23/12/2019
JE UNAFAHAMU MAANA YA URASIMISHAJI?
Urasimishaji Makazi - Ni kitendo cha kutambua na kuboresha miliki za wananchi kwenye maeneo yaliyoendelezwa bila kupangwa na kupimwa kisheria.
Urasimishaji ni zoezi shirikishi kwa sababu linatoa nafasi kwa kila mwananchi kukubaliana mipaka ya viwanja vyao ,kufungua njia na kutoa maeneo ya huduma za kijamii K**a vile shule, zahanati, maeneo ya wazi ,vituo vya polisi.
Yafahamu Malengo ya urasimishaji Makazi ni K**a ifuatayo:-
1. Kutambua ,kupanga, kupima na kumilikisha kila kipande ili kuongeza usalama wa miliki.
2. Kuongeza huduma za jamii na miundombinu ya msingi K**a vile barabara ,mifereji ya maji, maji ya mvua na masoko.
3. Kuongeza thamani ya ardhi na nyumba ya kuwawezesha wamiliki kutumia miliki hizo K**a rehani ili kupata mitaji kutoka taasisi za fedha.
4.Kupunguza migogoro ya ardhi hususani migogoro ya mipaka.
5. Kupunguza athari zinazotokana na majanga ya asili na magojwa ya mlipuko.
6.Kuongeza wigo wa mapato ya serikali yatokanayo na rasilimali ardhi.
Kwa ushauri wowote juu ya maswala ya ardhi na urasimishaji usisite kuwasiliana nasi kwa namba 0717311995 / 0769881795
Ardhi ni dhahabu