02/08/2020
TOFAUTI YA MTU MWENYE FIKRA ZA KITAJIRI NA MTU MWENYE FIKRA ZA KIMASKINI
1. Maskini huamini kwamba ni maskini kwa sababu ya ukoloni au unyonyaji unaofanywa na matajiri au nchi za kibepari LAKINI Tajiri huchukua 💯% ya wajibu wa kwa nini hakufanikiwa katika maisha
2. Maskini wengi huamini kwamba fedha ni mzizi na chanzo cha maovu katika jamii LAKINI Matajiri huamini kuwa ukosefu wa fedha ndiyo kiini cha maovu katika jamii
3. Maskini huamini kwamba kuna mambo ambayo hayawezekani na yanayowezekana, LAKINI Matajiri huamini kwamba mambo yote yanawezekana
4. Maskini hutumia mitandao ya kijamii kupoteza fedha LAKINI Matajiri hutumia mitandao ya kijamii kutengeneza fedha kwa kutangaza biashara na kujibana
5. Maskini hufuja na kutumia muda wake wa 80% kufanya mambo ya kijinga na 20% kufanya mambo muhimu, LAKINI Tajiri hutumia 80% ya muda wake kufanya mambo ya maana na 20% ya muda wake kufanya mambo ya kijamii
6. Maskini huamini kwamba akisoma sana elimu ya darasani atakuwa na maisha mazuri kitu ambacho si kweli, LAKINI Tajiri huamini kwamba akiwekeza muda kusoma vitabu vya watu waliofanikiwa na yeye pia atafanikiwa
7. Maskini wengi huamini kwamba pesa ndiyo kila kitu katika maisha, hudharau mawazo, LAKINI Tajiri huamini kwamba wazo bora ndio huleta pesa na kumfanikisha mtu kimaisha.
9. Watu maskini huamini kwamba elimu ni ufunguo wa maisha na msingi wa maendeleo, elimu ni nuru, mwanga nk. LAKINI watu matajiri huamini kwamba elimu ni nguvu tuli ( potential power) elimu inakuwa ufunguo wa maendeleo binafsi pale mtu anapokuwa anajua kuitumia ili kupata anachokitaka katika maisha yake.
9. Mtu mwenye fikra za kimaskini huamini katika kuajiriwa k**a ndiyo suluhisho la kuweza kupata maendeleo binafsi, LAKINI Mtu mwenye fikra za kitajiri huamini kwenye kujiajiri kwanza kwa njia hiyo ataweza kuajiri na wengine na hivyo kupunguza tatizo la ajira katika jamii.
10. Watu maskini mara nyingi huamini kwamba watafanikiwa kwa kupitia njia za mkato k**a vile rushwa, k**ari na wizi LAKINI.....