09/03/2021
π₯βπ₯βπ₯β
Ukweli unakuja kwamba ili mwaka uwe wa ushindi, mavuno, kuvuna, kuinuka, kusogea, kufika viwango vingine inakupasa wewe binafsi uweke juhudi za kipekee na tofauti. Lazima wewe binafsi ujipange na ukubali kujitoa vya kutosha.
Mabadiliko na maendeleo yako sio muujiza, hakuna mafanikio ya kimiujiza Rafiki yangu. Hakuna mahali utakwenda kupewa nguvu Fulani ambayo itakufanya kila unachokifanya kifanikiwe vile unavyotaka. Acha kabisa kupoteza muda wako mwaka huu kwenda sehemu hizo za kupewa nguvu za namna hiyo.
Kila mmoja anaanza mwaka kwa hamasa kubwa na kelele nyingi lakini baada ya siku chache utaanza kuona kila mmoja analalamika kwamba Maisha ni magumu, mwezi huu haufai na mengine mengi. Baada ya muda sio mrefu sana utaanza kusahau kabisa malengo uliyojiwekea mwaka huu, pia inawezekana mpaka sasa hujaweka malengo yeyote na unasubiria mambo yatokee yenyewe.
Utakuwa unaendelea kupoteza muda wako k**a mpaka sasa hujajua ni vitu gani unataka kwenye mwaka huu. Unajinyima haki zako wewe mwenyewe, unajikosesha fursa wewe mwenyewe, unajiweka kwenye hali mbaya wewe mwenyewe.
Habari njema ni kwamba bado nafasi ipo k**a mpaka sasa hujaweka malengo yeyote anza leo andika kila kitu unachotaka kitokee kwenye Maisha yako mwaka huu. Andika pia ni lini unataka vitokee vitu hivyo na ni vitu gani unatakiwa ufanye ili viweze kutokea k**a unavyopanga
#