11/03/2022
Hello ndugu zangu wapendwa, kuna habari za kuchafuka kwa maji ziwa Victoria na hasa sehemu za mwanzo za maingilio ya maji kati ya mto Mara na Ziwa Victoria katika wilaya ya Rorya ambapo maji yamegeuka kuwa meusi sana na yanatoa harufu kiasi ambacho hayawezi kunyweka ama kutumika kwa matumizi ya kawaida.
Team za serikali ziko kazini kutafuta chanzo cha uchafuzi huo na majibu yakipatikana yatatolewa na serikali kwa wakati wao.
Kwa sasa hali ya upatikanaji wa maji safi na salama kwenye baadhi ya maeneo hayo hasa vijiji vya mwambao na ziwa hilo imekuwa changamoto sana na tunahitaji njia mbadala wa haraka ili kuboresha hali ya maji kwa muda mfupi ili watu waweze kupata mbadala wa upatikanaji wa maji ya kutumia wakati serikali inashughulikia kupata suruhisho la kudumu.
K**a mdau wa maji, afya na mwana mazingira na mtanzania, hili limetugusa sana na baada ya kuongea na mwenyekiti wa Kijiji kimojawapo kilichoathirika cha Kyamwame bwana John Kitende tumekubaliana kuboresha kisima ambacho kilishakuwepo ambapo kinaweza tumika k**a njia mbadala ya watu kupata maji ya kutumia na kunywa wakati serikali inashughulikia tatizo lililopo.
Hivyo, tunahitaji mchango wa hali na mali ili kisima kiweze kuboreshwa ndani ya muda mfupi na watu wapate maji. Kinahitajika kiasi cha shilingi 1,000,000 za haraka ili matengenezo ya hicho kisima yafanyike na watu wapate maji.
Hivyo basi k**a mdau wa maji, afya na mazingira tunaomba mchango wako ili tuweze kuboresha kisima hiki ndani ya siku mbili na maisha upatikanaji wa maji yaweze kuendelea.
Tunaomba utume mchango wako kwa mhandisi Deus Masige 0713483590 ama NMB account ya taasisi ya Mazingira TAEEs namba 23510008869 jina litakuja Tanzania Association of Environmental Engineers.
Tunaomba tushikane mkono katika kipindi hiki kigumu kwa wananchi wetu. ππ½ππ½ππ½