05/05/2026
Nilizungumza na mfanyabiashara aliyekata tamaa wiki iliyopita. Alikuwa amekosea mara moja. Mara moja tu.
Anasema: 'Nilifanya uwekezaji mbaya, nikapoteza Tsh. milioni hamsini. Nadhani biashara si fungu langu.'
Nikamwuliza swali moja: 'Je, mtoto anapoanguka akijifunza kutembea, unasema hatembea tena?' Alicheka.
Kisha akaelewa.
Kushindwa si mwisho wa safari — ni sehemu ya mfumo wa kujifunza.
Kila CEO mkubwa duniani ana hadithi ya kushindwa.
Mfabiashara asiye na hadithi ya kushindwa ni mfanyabiashara asiyejaribu kitu kipya.
Tatizo haliko kwenye kukosea.
Tatizo liko kwenye kukosea kitu kilekile mara kwa mara bila kujifunza.
Biashara ni mchezo wa kujifunza haraka kuliko mshindani wako.
- Coach Sereka