Mr mesha

Mr mesha Tabora stand up

Mungu ana maguvu sana nipo vizuri zaidi ya jana
08/02/2023

Mungu ana maguvu sana nipo vizuri zaidi ya jana

Ukibisha uwe na sababu
30/01/2022

Ukibisha uwe na sababu

Baba bora niyule mwenye family bora
12/10/2021

Baba bora niyule mwenye family bora

24/07/2021

Najua baadhi yenu humu ni wataalamu wa masuala ya anga pia, sasa leo nataka tupeane fact za kutisha kuhusu sayansi ya anga za juu au fact nyingine yoyote lakini lazima iwe ya sayansi; mimi nitaanza na hii kuhusu eneo linalotisha zaidi kuwahi kugunduliwa na wanasayansi Ulimwenguni, hili eneo linaitwa Boötes void au kwa jina lingine linafahamika k**a Great Void ambalo lipo umbali wa miaka milioni 700 ya mwanga kutokea huku Duniani, hili eneo linatisha sana kutokana na weusi wake k**a inavyoonekana hapo kwenye picha yaani sehemu zingine zote kumezungukwa na nyota isipokuwa hapo katikati kwenye weusi ambapo mpaka leo hii wanasayansi wanashindwa kuelewa ni kwanini eneo hilo Ulimwenguni kuwe wazi hivyo. Hili eneo limetanuka kwa ukubwa wa miaka milioni 250 ya mwanga kutokea upande mmoja hadi mwingine, ukubwa ambao ni sawa na asilimia 0.27% ya kipenyo kizima cha Ulimwengu wetu wote ambao wenyewe umetanuka kwa miaka bilioni 93 ya mwanga kutokea upande mmoja hadi mwingine. Hili Boötes void kwa sasa ndilo eneo tupu kubwa zaidi kuwahi kugunduliwa na wanadamu na mpaka leo hii hakuna mtu anayefahamu ni kwanini eneo hili Ulimwenguni lipo tupu na nini ambacho kimesababisha eneo hili la Ulimwengu kuwa tupu bila hata chembe ya nyota, jambo la kutisha zaidi ambalo wanasayansi wanaamini kwa sasa ni kwamba hili Boötes void inaweza ikawa ndiyo mwisho wa Ulimwengu kwa maana hapo ndipo Ulimwengu wetu unapoishia na viumbe vyote Ulimwenguni huwa vinaangamiziwa hapo na pia Boötes void ndiyo inaweza ikawa sababu kwanini mpaka sasa hatujaona viumbe wengine (Aliens) kwa maana walikuwepo kwenye huu Ulimwengu wakaishi k**a sisi kisha wakaangamizwa na sisi pia tutapitia njia hiyo hiyo kuelekea kwenye hilo Boötes void na tukiangamizwa watakuja viumbe wengine yaani hivyo hivyo hii nadharia inafahamika k**a Kardashev III scale civilization, naomba niishie hapa. Tupe fact yako wewe ya kisayansi ya kutisha?

28/06/2021

Muonekano

24/06/2021

"Sayari yetu ni punje pweke ndani ya giza zito lililofunikwa na Ulimwengu. Katika upofu wetu, katika ukuu huu wote wa Ulimwengu, hakuna dokezo kwamba msaada utatoka mahali pengine kutuokoa sisi na chuki zetu wenyewe kwa wenyewe. Dunia ndiyo sayari pekee ambayo kwa sasa inafahamika kuwa na maisha. Hakuna mahali pengine popote, angalau katika siku za usoni sisi kizazi cha wanadamu tunaweza hamia. Uwezekano wa kutembelea sayari hizo ni sawa ila kuhamia na kuanzisha maisha hilo halitowezekana kwa kipindi chetu. Penda au usipende kwa wakati huu Dunia ndiyo sehemu pekee ambayo sisi wanadamu tunajivunia. Imekuwa ikielezewa kwa muda sasa kwamba elimu ya anga imekuwa ikitufundisha unyenyekevu na kutujenga tabia kwa sababu kupitia picha za anga za majuu imetuonesha sisi na majivuno yetu yote ni wapumbavu kiasi gani kutofahamu ya kwamba majivuno hayo yote yanafanyika ndani ya kipunje kidogo kinachoelea kwenye space ambacho sisi ndiyo tunaita nyumbani. Kwangu mimi nikiona picha k**a hizi inaonesha sisi wanadamu inabidi tupendane lakini pia tulipende zaidi na kulitunza pira hili la bluu linaloelea kwenye giza zito ambalo mimi na wewe tunaipa nyumbani na hakuna mahali pengine zaidi ya hapa. " - Carl Sagan

Address

Sinza
Dar Es Salaam
FUTURE

Telephone

+255714658524

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mr mesha posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mr mesha:

Share