31/12/2022
Mungu akikufikisha 2023 salama achana na tabia ya kuwatafuta watu ukiwa na shida. Huu ni ushamba.
Halafu unapoomba kitu ukanyimwa uache kuwatishia watu maisha kwamba hakuna ajuaye kesho! Kwani wewe kesho unaijua?
Jenga utamaduni wa kuwasalimia jamaa zako mara kwa mara ili hata ikitokea dharula ni rahisi kukushika mkono kuliko kuibuka tu wakati unashida.
Inakugharimu nini kuwasalimia ndugu zako? Hii tabia ya kusema una ndugu wengi matajiri lakini hawakusaidii bali unasaidiwa na watu baki unaisababisha mwenyewe.
Sikiliza, salamu ni nusu ya kuonana! Achana na tabia za kujipa umuhimu kwenye maisha ya watu,acha tabia mbaya na za hovyo unapoingia 2023!