16/11/2023
Sasa nitaeleza namna ya kujitafuta na kujipata kwa kutumia concept ya Ikigai
Ikigai ni nini?
Neno hili la kijapani lina maana sababu ya kuishi kiswahili reason of being, kingereza raison d'etre kifaransa.
Ikigai ni vile vitu vinakupa mwelekeo wa maisha na kukupa hamasa ya kusonga mbele.
Tafiti zilifanyika huko Japan baada ya kuona watu kule wanaishi miaka miingi sana (zaidi ya 100) wakiwa na afya amani na furaha. Pamoja na mambo mengine ilionekana sababu kuuubwa sana ni "ikigai"
Hebu angalia maisha ya watu wa zamani hapa kwetu Tanzania halafu angalia maisha ya watu wanaoishi sasa tena zaidi wale wa.tabaka la kati walioajiriwa na waliojiajiri.
Umri wa kustaafu kwa Tanzania ni miaka 60 je, unaona nini kinatokea kwa wastaafu wengi? Kwa haraka haraka kuna mambo makubwa matatu hutokea.
1. Kupata maradhi ya kudumu yasiyoambukiza
2. Kufilisika hata baada ya kulipwa fedha nyingi
3. Kutokuwa na furaha
Kustaafu kumekuwa kwa kuogopesha mno kiasi wengine hawataki hata kustaafu wengine wanadanganya hata umri.
Lakini ni kweli tunatakiwa kustaafu? Je, ukistaafu kazi umestaafu maisha? Neno kustaafu ama retirement halipo kwa vocabulary za wenzetu wajapan kwa sababu hawastaafu yaani wanaendelea kutimiza wajibu wao hapa duniani. Wamejipanga. Wako active mpaka umri mrefu.
Tunawezaje kujitafuta na kujipata sasa.
Kwa kutumia mchoro hapo juu tutaweza kupata kujua kwanini tunaishi kwanini tumekuja duniani na nini sababu au wajibu wetu. Kitu kinachokufanya uamke asubuhi. Hapa naukumbuka sana msemo wa *_"mbeba maono hafi"_* tunauchukulia poa k**a vile kuna watu specific ndo wana kazi maalumu hapa duniani kumbe hata mimi na wewe ni watumwa, watumishi hapa duniani kila mmoja kwa nafasi yake.
Angalia mchoro kwa makini kisha anza kujaza majibu kwa kutumia huo muongozo hapo.
Tenga walau saa moja, tafuta mahali pa utulivu chukua peni na karatasi/notebook tafakari kwa kina upate majibu sahihi kwani wewe ndo unayeweza kumtafuta wewe na kumpata. Majibu yako waweza kushare na watu wako wa karibu wanaokufahamu na kukujua na walio tayari kusema ukweli wanaweza kukuongezea ila usije beba maoni ili uwaridhishe chukua kile kinacholeta maana kwako.
1.
Hapa ni kile kitu ukifanya unapata burdaani ndani yani amani kabisa na kuwa na nguvu, kukufanya uwe hai na mwenye furaha na raha. Mifano ni mingi yaweza kuwa kuogelea kukimbia kusoma kupiga stories na washkaji, kuabudu, kuandika nk. Usiangalie unachoweza bali unachopenda
2. /AMBACHO WEWE NI MKALINWAO
Hapa inajumuisha mambonyote ambayo wewe ni mzuri katika kuyafanya. Uwe umejifunza au ni hobbies tu au vipaji ulivyonavyo. Mfano kuchora, kupiga chombo fulani cha mziki, kuimba, public speaking upasuaji(madaktari) kupika kushauri nk.
Hapa angalia vile unavyoweza bila kuangalia passion wala malipo. Yani kitu unakiweza haswaaa
3.
Hapa dunia inajumuisha kujitoa kwako kwa jamii inayokuzunguka na ulimwengu wote. Hii yaweza kuwa kile unachokiona wewe au wengine wanakiona inawezekana dunia inahitaji madaktari wanawake, wataalamu wa IT yanahitajika maji safi na salama, chakula bora, mbegu bora mafunzo ya vijana nk.
Angalia sana kile kinachohitajika bila kuweka mahitaji yako mbele kwenye hili eneo
4. KWA KUKIFANYA
Nini unaweza kufanya ukapata maokoto. Angalia nyuma sasa k**a passion yako vipaji vyako ujuzi wako.je, nini unaweza kufanya na ukalipwa? Je, ni kuandika, kuongea, nini ulichonacho ni hot sokoni?
UKIMALIZA HILO ZOEZI UTAANGALIA KILE KILICHOTOKEA SEHEMU ZOTE NNE NDO IKIGAI YAKO
Yaani utaona ni kitu
Unapenda kufanya hata bure
Unaweza kufanya
Dunia/jamii inakihitaji
Ukifanya kinaweza kukulipa.
Ni zoezi rahisi halafu gumu ila lina maana kuubwa sana kwa maisha yetu. Tusizurulezurule tu tukaenda zetu muda ukiisha. Tufanye vitu vya kutufurahisha na kuwanufaisha wengine lakini vinatuingizia maokoto.
[Mambo muhimu5 ya kuzingatia
1. Anza taratibu, focus kwenye mambo muhimu
2. Jitambue wewe mwenyewe na kujikubali
3. Tafuta amani na mwendelezo. Shiriki/shirikisha na watu wengine
4. Furahia mambo madogomadogo uliyonayo uyakuzeIshi sasa sio kesho