Fungua Kampuni YAKO SASA

Fungua Kampuni YAKO SASA Tupo kuusaidia umma kiuchumi katika usajili wa biashara; usajili na kufungua kampuni; leseni za biashara na vibali vingine vya kubiashara na makampuni

NAMNA YA KUFUNGUA KAMPUNI:-Nchini kwetu namna ya kufungua kampuni hufanywa kulingana na Sheria ya Makampuni Namba 12 ya ...
26/09/2017

NAMNA YA KUFUNGUA KAMPUNI:-
Nchini kwetu namna ya kufungua kampuni hufanywa kulingana na Sheria ya Makampuni Namba 12 ya mwaka 2002 k**a inavyofanyiwa marekebisho ya mara kwa mara.

Kwa ufupi mlolongo mzima wa kufungua kampuni unamezwa ns vipengele vifuatavyo hapa chini:-

(A) Upatikanaji wa jina la kampuni chini ya usimamizi wa BRELA; dhumuni ya hili ni kuhakikisha jina la kampuni halifanani au kuwa na ukaribu sana na jina la kampuni nyingine.
Pia jina kutokuwa na maana isiyofaa mfano matusi.

(B) Kutayarisha Katiba ya kampuni na kanuni/taratibu za kampuni "Articles of Association" na "Memorandum of Association" ambazo hutayarishwa na wanasheria kisha kuwasilishwa kwa msajili na baada ya kupitiwa na kujiridhisha msajili atatoa hati ya usajili "Certificate of incorparation"

(C) Kujaza fomu Namba 14a na 14b kwa mujibu wa Sheria ya Makampuni Mamba 12 ya 2002.
Hii ndio namna kwa ufupi na uchache wa taratibu za kufuata ili kufungua kampuni.

Kwa namna rahisi ni vizuri kumshirikisha mwanasheria katika hill kwani kuna taratibu nyingi za kisheria zinazopaswa kufuatwa.

Siku nyingine nitaeleza mambo ya kuhakikisha unafanya kabla na baada ya kufungua kampuni.

25/09/2017

FAIDA ZA KUFUNGUA KAMPUNI
Kampuni ni muunganiko wa watu zaidi ya mmoja (yaweza kuwa rafiki, baba, mama, Dada, kaka nk) wa kibiashara na kusajiliwa chini ya Sheria Na.12 ya 2002.

Kumekuwa na dhana potofu ya kwamba kampuni ni kwaajili ya wafanyabiashara wakubwa tu.
Bila kujali unafanya biashara gani (muuza kuku, mama ntilie, muuza mihogo, mkulima nk ) kwa maendeleo ya sasa ya kibiashara na teknolojia kuwa na kampuni ni jambo lisiloepukika.

Fikiria mwekezaji anaetaka kufungua kiwanda cha "chocolate" anaitaji maziwa ya kutosha, itamuia vigumu nfugaji wa kawaida kufanya biashara na mwekezaji huyu bila kuwa na kampuni. Jiulize kampuni hiyo ya mwekezaji je itaweza kufanya mikataba na mfugaji wa kawaida? au kampuni.
Hivyo ndivyo wafanyabiashara wengi wamekuwa wakikosa fursa za kiuchumi na za kifedha.

Wakulima wengi wamekuwa wakikosa faida huku kampuni ambazo zinanunua mazao kwa wakulima hao na kusafirisha nje ya nchi zikifaidika.
Mkulima anaelima nanasi anapata faida ndogo sana kuliko kampuni yenye tenda ya kusafirisha mananasi hayo South Africa tena kulipwa kulingana na uzito wa mzigo na si wingi.

Hivyo umefika wakati kwa jamii kuacha kufanya biashara kizamani na kimazoea.

Hizi ni kati ya faida nyingi za kufungua kampuni.
- kuwa na uwezo wa kufanya biashara
zaidi ya moja (tofauti tofauti).
- kupanua fursa za kiuchumi za ndani na
za kimataifa.
- kupata mkopo kirahisi katika taasisi za
fedha.
- kuwa na uhakika wa kuendelea kufanya
biashara hata unapokuwa na tatizo mf
ugonjwa.
- kuongezea kampuni haifi mpaka sheria
itamke hivyo.

Address

Ilala. Kariakoo, Mtaa Wa Swahili Na Udoe
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 08:00 - 06:30
Tuesday 08:00 - 06:30
Wednesday 08:00 - 06:30
Thursday 08:00 - 06:30
Friday 08:00 - 06:30
Saturday 08:30 - 05:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Fungua Kampuni YAKO SASA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share