18/11/2021
Mgodi ni eneo ambalo madini uchimbwa katika uso wa dunia au chini ya ardhi katika miamba.
K**a zilivyo biashara zingine,uanzishaji wa mgodi pia unahitaji umakini mkubwa kwa sababu ni biashara inayotumia mtaji mkubwa.
Leo Geoswahili tuta angazia baadhi ya mambo muhimu ya kuzingatia ili kuwa na biashara yenye faida k**a ifuatavyo;
1.Hakikisha una elimu ya kutosha kuhusu madini.
-Elimu hii utaipata kwa kuongea na watu wanaochimba madini,wataalam wa madini,kusoma vitabu,kushiriki uchimbaji wa madini katika maeneo mbalimbali na kadhalika.
2.Tambua aina ya madini unayotaka kuchimba,Je ni madini ya metaliki,viwanda,ujenzi,vito n.k
3.Tambua ukubwa wa soko la hayo madini unayotaka kuchimba.
-Je madini hayo yana soko??wapi wananunua??bei ni sh ngapi??yanauzwa kwa kipimo kipi??.
4.Tambua aina teknologia inayohitajika kuchimba madini husika
-Aina ya vifaa vya kuchimbia,mbinu za kuchenjua n.k
5.Tambua aina za sheria na leseni zinazohitajika ili kuanzisha mgodi wa uchimbaji madini.
Mfano;
-Leseni ya uchimbaji.
-vibali vya mazingira.
-muktasari ya kijiji
-usajili wa kampuni n.k
6.Tambua uhalisia wa uwepo wa madini unayohitaji kuchimba katika eneo tarajiwa.
-Tumia wataalam wa uhakika mfano Geoswahili,
7.Tambua miundombinu itakayohitajika katika mgodi wako.mfano;
-Maji safi na salama.
-Barabara za kuingia na kutoka mgodini.
-vyanzo vya nishati.
-Makazi ya wafanyakazi n.k
8.Mtaji wa kuendesha shughuli za uchimbaji madini,mtaji wa uchimbaji madini utajumuisha gharama za mambo yafuatayo.
-Gharama za utafiti wa madini katika eneo husika.
-Gharama za kukata leseni na vibali mbalimbali.
-Gharama za kununua vifaa vya uchimbaji.
-Gharama za kuendeshea mgodi.
-Gharama zingine pia kadri zitakavyojitokeza.
Haya ni baadhi tu ya mambo muhimu katika kuanzisha mgodi ila yapo mengi, kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana nasi.
Geoswahili ni taasisi binafsi,tunatoa huduma za ushauri katika sekta ya madini.
Wasiliana nasi;
Geologist,
Whatsap: +255653855050
Email: [email protected]