10/02/2022
*Zijue aina za uchafu na harufu sehemu za siri kwa mwanamke!*
Njia ya uzazi huanza kutoa majimaji wakati wa balehe. Hii ni hali ya kawaida. Maji yanayotoka ukeni huwa yamechanganyika na vimelea. Maji maji haya husaidia kuondoa ngozi ya uke iliyokufa hivyo kufanya uke kuwa katika hali ya usafi na yenye afya.
Iwapo sehemu ya uke inatoa harufu kali au uchafu usiokuwa wa kawaida hali hiyo hutokana maambukizi au magonjwa mengine.
1.Uchafu laini wenye rangi ya kijivu/mweupe wenye harufu k**a shombo ya samaki
Hali hii husababishwa na ugonjwa unaojulikana k**a Bacterial Vaginosis. Harufu husikika zaidi baada ya tendo la ndoa
2. Uchafu wenye rangi ya njano ama kijani wenye harufu k**a yai viza.
Hali hii husababishwa na Ugonjwa ujulikanao k**a Trikmona (Trichmonas). Dalili nyingine ni maumivu wakati wa tendo la ndoa na wakati wa kukojoa. Pia mama hupata miwasho sehemu za siri.
3. Uchafu wa rangi ya njano k**a usaha sehemu za siri
Hali hii husababishwa na ugonjwa wa Kisonono. Hata hivyo karibu nusu ya wanawake wenye Kisonono hawana dalili zozote.
4.Kuongezeka kwa majimaji sehemu za siri (Uchafu mwingi usiokuwa wa kawaida)
Hali hii husababishwa na ugonjwa wa Klamidia (Chylamidia).Wanawake wenye maambukizi hawana dalili.
5.Uchafu mzito,mweupe k**a maziwa mgando hauna harufu.
Hali hii husababishwa na maambukizi ya fangasi sehemu za siri.
6. Damu au uchafu wenye rangi ya kahawia(brown)
Hali hii inasababishwa na maambukizi kwenye mfuko wa uzazi au saratani ya kizazi