Public relations writing

Public relations writing Public relations deals with the writing attempting to establish relation between organization.

QUESTION AND ANSWER ABOUT THE IMPACT OF ENVIRONMENT IN TANZANIA
06/06/2024

QUESTION AND ANSWER ABOUT THE IMPACT OF ENVIRONMENT IN TANZANIA

HISTORIA YA VITA KUU YA KWANZA YA DUNIA
05/06/2024

HISTORIA YA VITA KUU YA KWANZA YA DUNIA

HISTORIA KUHUSU VITA VYA MAJIMAJI Vita ya Maji Maji ulikuwa upingaji mkali wa Waafrika dhidi ya utawala wa kikoloni wa U...
30/05/2024

HISTORIA KUHUSU VITA VYA MAJIMAJI
Vita ya Maji Maji ulikuwa upingaji mkali wa Waafrika dhidi ya utawala wa kikoloni wa Ujerumani katika maeneo ya kusini ya koloni la Afrika Mashariki ya Kijerumani.vilishirikisha baadhi ya makabila ya kusini mwa Tanzania ya leo dhidi ya sera ya Kijerumani iliyoundwa kwa nguvu kuwalazimisha watu wa Tanganyika kulima zao la pamba.
Vita hivyo vilidumu kuanzia mwaka 1905 hadi 1907.

-Chanzo kikubwa cha vita hii ni kwamba wanajamii walichoka kunyanyaswa na wakoloni. Baadhi ya manyanyaso hayo wakoloni waliwataka wanajamii kulima mazao ya kibiashara na walikatazwa kulima mazao ya chakula; kwa mantiki hiyo wanajamii walilima mazao ya biashara na kuacha kulima mazao ya chakula kwa lengo la kuwanufaisha wakoloni huku wao wakipata njaa kwa sababu ya kutolima mazao ya chakula kwa ajili ya kuwapatia chakula na huku adhabu kali ikitolewa kwa wale watakaopinga.

Kwa sababu hiyo wananchi walilazimika kufanya kazi huku wakilipwa mshahara mdogo au kutolipwa kabisa. Watu ambao hawakulazimika kufanya kazi ni watoto wadogo na wazee; kwa wale vijana wenye nguvu walifanyishwa kazi ngumu lakini kwa upande wa wasichana na mama wajawazito waliufanya kazi za ndani.

-Moja ya changamoto walizozipata kwa upande wa vijana wa kiume ni kudhalilishwa kwa kupigwa mijeledi wakiwa uchi mbele ya wanawake wao na pia walitozwa pesa kubwa ukilinganisha na mshahara wanaopata ni kidogo: hizo ndizo baadhi ya changamoto walizozipata. Hivyo basi waliamua kukataa manyanyaso na masumbuko dhidi ya wakoloni.

-Tunaona kwamba wahusika wakuu ni mtemi wa wanajamii Kinjekitile Ngwale na watemi wa Kijerumani.

-Tunaona kwamba mtemi huyu wa kabila la Wangindo aliamini kwamba maji ndiyo silaha ya kipekee ambayo ingetumika kuwashinda wakoloni hata akawaambia wananchi wake kwamba wakoloni wakirusha silaha waseme "maji" kwa madai ya kuwa silaha itabadilika na kuwa maji.

-Wanajamii wake waliamini kusikiliza, kwa hiyo basi vita ilipoanza wakoloni walipoanza kuwashambulia wanajamii walisema, "maji", lakini tunaona kwamba jinsi walivyokuwa wakisema "maji" ndivyo walivyozidi kushambuliwa.

-Tunaona madhara makubwa waliyoyapata: ni wanajamii wengi walipoteza maisha kwa hiyo nguvukazi ilipungua kwa kiwango kikubwa, lakini tunaangalia chanzo kikubwa kabisa ni kupinga manyanyaso pia madhara mengine ni k**a yafuatayo Vifo Kubakwa kwa wanawake Kukumbwa na njaa Mlipuko wa magonjwa Kukosekana kwa nguvu kazi ya jamii Miundombinu kuharibika Kukosekana kwa chakula

30/05/2024

UGONJWA WA CORONA
Virusi vya korona ni jamii kubwa ya virusi vinavyojulikana kusababisha magonjwa yanayoanzia homa ya kawaida hadi homa kali k**a vile Homa Kali ya Upumuaji ya Mashariki ya Kati (MERS) na Homa Kali ya Mfumo wa Upumuaji (SARS).

Virusi vipya vya korona (COVID-19) viligunduliwa 2019 huko Wuhan, China. Hivi ni virusi vipya vya korona ambavyo havijatambuliwa hapo awali kwa wanadamu.

Kozi hii hutoa utangulizi wa jumla wa COVID-19 na virusi vinavyoibuka vya mfumo wa upumuaji na inawelenga wataalamu wa afya ya umma, wasimamizi wa majanga na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa, mashirika ya kimataifa na Mashirika yasiyo ya Kiserikali.

K**a ilivyo jina rasmi la ugonjwa lilianzishwa baada ya kuundwa kwa nyenzo, mtajo wowote wa nCoV unahusu COVID-19, ugonjwa ambukizi unaosababishwa na virusi vya korona vilivyoguduliwa hivi karibuni.

Tafadhali kumbuka kuwa maudhui ya kozi hii yanasasishwa kwa sasa ili kuonyesha mwongozo wa hivi majuzi zaidi. Unaweza kupata taarifa mpya kuhusu mada fulani zinazohusiana na COVID-19

MIAKA 60 YA UHURU WA TANZANIA            Desemba 9 mwaka 1961 mambo makubwa mawili yalifanyika katika sehemu ya maadhimi...
29/05/2024

MIAKA 60 YA UHURU WA TANZANIA

Desemba 9 mwaka 1961 mambo makubwa mawili yalifanyika katika sehemu ya maadhimisho ya uhuru wa Tanganyika,mosi ilikuwa ni kushusha bendera ya mkoloni na kupandisha bendera ya taifa huru na wakati huohuo na kupandisha mwenge wa uhuru katika kilele cha mlima Kilimanjaro tukio hili la kupandisha mwenge haikujulikana sana kwa maana yake hadi pale Baba wa taifa Mwalimu Julius kambarage nyerere alipozungumza mambo yafuatayo kuhusu tukio hilo "tunataka kuwasha mwenge na kuuweka juu ya mlima Kilimanjaro umulike hata nje ya mipaka yetu ulete tumaini pale ambapo hakuna matumaini ,upendo mahali palipo na chuki na heshima palipojaa dharau" miaka 60 baada ya uhuru wa Tanganyika sasa ikifahamika zaidi kwa jina la Tanzania kutokana na muungano wa Tanganyika na Zanzibar wa mwaka 1964.
Huko nyuma miaka michache kabla ya uhuru matukio ya namna hivi yalikuwa yakihusishwa na serikali ya kikoloni na wananchi walipigana kutaka uhuru wao. Watanzania wakati ule walipigana ili wapate haki ya kuchagua viongozi wao waliowataka kwa kuzungumzia matatizo yao kwa uwazi kutofungwa bila makosa au utu wao kutokutetwa kwa namna yoyote ile.
Katika mwaka wa kwanza wa uhuru wa Tanzania ilianza kujipambanua k**a taifa linaloamini katika umajumui wa Afrika Nyerere akielezwa muwa tayari kwa kusubiri Tanzania isiwe huru ili Jomo Kenyatta aachiwe huru kutoka jela Kenya na kuja kuwa raia wa shirikisho la Afrika mashariki na kushiriki katika harakati za kumkomboa mtu mweusi barani Afrika na kwingine duniani
Pia katika elimu Tanzania ilianza kufanya jitihada za makusudi za kusomesha watu wake kwa kuanzisha chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM) na vyuo vingine vya kistadi kiasi kwamba kufikia mwishoni kwa mwaka 1970 Tanzania ilikuwa ikitajwa kuwa mojawapo ya nchi zilizofuta ujinga kwa kiasi kikubwa duniani huku UDSM ikitajwa k**a mojawapo ya vitovu vya fikra za kimapinduzi barani Afrika
Pia Tanzania ilianzisha viwanda vingi vilivyotumia malighafi kutoka kwa wakulima na wazalishaji wengine watanzania na ingawa vipato vyao havikuwa vikubwa.
Kwahiyo katika kizazi cha kwanza cha watawala wa Tanzania kilifanikiwa kufanya jambo moja kubwa kuunganisha watu kutoka makabila,dini, mila na tamaduni tofauti na kutengeneza nchi ya watu wanaojiita watanzania lakini pia kwa kuangalia kuhusu vigezo k**a ujenzi wa barabara, ukuaji wa uchumi, upatikanaji wa huduma na bidhaa muhimu kwa maisha ya watu,tofauti ukilinganisha hali iliyokuwa miaka 60 iliyopita

MAADHIMISHO YA MEI MOSI 2024 YALIYOFANYIKA KITAIFA KATIKA UWANJA WA SHEIKH AMRI ABEID KARUME MKOANI ARUSHA MGENI RASMI  ...
28/05/2024

MAADHIMISHO YA MEI MOSI 2024 YALIYOFANYIKA KITAIFA KATIKA UWANJA WA SHEIKH AMRI ABEID KARUME MKOANI ARUSHA MGENI RASMI SAMIA SULUHU HASSAN.

25/05/2024

Karibu ujipatie simpo shoes za uhakika kwa bei nafuu sana karibu san

Address

Mabibo Mwisho Dar Es Salaam
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Public relations writing posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share