08/11/2021
Kiukweli inauma sana, tumesoma kwa miaka mingi, tumetumia gharama kubwa za ada, tuition, nauli, matumizi, peni, daftari mpaka kufika chuo kikuu lakini baada ya kumaliza ajira hakuna tumebakia kuhangaika. Kiukweli inauma, tuna ambiwa tujiajiri wakati hatukuandaliwa vizuri kwenye sekta hiyo, yani maisha ya sasa kusoma ni k**a kupoteza muda maana hakuna mwenye uhakika k**a elimu itamsaidia ama la. Inauma inauma inauma inauma sana.
Halafu na bodi ya mikopo wanasema tuwalipe pesa zao wakati hatuna ajira wala chanzo cha mapato, zikitangazwa nafasi za ajira wanataka uwe chini ya umri wa miaka 25 au uwe umepitia JKT sasa sisi tulio soma chuo tukiwa na umri mkubwa tukaombe wapi ajira? Je wale ambao hatukupangiwa kwenda jeshini tuombe wapi kazi. Inauma.
Me ndio maana niliamua kuanzisha hii shule ya biashara yani nimeanza upyaa huku nimeunganisha vijana waliopo chuo na walio maliza waje tujaribu kutafuta njia ya kutoboa kwenye maisha maana ajira sio jambo la kutegemea tena.