Jongwena Company CO LTD

Jongwena Company CO LTD Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Jongwena Company CO LTD, Business service, DAR ES SALAAM, Dar es Salaam.

29/11/2025

NDOTO ZA KUWEPO KATIKA GARI ( Sehemu ya Kwanza )
Bwana Yesu asifiwe, Namshukuru Mungu muumba mbingu na nchi kwa wema na fadhili zake kila leo.
Tuendele na somo letu la ndoto.
1:UNAPOOTA UPO NDANI YA GARI.
👉Gari katika ndoto hutumika kuelezea maisha yako vile yalivyo mfano ndoa, kazi,biashara, familia na n.k
👉K**a ulikuwa unaombea kazi, ukaota umepanda gari, Ina maana umefanikiwa kupata itaji lako lile ulilokuwa unaliomba.
👉K**a umeota gari linakuhacha,-Ina maana kuna mahali unapaswa upige hatua Ila kuna mkwamo juu yako,inaweza ikawa ni wa kiroho au kimwili au unajikwamisha wewe mwenyewe.
👉K**a Pia umeota umechelewa gari- Hiyo ni Sawa Sawa na kuhachwa na gari,- Ila ujumbe wake hapa upo na mna ya kuweza kukomboa wakati, unaambia maisha yako yapo katika mda ( efeso 5:16 ).
👉Kuota gari limepata ajali- Ina maana kuna anguko au mabaya katika kazi zako au shughuli zako
👉Kuota gari linapita barabara mbovu, ina maana maisha yako hayaendi vile ulivyokisudia.
👉Kuota gari linarudi nyuma,-Ina maana maisha yako yapo katika anguko au kukwama,
👉Kuota gari linakimbia kwa kasi- Ina maana kuna roho ya dhuluma, au Kuibiwa au kutapeliwa inakufuatilia.
Hayo ni baadhi ya tafsiri za ndoto zinazotokana na kuota upo NDANI ya gari, ila zipo nyingi sana inategemea na hali yako vile ilivyo na mazingira yaliopo NDANI ya ndoto.
Shalom shalom.

25/11/2025

NDOTO ZA KUOTA UPO CHOONI.
👉Ukiota unajisaidia haja ndogo- Ina maana Shida zako ndogo ndogo unaenda kuzitatatua.
👉Ukiota umeenda CHOONI umeshindwa kujisaidia haja ndogo,-
Ina maana Kuna kikwazo katika maisha yako zinazokukwamisha kutatua shida zako.
👉Umeota umeenda chooni katika kujisadia haja ndogo umeona ufa Ina maana Kuna fitina zinakufuatilia katika maisha yako.
👉Ukaota upo chooni harafu unachunguliwa Ina maana Kuna aibu inakufuatilia
ZINGATIA: Kwa kawaida ndoto za aina hii uwa zinakujaga mara moja tu kutokana na maisha yako vile yalivyo kwa Wakati huo.

UOTAJI WA MARA KWA MARA- Inaashiria kuwepo kwa kifungo cha miungu juu yako.
Shalom shalom

22/11/2025

NAMNA YA KUOMBEA NDOTO ZINAZOHUSU SAFARI ( KUTEMBEA KWA UZITO NA KUCHELEWA )
1)Baba katika jina la Yesu kristo ninashukuru kwa neema yako na baraka zako zilizokuwa juu ya maisha yangu kila inapoitwa leo, naomba ukanisamehe makosa niliyokutendea, dhambi ninazozijua na nisizozijua, ukanitakase Kwa damu yako ya thamani.
2)Kila roho iliyok**ata nafsi yangu, inayonichelewesha kufikia malengo ishindwe kwa jina la Yesu
3)Kila nguvu ya giza iliyoshikilia hatua zangu ikashindwe na ikaachilie miguu yangu na hatua yangu
4)Madhabahu ya ukoo au mtaa ninapokaa iliyoishikilia nafsi yangu ikashindwe katika jina la Yesu.
5)Adui aliyek**ata saa yangu ya mafanikio na kurudisha nyuma mishale ya saa, dakika na siku na mwaka, leo ninakupiga kwa 🔥 moto, hachilia saa yangu na mda wangu, uende sasa k**a nilivyopangiwa.
6) Kila nguvu ya giza iliyok**ata ufahamu wangu na kunizungusha Sehemu ile ile moja, pasipo kuona matukio au mwanga hachilia ufahamu wangu kwa jina la Yesu.
7) Bwana Yesu niongoze katika hatua zangu, na nifundishe namna ya kufanikisha mipango ya kiroho na kimwili
8)Baba katika jina la Yesu Ninakushukuru kwa kuwa miguu yangu ufanya ya kulungu na kunisimamisha mahali pangu pa juu.
9)Ninakushukuru kwa unafanya mimi kuwa juu, na kuniketisha na wakuu katika jina la Yesu
10)Baba Ninakushukuru kwa sasa malango yangu yapo wazi sasa, wale waliokusudiwa juu yangu ninaendaa kuonana nao, na wale mataifa ( watu wengine ) wanaenda kunitumikia sasa.
Katika jina la Yesu

19/11/2025

KUOTA UNATEMBEA LAKINI HAUFIKI AU UNATEMBEA KWA SHIDA AU KWA UZITO.
Bwana Yesu asifiwe sana ndugu wapendwa, namshukuru Mungu kwa baraka zake na uzima juu ya maisha yetu kila inapoitwa leo.
👉Unapoota unatembea lakini haufiki au unatembea kwa shida ina maana kuwepo kwa roho ya kukuchelewesha kufikia malengo yako au hatima yako.
👉 Malengo ya mtu au hatima yake ipo katika kipindi maalum cha uyo mtu aliyewekewa kuona mema au kufanikiwa, kipo ndani ya mda na wakati wake alionao.
👆 Safari au mwenendo ni kiwakilishi cha mda wako wa mafanikio au nafasi yako ya kiroho kinachokuwezesha kufanikiwa kwako.Vile ambavyo utakavyoonekana katika ndoto unatembea ndivyo ilivyo kwa mafanikio yako katika maisha yako ya kila siku.
Mfano: Kutoka 14:25
[25]Akayaondoa magurudumu ya magari yao, *hata yakaenda kwa* *uzito* ; na Wamisri wakasema, Na tukimbie mbele ya Israeli; kwa kuwa BWANA anawapigania, kinyume cha Wamisri.
👆Tunaona wamisri kadili walivyojitahidi kutembea mwendo wao haukuweza kupiga hatua, ina maana walikuwa palepale katika lile eneo moja,ingawa masaa yalikatika, siku iliisha, kutembea kwao hakukua na maana kwao.
👉👉Ina maana unapoona unatembea haufiki ina maana kuna shambulio la kiroho limekuk**ata au linakuzuia usifanikishe mipango yako, utakuta unafanya biashara lakini haiongezeki, unapambana wewe lakini bado upo palepale miaka yote.
👆 Unaitaji nguvu ya Mungu ikutoe mahali ambapo umek**atwa au kushikiliwa.

KUTEMBEA LAKINI HAUFIKI.
👉 Hii ni baadhi ya kiashiria kunachokuonyesha kuwa mipango yako au malengo yako yatachelewa kutokea kutokana na roho hii iliyokuk**ata au mipango yako uliyonayo.
Mfano: Kumbukumbu la Torati 2:2-3
[2]BWANA akanena, akaniambia,
[3]Mlivyouzunguka mlima huu vyatosha; geukeni upande wa kaskazini.
👆Vipo baadhi ya mambo yatakufanya usifanikiwe au usisonge mbele, mpaka Mungu haingilie kati k**a ilivyo kuwa kwa Musa.
Unaweza ukakaa katika eneo moja mda mrefu bila ya mafanikio au kufaulu.
Shalom shalom

19/11/2025

KUOTA UNAHAIRISHA SAFARI MARA KWA MARA.
👆Wapo watu wanaota wanahairisha safari zao katika ndoto uwa hawasafiri.
Ndoto ya namna hii uwa imebeba ujumbe wa mkubwa katika maisha yako, yaani kuna kiwango kizuri tu ambacho Mungu amepanga ukivuke au ufanikiwe, lakini unajikwamisha wewe mwenyewe ( kuhairisha ).
👉👉Kwa kawaida Mungu wetu uwa anatuwazia mawazo mema katika maisha yetu, na ata wakati mwingine Mungu anatumia ndoto kutueleza mipango yetu, ila kwa kutokujua thamani yetu au ndoto tuzoota tunajikuta tunakwama.
👆 Muhimu la kutafakari katika ndoto yako hii kwanini ulishindwa kusafiri? au kwanini iliahirisha hiyo safari uliyotakiwa kusafiri katika ndoto, au kuna kitu gani kilichokufanya kuhairisha safari yako.
👉Bila kushughulikia ndoto hii ukajikuta unavhelewa Mahali Mungu alichokusudia kwako kufika, yamkini inaweza kuwa kuna kifungo cha giza au kuna mambo ya kuzingatia katika safari yako.
Bwana Yesu awabariki sana.
Shalom shalom

18/11/2025

NDOTO ZA SAFARI ( Sehemu ya kwanza )
Kuota umepotea njia
Bwana Yesu asifiwe, ninawasalimu kwa jina la Yesu Kristo, namshukuru Mungu kwa baraka na kibali chake katika maisha yangu, na wema wake na fadhili zake zilizo kuu kwangu.
👉👉 UNAPOOTA umepotea ina maana gani kwako?
Andiko Yeremia 50:6
[6]Watu wangu wamekuwa kondoo *waliopotea* , wachungaji wao wamewapoteza; wamewapotosha milimani; wamekwenda toka mlima hata kilima, *wamesahau mahali pao pa kupumzika.*
👆Ina maana kuwa umekosea mwelekeo au maelekezo namna ya kufika kule unapaswa kufika ingawa unapajua, pia ni ishara ya kuwa ulikuwa unayemtegemea k**a kiongozi wako hakukuonyesha njia sahihi ya kupita.
👆Pia ni angalizo kuwa makini na kiongozi wako k**a umepotea njia ikiwa yeye ndie muongozaji wa njia hiyo.
Andiko Luka 6:39
[39]Akawaambia mithali, Je! Aliye kipofu aweza kuongoza kipofu? Hawatatumbukia shimoni wote wawili?
👆
Mtu unaemtegemea kuwa atakufikisha salama ndiye uyo atakaekupelekea katika maanguko yako, ikiwa umeota mtu anakuongoza njia.

_Mambo ya kuzingatia_
1)Mungu anaweza kukuonyesha mwenyewe kwa roho mtakatifu ( isaya 49:10 na Zaburi 32:8)
2)Atakuinulia mtu au watu ambao ni sahihi kwako kukuongoza na kukuvusha katika hiyo shida.
Ni muhimu kujua ni eneo gani ambalo Mungu anakupa ujumbe wa kupotea inawezekana ni biashara, mahusiano, au ndoa, au tabia yako na mwenendo wako au kanisani na n.k
Shalom shalom
👆👉👉Tutaendelea👉👆👆

17/11/2025

MAOMBI YA USIKU,.
Zaburi 34:7
[7]Malaika wa BWANA hufanya kituo,
Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.
Zaburi 127:1
[1]BWANA asipoijenga nyumba
Waijengao wafanya kazi bure.
BWANA asipoulinda mji
Yeye aulindaye akesha bure.
👉Baba katika jina la Yesu,nina kushukuru kwa baraka zako na wema wako Bwana wa majeshi.
Ninajifunika kwa damu ya Yesu usiku huu kuanzia utosini mpaka unyayoni.
Ninafunika anga lililo katika nyumba yangu kwa damu ya Yesu
Nina mfunika kila mmoja aliye katika nyumba yangu, nafunika biashara yangu, kazi yangu na ndugu zangu kwa damu ya Yesu.
👉Malaika wa Bwana fanya kituo usiku huu ukizunguka na kulinda nyumba yangu, familia yangu na ndugu zangu
👉 Baba asante kwa kuwa wewe ndie mlinzi wangu wa pekee, unilindae usiku huu, zidi ya mabaya na uharibifu na vita ya usiku katika jina la Yesu kristo Amen

28/10/2025

NDOTO ZINAZOASHIRIA KUWEPO KWA KIFO AU MAUTI ( Sehemu ya kwanza )
Bwana Yesu asifiwe Sana, Leo tutajifunza baadhi ya viashiria vinavyotuonyesha kuwa kuna roho ya mauti inakufuatilia.

Andiko.Mwanzo 49:29
Akawaamuru, akasema, Mimi ninakwenda kukusanywa pamoja na watu wangu; mnizike pamoja na baba zangu, katika pango iliyomo shambani mwa Efroni, Mhiti;

Mwanzo 49:30
katika ile pango iliyomo shambani mwa Makpela, iliyo mbele ya Mamre katika nchi ya Kanaani, aliyoinunua Ibrahimu pamoja na shamba kwa Efroni Mhiti, pawe milki yake ya kuzikia.

Mwanzo 49:31
Humo walimzika Ibrahimu, na Sara mkewe; humo wakamzika Isaka, na Rebeka mkewe; nami humo nikamzika Lea;

Mwanzo 49:32
shamba na pango iliyomo lililonunuliwa kwa wazawa wa Hethi.
Mwanzo 49:33
Basi Yakobo alipokwisha kuwaagiza wanawe, akakunja miguu yake kitandani, akafa, akakusanywa pamoja na watu wake.
👆🏻Kwa kawaida vile ambavyo ulivyo katika jamii, familia, koo na kitaifa, ndivyo na ulimwengu wa roho upo hivyo hivyo, wale unauhusiana nao katika familia, ukoo na taifa ndivyo ilivyo katika ulimwengu wa roho.
👉Unapo ota kuwa umemuona ndugu yako aliyefariki katika ndoto upo nae wa familia moja, inamaana kuwa kuna roho ya mauti inafuatilia hiyo familia yenu.
Katika andiko la mwanzo hapo juu Yakobo aliwaambia wanae ninaenda kujiunga na wazee wangu, yaani kwa Ibrahim na Isaka.
👉Kwahiyo unapomuota ndugu yako aliyekufa katika familia yenu, uyo anawakilisha roho ya mauti inataka kuwepo KATIKA familia yenu au mtu katika familia yenu atafariki.
👉Wakati mwingine unaweza kuota Fulani amefariki umo katika ndoto, hiyo inaashiria uliyemuota anafuatiliwa na kifo, muweke katika maombi.
Kwa kawaida ulimwengu wetu wa mwili uwa unamipaka ya kujua mambo yanahusu maisha yetu, hatujui ya kesho, Ila ukiwa katika ulimwengu wa roho hakuna mipaka au ukomo wa mambo
👉andiko Mwanzo 25:8
Ibrahimu akafariki, naye akafa katika uzee mwema, mzee sana, *ameshiba siku,* akakusanyika kwa watu wake.
Kushiba ndotoni ni ishara ya kifo

04/06/2023

MAOMBI YA KUOMBEA NDOA NA FAMILIA.
Katika familia baba ndie kichwa cha nyumba K**a neno linavyosema katika efeso 5:33.
Katika andiko hilo la efeso neno limeoredhesha vipaumbele muhimu ambavyo ndoa inapaswa kuwa au baba au mama, navyo ni I): upendo ( ii) heshima ( iii ) umoja (iv) utawala (v) kumstahi ( kuwa na adabu.
👉🏻NAMNA YA KUOMBA.
Baba katika jina la Yesu Asante kwa uzima ulionipatia katika maisha yangu siku hii ya leo,baraka zako na wema wako katika maisha yangu, ninaomba ukanisamehe kwa makosa niliyokukosea na dhambi zangu ukanisamehe,ninaomba damu yako ya thamani ikanitakase na kunisafisha nafsi yangu na roho yangu, ninatubu kwa niaba ya mume/mke wangu ninaomba rehema juu yake ninaomba rehema juu ya ndoa yangu baba ukatusamehe familia yangu na watoto zangu tumekutenda dhambi.
1:Baba ninaomba roho ya upendo ikawale ndoa yangu, upendo ukawe ndani ya mume/mke na watoto, tukapande kwa jina la Yesu.
2:Baba ninaomba roho ya umoja Kati yangu na mume wangu/mke wangu na familia yangu
3:Baba ninaomba mamlaka ya utawala K**a kichwa cha familia kikatawale kwa mume wangu, na watoto, ndugu wakamuheshimu mume wangu.
4:Baba nipe Moto wa kumuheshimu mume wangu, niondolee madharau,kiburi,kujiinua na hasira za kijinga katika ndoa yangu.
5:Baba naomba roho ya adabu na hekima katika ndoa yangu ikatawale katika maisha yangu.
Sasa hapo ushaomba kuhusu tabia au mambo yanayochangia anguko katika maisha yako ya ndoa.
👉Sasa Kuna tabia au mambo yanayosababishwa na nguvu za Giza, husuda na vijicho katika maisha ya mtu, uchawi na uganga.
Mfano: mwanzo 11:6-11.
Kisa hichi kinaeleza kuwepo kwa watu wenye malengo sawa na nguvu sawa na umoja wa kufanya Jambo lao na kufanikiwa na walikaa pamoja, Kilichofanyika Mungu alishuka na kuwatawanya wote.
😭 Kwahiyo katika ndoa au mahusiano kumbe anaweza adui akaingia na kusambaratisha umoja na uhusiano wenu badala ya kuelewana mkawa hamuelewani wala kusikilizana.
👉🏻NAMNA YA KUOMBA.
1: Wewe adui ulieingia katika ndoa yangu ili kusambaratisha Ninakuharibu kwa jina la Yesu.
2:Ninaharibu Kila kazi za wachawi katika ndoa yangu, maana imeandikwa hakuna uchawi wala uganga juu yangu Mimi
3:Ninaharibu na kusambaratisha kila roho mlizihachilia kwangu zikishindwe kwa jina la Yesu, iwe mafarakano, kutoelewana, kusikilizana au uzinzi au uesherati.
4:Ninavunja na kusambaratisha kila vikao vyenu vya kichawi mlivyokaa kinyume nami vikashindwe kwa jina la Yesu
5:Ninahachilia amani,upendo,furaha, maelewano, kibari katika ndoa yangu.
6:Ninamleta pamoja mume wangu, mke wangu,mtoto wangu, watoto wangu katika ndoa yangu katika jina la Yesu.
7:Baba naomba neema yako ikatawale juu ya familia yangu, ukamlinde mume wangu,mtoto wangu,mke wangu kwa jina la Yesu.
8:Bariki watoto zangu, fungua fahamu zao mashuleni wanaposoma,wakawe vichwa na si mkia.
9:Bariki nyumba yangu, ondoa magonjwa, umaskini, fungua madirisha ya mbinguni na malango yetu yakawe wazi juu yetu kwa jina la Yesu.
Festo wilfred
5-06-2023

29/03/2023

NDOTO UNAZOOTA.
Bwana Yesu asifiwe wapendwa ninatumaini mnaendelea vizuri na Mungu na Bwana Yesu Kristo,
Kwa kawaida ndoto UNAZOOTA zinatokana na maisha ambayo unayo kwa kipindi hicho au yale uliyapitia katika maisha yako au yajayo katika maisha yako.
Ni muhimu kwa anaitaji tafsiri ili kupata TAFSIRI SAHIHI, akaelezea vile alivyo katika maisha yake kwa wakati huo anapoitaji tafsiri, zipo tafsiri ambazo zinatokana na neno la Mungu moja kwa moja kutokana na ndoto hiyo ulio ota, zipo tafsiri zinaitaji kujua mazingira au mambo unayopitia.
Mfano: Matendo ya mitume 10:9-34, utasoma kwa wakati wako.
👉Kisa hapo kinaeleza Petro kuona maono, yale maono aliyoyaona hakutambua maana yake ila kadili ya mazingira aliyokutana nayo na kujishughulisha katika mazingira yale akaelewa maana ya maono na kupata majibu yake na ikampa wepesi wa kutokuwa mpinzani kwa kile anacho amini.
👉🏻Zipo ndoto nyingine unaota kutokana na mawazo unayowaza wakati kabla haujalala inapelekea kuota usiku, sasa hapo inategemea umewaza Nini? ( Mathayo 1:20)
Yusufu alikuwa anatafakari au anawaza kuhusu mimba ya Mariam, ikampelekea kuota ndoto usiku.
Ni muhimu sana kwa anaeitaji tafsiri kujua chanzo cha hiyo ndoto, kabla haujaota ulikuwa kwenye hali gani.
Shalom shalom
Festo wilfred ( 29-3-2023 )

Address

DAR ES SALAAM
Dar Es Salaam
255

Telephone

0718904632

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jongwena Company CO LTD posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share