4ObQ
Telegram π
https://t.me/daarusalafiyah
WhatsAppπ
https://chat.whatsapp.com/IlIwTVKC5NjIhIyZRzq2IK
Google π
http://www.daarussalafiya.com/
Instagramπ
https://instagram.com/daarussalafiyah
DAARU SSALAFIYYAH MEDIA TANZANIA:TUSHINDANE NA WAOVU KATIKA MITANDAO MPAKA IBAINIKE HAKKI