05/02/2024
*Anaandika Baba Askofu Benson Bagonza kuhusu kifo cha Kada wa CCM Thadei Ole Mushi*
1. Nimeumizwa sana na kifo chake.
2. Aliwahi kutetea hadharani haki yangu ya kuishi.
3. sikuwa nakubaliana naye mambo karibu yote isipokuwa moja: haki yake ya kusema na kutoa mawazo yake.
4. Hakuwa mvumilivu wa hoja zilizoonekana kuwa nguvu dhidi ya chama chake. Alikuwa tayari kupotosha hoja kinzani bila kunoa ya kwake ikubalike.
5. Niliumia mno alipotokea hadharani kukanusha na kuwazodoa waliokuwa wakituhumu mchezo mchafu juu ya kuugua kwake.
6. k**a kulikuwa na robo ukweli ktk tuhuma zile, basi watesi wake walimtumia kuwasafisha. Hakuna wa kuwachafua sasa.
7. Kwa msimamo wake wa kutetea uhuru wa maoni, alitengeneza maadui ndani ya chama alichokuwa anakitetea.
8. chama chake kinawaheshimu na hata kuwalinda wanaokikosoa wakiwa nje kuliko kinavyoweza kuwavumilia wanaokikosoa wakiwa ndani.
9. Wanaosema hakuwa chawa, hakupenda uteuzi na alijisimamia, wafikiri upy na kupitia maandiko yake.
9. k**a hakuwa chawa basi hatuna chawa.
10. Katika ombwe la fikra pevu miongoni mwa vijana wanaojihusisha na masuala ya siasa, alikuwa pekee kutumia muda wake kuandika na kujadili bila kutukana. Hatunao wengi.
Familia imempoteza mtu muhimu mapema.
Chama chake kimempoteza Mwenezi mwenye hoja kuliko yule.
Wizara ya elimu imempoteza mwalimu hodari aliyeitetea kazi yake.
Kwa heri Ole Mushi. Umeacha nchi gizani, unaenda kaburini penye giza. Yawezekana hakuna ulichopoteza hata k**a sisi twaweza kuwa tumepoteza.
RIP Ole Mushi