26/09/2017
NAMNA YA KUFUNGUA KAMPUNI:-
Nchini kwetu namna ya kufungua kampuni hufanywa kulingana na Sheria ya Makampuni Namba 12 ya mwaka 2002 k**a inavyofanyiwa marekebisho ya mara kwa mara.
Kwa ufupi mlolongo mzima wa kufungua kampuni unamezwa ns vipengele vifuatavyo hapa chini:-
(A) Upatikanaji wa jina la kampuni chini ya usimamizi wa BRELA; dhumuni ya hili ni kuhakikisha jina la kampuni halifanani au kuwa na ukaribu sana na jina la kampuni nyingine.
Pia jina kutokuwa na maana isiyofaa mfano matusi.
(B) Kutayarisha Katiba ya kampuni na kanuni/taratibu za kampuni "Articles of Association" na "Memorandum of Association" ambazo hutayarishwa na wanasheria kisha kuwasilishwa kwa msajili na baada ya kupitiwa na kujiridhisha msajili atatoa hati ya usajili "Certificate of incorparation"
(C) Kujaza fomu Namba 14a na 14b kwa mujibu wa Sheria ya Makampuni Mamba 12 ya 2002.
Hii ndio namna kwa ufupi na uchache wa taratibu za kufuata ili kufungua kampuni.
Kwa namna rahisi ni vizuri kumshirikisha mwanasheria katika hill kwani kuna taratibu nyingi za kisheria zinazopaswa kufuatwa.
Siku nyingine nitaeleza mambo ya kuhakikisha unafanya kabla na baada ya kufungua kampuni.