06/05/2021
UFAFANUZI KUHUSU MAANA YA UREMBO NA VIPODOZI
Biashara ya urembo na vipodozi ni kitu kimoja kwani lengo la mtu kutumia vipodozi ni ili apendeze au kuwa mrembo. Hivyo basi unaposema biashara ya bidhaa za urembo unakuwa unamaanisha vipodozi na vitu vyote vinavyo husiana na watu kupendeza au kuwa katika hali ya usafi na unadhifu.
Hata hivyo kuna baadhi ya watu huweka biashara ya urembo katika kundi lake na biashara ya vipodozi katika kundi lengine kulingana na wanavyoona. Mara nyingi watu hawa huwa wanahusisha urembo na vitu vya kuvaa k**a vile hereni, pete, bangiri, mikufu, nywele za bandia, kucha na kope za bandia. Huku wakihusisha vipodozi na bidhaa zote za ngozi, nywele na manukato k**a vile Cream, losheni, dawa za meno, Pafyumu, sabuni, shampuu na poda.
Lakini kitalamu vipodozi ni kitu chochote kile kinacho weza kutumiwa katika kufanya muonekano wa mtu uwe wa kuvutia zaidi au kuwa na harufu nzuri. Kwa hapa kwetu Tanzania na duniani kote vipodozi hujumuishwa ndani ya kundi kubwa la bidhaa za afya( Health care products ). Biashara ya vipodozi ni moja kati ya biashara zinazodhibitiwa kisheria ( regulated business ) na usimamizi wa biashara ya bidhaa hizi kwa Tanzania bara unafanywa na Mamlaka ya chakula na dawa ( TFDA ).
K**a ulikuwa hujui basi biashara ya urembo na vipodozi ni moja kati ya biashara kubwa duniani ambayo inaingizia watu mamilioni ya pesa kila kukicha. Kwasasa mahitaji ya bidhaa za vipodozi yapo juu sana tofauti na vipindi vya nyuma. Nadhani ukiondoa biashara ya chakula basi biashara ya urembo na vipodozi inashika namba mbili duniani kwa kupanda kwa kasi. Sidhani k**a kuna binadamu leo hii duniani anaweza akajitokeza mbele za watu na kudai hatumii kipodozi cha aina yoyote na k**a yupo basi hana tofauti na wanyama wanaoishi porini.
Narudia tena biashara hii ya urembo na vipodozi ni moja kati ya biashara zinazoenea kwa kasi ya ajabu hapa nchini, karibu kila mtaa huku mjini huwezi kupita hatua chache bila kukutana na duka la vipodozi. Kwa taharifa yako tu biashara ya vipodozi ni biashara ambayo soko lake ni kubwa sana na linaendelea kukua siku hadi siku sasa wewe endelea kuzubaa na kushangaa shangaa mataa tu.
Nakuibieni siri tu k**a mlikuwa hamjui basi biashara hii ya urembo na vipodozi unaweza kuanzisha na mtaji wowote ule haijarishi unamtaji mdogo au mkubwa unachotakiwa ni kuwa mjuzi na mbunifu katika kuindesha na kuisimamia biashara yako. Kwa bahati nzuri biashara hii inaitaji ujuzi kidogo tu katika usimamizi na uendeshaji wake.
Ni ujuzi gani huo ambao unahitajika ili niweze kusimamia na kuendesha vyema biashara yangu ya urembo na vipodozi? Kuwa na mimi katika kipindi kijacho ili uweze kufahamu zaidi.
HITIMISHO
Mwisho wa kipindi hiki ndio mwanzo wa kipindi kingine. Tukutane hapo kesho ili tuweze kuliendeleza gurudumu la maendeleo yetu mbele. Nawaombeni kila mtu baada ya kusoma makala hii hapo alipo kwanafasi yake ainue mikono yake juu kisha amwambie Mungu maneno haya" Asante Mungu kwa kwenda kubadilisha maisha yangu kupitia biashara hii ya urembo na vipodozi🙏🙏🙏".
ZINGATIA
Usisahau kufollow ukurasa huu iliuweze kuwa karibu kabisa na Uncle Rama kwa kuendelea kupata masomo mengi zaidi yanayo husu biashara. Pia usisahau kushare elimu hii, k**a si wewe basi inaweza kumsaidia ndugu, rafiki au jamaa yako.
Mimi ndugu yenu kipenzi RAMA WA KITABUNI
@ Uncle rama