Child Welfare

Child Welfare We provide a specialized welfare, consulting service dedicated to the parenting and child protection

05/02/2026

🌟 HUDUMA YA KUWAJENGEA VIJANA STADI ZA MAISHA 🌟

Je, wewe ni kijana au mzazi unayejali mustakabali wa kijana wako?
Tunatoa mafunzo na usaidizi wa stadi za maisha ili kuwasaidia vijana:

βœ… Kujiamini na kujitambua
βœ… Kufanya maamuzi sahihi
βœ… Kudhibiti hisia na msongo wa mawazo
βœ… Kuwasiliana kwa ufanisi
βœ… Kujiepusha na tabia hatarishi
βœ… Kujenga ndoto na malengo ya maisha

🎯 Huduma zetu zinawalenga:

Vijana wa shule na vyuo

Vijana walioko nje ya mfumo wa elimu

Vijana wanaojiandaa na maisha ya kazi na uongozi

πŸ“ž Wasiliana nasi leo:
+255 754 761 389

πŸ‘‰ Tuandikie au tupigie kwa maelezo zaidi.
Tuwaandae vijana wa leo kuwa viongozi wa kesho.

🟦 Malezi ya watoto na mahitaji yao kulingana na umriπŸ‘Ά Miaka 0–5: Upendo na usalama hujenga ubongo wa mtoto.πŸ§’ Miaka 6–12:...
05/02/2026

🟦 Malezi ya watoto na mahitaji yao kulingana na umri
πŸ‘Ά Miaka 0–5: Upendo na usalama hujenga ubongo wa mtoto.
πŸ§’ Miaka 6–12: Kosa ni nafasi ya kufundisha, si kuumiza.
πŸ§‘β€πŸ¦± Balehe: Sikiliza kwanza kabla ya kusahihisha.
πŸ‘¨ Baba: Uwepo wako una nguvu kuliko zawadi.

02/01/2026
05/11/2024

Hatua muhimu za kuzingatia na kumsaidia mtoto katika Makuzi na Maendeleo kwa umri.
Kuzaliwa hadi miezi minne (0 – 4)
Maendeleo ya Hisia/Ufahamu
β€’ Mtoto mwenye afya anaweza kuona, kusikia na kunusa mara baada ya kuzaliwa. Huitambua sauti ya mama yake, harufu na sura yake.
β€’ Baba yake ni muhimu sana kwa maendeleo ya mtoto, hivyo ashiriki katika kumtunza mtoto.
β€’ Mtoto anaweza kujifunza mengi kutoka kwa ndugu zake, na wao kutoka kwake, hivyo inatakiwa ndugu wacheze naye na kusaidia kumtunza
β€’ Kumbembeleza akikasirika humsaidia kujenga imani na kuwasilisha hisia zake kwa mzazi/mlezi.
β€’ Kunyonyesha maziwa ya mama kunamleta mtoto kuwa karibu, kulelewa kwa upendo na kujenga mahusiano.

Mawasiliano
β€’ Mtazame mtoto machoni na utabasamu (kwa mfano wakati wa kumnyonyesha). Kuongea nae kwa kumtazama usoni, kurudia sauti zake na kumuimbia itamsaidia kujifunza kuwasiliana.
β€’ Atatambua na kuhisi akiguswa na mama yake, akimtazama, akitabasamu na kwa sauti yake. Atajaribu kuwasilisha mahitaji yake kwa kujongea, kutoa sauti mbalimbali na kulia.
Kujongea
β€’ Mapema mtoto huitambua miguu na mikono yake. Kumuacha aitumie miguu na mikono yake kutamsaidia kuwa mkak**avu.
β€’ Ataanza kufikia vitu na kuviweka mdomoni kwa sababu hujifunza kwa ladha na kugusa.
Atajaribu kuinua kichwa ili kuona vinavyomzunguka. Msaidie kwa kumbeba ukiinua kichwa chake na mgongo ili aweze kuona. Kumuacha abingirike kwenye sehemu salama kutamsaidia kukomaza misuli.

05/11/2024

Zipo athari zinazompata mtoto k**a hakutakuwa na mahusiano ya karibu na mzazi/mlezi wake. Athari hizo ni k**a ifuatavyo;
β€’ Mtoto kujisikia hayuko salama
β€’ Kuchanganyikiwa
β€’ Kutokuamini mtu
β€’ Kuwa na hasira na msongo wa mawazo
β€’ Kushindwa kufanya chochote
β€’ Kutokuwa na mahusiano mazuri na watu wengine ukubwani
β€’ Watoto wanaokosa mahusiano mazuri na mzazi/mlezi hukosa kujiamini na baadaye katika maisha hupata shida kupambana na mazingira, hukosa ushirikiano mzuri na wenzao, hukosa uwezo wa kutatua matatizo yao na msukumo wa kimaendeleo. Hivyo watoto wote walelewe katika familia kwa upendo na pale inaposhindikana kabisa ndio wapelekwe kwenye vituo maalum vya kulelea watoto.

Mahusiano ya karibu kati ya mtoto na mzazi  Huu ni mchakato wa mtoto mchanga kujenga mahusiano na mama au baba na hii in...
05/11/2024

Mahusiano ya karibu kati ya mtoto na mzazi

Huu ni mchakato wa mtoto mchanga kujenga mahusiano na mama au baba na hii inasababishwa na mwitikio wa baba au mama kwa mtoto.
Hutokea katika miaka miwili ya mwanzo hasa kati ya miezi miwili na miezi saba baada ya mtoto kuzaliwa. Wakati huu mtoto huanza kujenga njia binafsi za mawasiliano kati yake na mzazi/ mlezi wake.

20/09/2024

KUZUNGUMZA NA MTOTO ALIYOPO TUMBONI/KABLA YA KUZALIWA

Baba na mama wanapaswa kuongea na mtoto kabla hajazaliwa, akiwa bado tumboni. Watoto wanaweza kutambua sauti za binadamu wakiwa bado tumboni na baada ya kuzaliwa wanaweza kuzisikia sauti hizo kuwa za kufurahisha na zinatambulika. Kuongea na mtoto tumboni kunaimarisha uhusiano na imani ya mtoto baada ya kuzaliwa.
β€’ Wazazi watarajiwa, mama na baba wanapaswa kuongea na mtoto akiwa tumboni kuhusu wanakokwenda na wanafanya nini, kumsimulia hadithi, kuimba nyimbo, na kumwelezea kuhusu ulimwengu ambao unamngojea mtoto.
β€’ Wakati wa ujauzito, baba ana fursa ya kujongea karibu na tumbo la mama kuzungumza na mtoto kuliko mama. Baba ambao humpatia utulivu mtoto tumboni wanaweza pia kuwa wazuri katika kumtuliza mtoto kwa sauti yao baada ya kuzaliwa.
β€’ Mama na baba ambao wanatumia muda pamoja wakifurahia kuongea na kuimba kwa mtoto wao tumboni wanaimarisha ukaribu, upendo, na uaminifu wao kwa kila mmoja pamoja na kwa mtoto aliye tumboni.
β€’ Ongea na kumwimbia mtoto, ukijua kuwa anaweza kusikia, humsaidia mtoto kutambua sauti na kuimarisha uhusiano baada ya kuzaliwa. Mtoto mchanga anaweza kuhisi faraja, akiwa anaijua tayari sauti ya mama au baba yake. Pia inaweza kumsaidia katika maendeleo ya lugha na mawasiliano.
β€’ Katika kipindi cha karibia wiki 14, mtoto wako anaweza kuanza kusikia sauti yako. Tumia vidokezo hivi vya ujauzito kuzungumza na mtoto wako: imba nyimbo za kubembeleza au wimbo wako unaoupenda, soma gazeti au kitabu cha watoto kwa sauti, zungumza na mtoto wakati ukiwa peke yako na unapokuwa umechoka, zungumza na mtoto unapotembea ndani ya nyumba, shambani, au bustanini, n.k.

20/09/2024

Kuzungumza na watoto wachanga wa umri wa mwaka 0 hadi 1 (Walengwa: watoto wachanga wa umri wa hadi mwaka 1)
Wazazi na walezi wanapaswa kutumia kila fursa ya kuzungumza, kuimba, kucheza na kuwasiliana na watoto wachanga kwa sababu ubongo wao unakua kwa kasi, unabeba na kuchakata taarifa mpya ambazo zinafungulia njia mpya za ufahamu.
β€’ Wazazi na walezi wanapaswa kuzungumza, kuimba, na kucheza na watoto tangu kuzaliwa kwao kwani hii huusaidia ubongo wa mtoto kukua na kuendeleza uwezo wake. Mtoto atapata faraja kwa sababu ya sauti yako na atajua kuwa unamjali.
β€’ Mama, baba, na walezi ambao husikiliza kwa makini wanaweza kujifunza maana ya sauti tofautitofauti ambazo mtoto huzitoa kabla hata hajaweza kuzungumza.
β€’ Kurudia sauti za mtoto kwa sauti kubwa na kuangaliana naye mara kwa mara kunasaidia kuchochea maendeleo ya lugha na mwenendo wa kijamii.
β€’ Wakati watoto wachanga wanapolia, huwa wanajaribu kuwasiliana. Mtoto anayelia anaweza kuwa ameshtushwa, au kushangazwa, anaweza kuwa anahisi joto sana, baridi sana, au njaa na anahitaji kula. Anaweza kuwa na gesi tumboni na anahitaji kusaidiwa, au nguo zinahitajika kubadilishwa. iWanaweza pia kuwa wanamea meno yameanza kuota au kujisikia kuumwa, au wanahitaji tu kubebwa na kuhisi kupendwa.
β€’ Haiwezekani kumharibu mtoto. Watoto wachanga wanafaidika na wanahitaji upendo, kuwajali, na umakini wote wanaoweza kupata. Wazazi na walezi wanaweza kumsaidia mtoto kuelewa na kuzingatia ratiba k**a vile wakati wa kulala bila kusababisha mtoto kuhisi wasiwasi au kutelekezwa.
β€’ Shughuli na mazungumzo ambayo wazazi na walezi wanaweza kufanya na watoto wachanga:
o Maelezo ya kitu chochote kinachotokea - unachokifanya, unapoenda, na unachokiona. Elekeza na mwonyeshe mtoto vitu unavyovielezea.
o Ongelea kuhusu rangi tofautitofauti, hesabu hatua unazozipiga au vyakula unavyovitayarisha, ongelea na iga sauti tofautitofauti za wanyama.
o Wakati mtoto wako anapotoa sauti, mjibu kwa kurudia sauti hizo na kuongeza maneno. Hii husaidia kujifunza kutumia lugha.
o Soma na kumsimulia hadithi mtoto wako. Hii husaidia kukuza na kuelewa lugha na sauti.
o Mwimbie na kumpigia muziki mtoto wako. Imba pamoja na redio. Hii humsaidia mtoto wako kuendeleza upendo wa muziki na kukuza maendeleo ya ubongo.
o Mpongeze mtoto wako na tumia muda wa kumbembeleza na kumbeba mtoto wako kwa sababu hii inaonyesha upendo na usalama.
o Cheza na mtoto wako wakati akiwa macho na mwenye utulivu. Angalia ishara k**a amechoka. Mara nyingine wanahitaji kupumzika baada ya kucheza.
o Vuta akili ya mtoto wako kwa midoli na umpeleke mtoto mahali salama wakati wanapoanza kutembea na kugusa vitu ambavyo hawapaswi kuvigusa.

18/09/2024

Kuhamasisha nidhamu Chanya

Mama, baba na walezi wanaotumia njia zisizo za ukatili katika kusimamia nidhamu ya mtoto watatambua kuwa ina ufanisi sana na husaidia kujenga mazingira ya nyumbani yenye usalama, upendo, na amani.
Adhabu ni kumletea mtoto maumivu ya kimwili ambayo humfanya mtoto aumie. Watu wazima huwapa adhabu watoto wanapofanya kitu kinachodhaniwa kuwa kibaya au kisicho sahihi. Adhabu huleta chuki na hasira kwa mtoto na kwa matokeo yake haileti mabadiliko mazuri ya tabia.
β€’ Ikiwa mzazi anachagua kupiga k**a adhabu, mtoto anaweza kujeruhiwa.
β€’ Inaweza kusababisha madhara ya kimwili, ambayo kwa upande wake yanaweza kusababisha ulemavu mdogo au mkubwa na wakati mwingine hata kifo.
β€’ Adhabu inaweza kusababisha matatizo ya kihisia kwa mustakabali wa mtoto.
β€’ Kwa mujibu wa uzoefu, watu wazima wengi ambao walipewa adhabu wakiwa watoto wanakuwa na tabia za ukatili na unyanyasaji kwa watoto na wanafamilia wao.
β€’ Kadri adhabu inavyozidi kuwa kali, uwezekano wa mtoto kupoteza imani, kuwa mkatili, mhalifu, au hata mgonjwa wa akili unazidi kuongezeka.

Mambo/Maswali ambayo wazazi na walezi wanapaswa kujiuliza kabla ya kutumia adhabu.
β€’ Lengo la adhabu ni kumfundisha mtoto au kupunguza hasira tu?
β€’ Je, mtoto anaweza kuunganisha adhabu aliyopewa na kitendo chake kibaya?
β€’ Je, adhabu inatolewa kulingana na sheria ya adhabu?
β€’ Je, kuna adhabu mbadala ambayo ni nyepesi lakini bado inaweza kuleta matokeo mazuri yanayokusudiwa?
β€’ Je, adhabu inadhalilisha, ni yenye ukatili, au ni kali kiasi cha kumfanya mtoto asistahimili?

Send a message to learn more

18/09/2024

Lishe bora wakati wa ujauzito (walengwa: Mama na mtoto aliyeko tumboni)
Baba na wanafamilia wote wanapaswa kuwahamasisha wasichana, wanawake, wajawazito, na akina mama wapya kula vyakula bora na vya aina mbalimbali vinavyopatikana katika maeneo yao, kwani hii itawasaidia kuepuka matatizo wakati wa ujauzito na kujifungua watoto wenye afya njema.
β€’ Kula milo mitatu ya chakula bora na kupata vitafunwa muda wote ni vizuri ili kukidhi mahitaji ya lishe bora ya mama na mtoto. Vitafunwa vyenye kiasi kizuri cha virutubisho k**a matunda, mboga, nafaka, na maziwa vinafaa zaidi.

β€’ Kula aina mbalimbali za vyakula bora ni muhimu wakati wote wa ujauzito. Hii inajumuisha matunda na mbogamboga, maharage, nyama, samaki, maziwa, kuku na dagaa.
β€’ Wakati wa kuhudhuria kliniki, mhudumu wa afya atachunguza hali ya lishe ya mama mjamzito, kutoa ushauri kuhusu lishe bora na mtindo wa maisha na kutoa virutubisho kwa ajili ya matokeo bora ya ujauzito.
β€’ Kumtunza mama mjamzito ni jukumu la jamii nzima. Ili kusaidia mimba zenye afya na wanaozaliwa, baba, wanafamilia, waajiri na washiriki wengine katika jamii wanapaswa kupunguza mzigo wa kazi kwa wanawake wajawazito na kuwahimiza kupumzika na kula vizuri.

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Telephone

+255715761389

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Child Welfare posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share