Initiative for Human Life Development

Initiative for Human Life  Development Work as partner to the government in order to meet millennium development goals.

EXECUTIVE SUMMARY

IHLD is an Institution of local non – government organization which dedicated to provide quality of social services in order to improve people’s life to the entire society. It was established May, 2013 after seeing a significant number of social problems to the community, that’s are; lack of knowledge and skills to the house maids when it comes to the issue of managing disaster

while at home, first aid management, life skills, and awareness, package on gender based violence, and violence against children, housekeeping. Institution also aims to provide health education, family budget preparation, how to prepare will to the family level, writing work plan, goals setting training, environmental sanitation and conservation, good governance, conflict resolution and peace building, entrepreneurship, agriculture and livestock keeping, marketing strategies to the community. IHLD as a change agent institute intend to empower the marginalized and vulnerable community to social, cultural, political and economical aspects, moreover program aims to link community to utilize available resources for the betterment of the entire life. Through collaboration with local government and other stakeholders, program will accomplish tasks by having the multi disciplinary team with capacity and ability to perform the intended goals. Events like bonanza, sports, games, festivals, theater performance groups, meetings, seminars, workshops and training's will be part of the strategies to meet beneficiaries. Generally institute believes in working with local government with other stakeholders it will in position to reduce or eliminate poverty to the community.

Taasisi ya IHLD inajipanga kuandaa Maonesho ya Bidhaa za Vikundi ya Wakina Mama Wajasiriamali Wadogo Tabata Segerea.
22/09/2020

Taasisi ya IHLD inajipanga kuandaa Maonesho ya Bidhaa za Vikundi ya Wakina Mama Wajasiriamali Wadogo Tabata Segerea.

Usimamizi wa Vikundi1. Jipe Moyo Utaweza (JMU) - Segerea2. Mangumi Youth Group (MY) - Segerea
23/04/2020

Usimamizi wa Vikundi
1. Jipe Moyo Utaweza (JMU) - Segerea
2. Mangumi Youth Group (MY) - Segerea

05/01/2020
🖋
29/09/2019

🖋

03/08/2018

Wiki ya Kimataifa ya kunyonyesha mtoto: Zifahamu faida za kunyonyesha

Tamaduni nyingi zisizomruhusu mwanamke kunyonyesha maeneo ya umma pia ni changamoto kwa wanawake wanaonyonyesha
Wakati ulimwengu ukiadhimisha wiki ya kimataifa ya kunyonyesha mtoto na kuelezea faida zake kwa wazazi na taifa, wakazi wa dunia wanahamashishwa kufahamu umuhimu wa maziwa ya mwanzo kabisa ya mama kwa mtoto .

Takriban 40% tu ya watoto wachanga wenye umri kati ya miezi 0 hadi 6 ndio wanaoishi kwa kunyonyeshwa pekee, kulingana na Shirika la Afya duniani.

Kadhalika Shirika hilo linasema kuwa zaidi ya maisha ya watoto 820,000 walio na umri wa chini ya miaka 5 yanaweza kunusurika kila mwaka, ikiwa watoto wenye umri kati ya miezi 0 hadi 23 wangenyonyeshwa kikamilifu.

Ukweli kuhusu umuhimu wa kunyonyesha:
Kunyonyesha ni moja ya njia sahihi ya kuhakikisha mtoto anakuwa mwenye afya na kuendelea kuishi.

K**a viwango vya kunyonyesha vingekuwa vya hali ya juu duniani, takribani maisha 820,000 ya watoto yangenusurika kila mwaka, linasema Shirika la Afya Duniani (WHO).

Unyonyeshaji wa mtoto kwa miezi 6 kuna faida nyingi za kiafya kwa mama na mtoto.
Kumnyonyesha mtoto mara anapozaliwa kwa kipindi cha saa moja, humkinga kwa maambukizi yanayowapata watoto wachanga na kupunguza vifo vya watoto wachanga.

Maziwa ya mama pia ni chanzo muhimu cha nguvu na virutubisho kwa watoto wa kati ya miezi 6 hadi 23.
Maziwa ya mama yanaweza kuchangia nusu au zaidi ya nguvu za mtoto katika umri wa miaka 6 hadi 12
Watoto na vijana wadogo walionyonyeshwa wakiwa wachanga wana uwezekano mdogo wa kuwa na uzito wa mwili wa kupindukia .
Unyonyeshaji wa mtoto humsaidia kuboresha uwezo wa utambuzi wa akili (IQ), mahudhurio ya shule , na pia huhusishwa na mapato ya juu katika maisha yake ya utu uzima.

Kunyonyeshwa kwa muda mrefu pia huchangia afya na maisha bora ya mama kwani humpunguzia hatari ya kupata saratani ya mfuko wa mayai ya uzazi na matiti.
Kunyonyesha hutengeneza vichocheo vya mwili ( hormone) ambazo humtuliza mama na mtoto

Juma hili linaadhimishwa huku baadhi ya wanawake duniani wakishindwa kuwanyonyesha watoto wao ipasavyo kutokana na sababu mbali mbali.

Takribani 40% tu ya watoto wachanga wenye umri kati ya miezi 0 hadi 6 ndio wanaoishi kwa kunyonyeshwa pekee, kulingana na Shirika la Afya Duniani

Licha ya juhudi mbali mbali ambazo zimekuwa zikifanyika kuelemisha wakina mama na jamii nzima juu ya umuhimu wa kunyonyesha na maziwa ya mama kwa mtoto, baadhi ya mila na tamaduni hususani za Kiafrika zimekuwa na changangoto kubwa ya kuelewa na kukubali umuhimu wa kunyonyesha kutokana na kukosa elimu ya kunyonyesha.

Miongoni mwa changamoto zinachangia wanawake kushindwa kuwanyonyesha watoto wao ni pamoja na kazi, magonjwa pamoja na tamaduni nyingi zisizomruhusu mwanamke kunyonyesha maeneo ya umma.

Aidha baadhi yao wamekuwa na imani potofu kuhusu suala zima la kunyonyesha na faida zake. Hili limechangia pakubwa katika kudhoofisha jitihada za kuhakikisha kila mama mwenye mtoto mchanga anamyonyesha ipasavyo.

Baadhi ya imani potofu kuhusu kunyonyesha:
Maziwa ya kwanza ya mama si mazuri kwa mtoto yanapaswa kumwagwa
Kunyonyesha humfanya mama anenepe kupindukia

maziwa ya mama pekee hayawezi kumridhisha mtoto wa umri wa miezi 0 hadi 6.
Baadhi ya vyakula si vizuri kwa wanawake wanaonyonyesha

Ni lazima mtoto mchanga anywe maji mara baada ya kuzaliwa
Maziwa ya mama humfanya mtoto ajihisi mwenye kiu

Baadhi ya wanawake hudai wanaponyonyesha matiti yao husinyaa na kuanguka.
Shirika la watoto la Save the Children linasema kuwa watoto wenye utapiamlo unaochangiwa na kutonyonyeshwa ipasavyo unakadiriwa kusabisha vifo vya watoto 2.7 kila mwaka.

Wataalam wanasema mguso wa mwili baina ya mama na mtoto wakati wa kunyonyesha husaidia kuchochea uzalishaji wa maziwa ya mama

Wiki ya kimataifa ya kunyonyesha inaadhimishwa huku Serikali na wakazi wa dunia kwa ujumla wakitolewa wito kuwasaidia wanawake kuwanyonyesha watoto katika kipindi cha saa moja ya kwanza ya uhai wake.

Wataalam wanasema mguso wa mwili kwa mwili pamoja na kunyonya husaidia kuchochea uzalishaji wa maziwa ya mama , yakiwemo maziwa ya mwanzo kabisa ya mama baada ya kujifungua ambayo hutambuliwa k**a''chanjo ya kwanza'', yenye virutubisho vingi pamoja na kinga ya ya mwili.

03/08/2018

FURSA

TAASISI YA TEC INAWATANGAZIA VIJANA MANISPAA YA ILALA KUANZIA MIAKA 18-24 KUWA, KUNA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI YANAYOTOLEWA CHINI YA MRADI WA VIA JIANDALIE AJIRA KWA VIJANA, YANATARAJIWA KUANZA TAREHE 18/09/2018. FOMU ZA MAOMBI ZINAPATIKANA OFISI ZA IHLD - SEGEREA. MWISHO WA KURUDISHA FOMU NI TAREHE 24/08/2018.

KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA KWA NAMBA+255 758 258 722
& +255 689 429 132
UKIPATA UJUMBE HUU MTAARIFU NA KIJANA MWENZIO

Life Skills Program for Kids Session Muhimbili Hospital kwa Watoto wanaotibiwa Saratani.  Sisi sote ni Wazazi na hawa wo...
03/06/2018

Life Skills Program for Kids Session Muhimbili Hospital kwa Watoto wanaotibiwa Saratani. Sisi sote ni Wazazi na hawa wote ni Watoto wetu.

02/06/2018
Ushirikiano wako ni Faraja kwa Watoto wetu
26/05/2018

Ushirikiano wako ni Faraja kwa Watoto wetu

Wazazi mnaoajiri wasaidizi wa nyumbani (House Girl/House Boy).  Hakikisha una kitabu maalum cha Kuandikiana kimaandishi ...
25/07/2017

Wazazi mnaoajiri wasaidizi wa nyumbani (House Girl/House Boy). Hakikisha una kitabu maalum cha Kuandikiana kimaandishi kati yako na wafanyakazi wako pale unapomlipa. Usimpe hela kienyeji bila kuandikishiana na kusainishana.

MDs' wa IHLD
17/05/2016

MDs' wa IHLD

BajetiLeo nimeona tuzungumze kuhusu bajeti. Hili jambo limekuwa ni gumu sana miongoni mwetu. Jambo muhimu ni kujua kiasi...
27/04/2016

Bajeti

Leo nimeona tuzungumze kuhusu bajeti. Hili jambo limekuwa ni gumu sana miongoni mwetu.
Jambo muhimu ni kujua kiasi unachopata kwa mwezi ukitoa kodi zote, kiasi ambacho unatakiwa ukipangie matumizi.
Kwa kawaida yapo matumizi ya aina kuu mbili, haijalishi unafamilia au unaishi mwenyewe na aina hizo ni Matumizi ya Lazima na Matumizi ya Ziada.

Matumizi ya lazima ni kwa mfano:
• Fungu la 10
• Kodi ya nyumba
• Ada za shule
• Chakula
• Mahitaji ya nyumbani mfano; sabuni, mafuta n.k.
• Nauli / mafuta ya gari
• Bili za umeme, maji, msaidizi, mlinzi n.k
• Mawasiliano
• Matibabu
• Akiba
Mahitaji ya ziada ni k**a
• Nguo na viatu
• Michango na zawadi
• Burudani
Tenga kiasi kinachohitajia kwa kila kipengele kwa mwezi. Hakikisha fedha uliyotenga inatosha na usibadili matumizi ya fedha bila sababu ya msingi.

Fedha inayobaki kwa mwezi weka pembeni k**a akiba au unaweza itumia kwa matumizi ya ziada. Mara zote hakikisha umekamilisha matumizi yote ya lazima kabla ya kutumia kwa matumizi ya ziada. Na matumizi ya ziada yanaweza yakawa ni kila baada ya kipindi fulani mfano miezi mitatu hadi sita ili kuweka akiba zaidi kuliko kutumia fedha.
Hakikisha unaifuata bajeti yako k**a ulivyojipangia ili uweze kuona mafanikio.
Mwanzo itakuwa ngumu kidogo ila kadiri unavyojizoeza baadaye itakuwa rahisi sana.
Epuka kununua kitu bila kukipangia bajeti. Tumia pesa yako kwa busara kwa mafanikio yako na familia yako. Pia jitahidi kuwafundisha watoto jinsi ya kutumia fedha kwa uangalifu na kwa bajeti.
Bajeti haimaanishi ianzie kwa wenye uwezo mkubwa hapana, ianzie chini popote pale ili kujikwamua kutoka chini zaidi kwenda juu zaidi kimafanikio

Address

Dar Es Salaam
255

Telephone

+255765903379

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Initiative for Human Life Development posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share