27/06/2018
MWANAFUNZI FESTIVAL
JUNE 29- UKUMBI BCIC MBEZI BEACH...... KITUO JOGOO..
MATANGAZO
Kila siku: Radio WAPO 98.1 FM.. Kila siku matangazo
Alhamisi June 28: Radio WAPO FM-kipindi Meza ya busara....saa 4 mpaka 6 mchana
Ijumaa June 29.. SIKU YA TUKIO: TBC 1..asbh saa 12 mpaka 12.
Habari watanzania wenzangu.
Napenda kuchukua fursa hii kuwakaribisha katika Tamasha la Mwanafunzi(Mwanafunzi Festival) awamu ya pili,ambalo litafanyika Ijumaa wiki hii,BCIC Mbezi Beach,unapitia/kushukia kituo cha Jogoo karibu na Interchick. Tamasha litaanza saa mbili mpaka saa 10 Jioni. Mwaka jana tulikuwa na wahudhuriaji wapatao 1,958(waliofika na kujiandikisha kwenye daftari).
KWA UFUPI. Vijana wetu,waliowengi hawajui wanawezaji kufanikiwa katika masomo yao wawapo shuleni ili wafaulu kwa kiwango cha juu ndio MAANA tunawaletea WANAFUNZI WALIOONGOZA KITAIFA ili watuambie walitumia mikakati gani,waliishi maisha gani wakiwa wanafunzi yaliyowafanya VINARA.
Elimu,ni njia mojawapo ya kumfanya mwanadamu awe na taaluma Fulani,mfano Mhandisi,Mwanasheria,Mhasibu, Daktari n.k. Je Mwanafunzi atumie vigezo gani kuweza kujua asomee nini ,kile ambacho kinaendana na kipaji chake ili afanikiwe na aweze kuishi maisha mema. Kwenye kongamano,ndio maana utakutana na wataalamu waliobobea katika fani mbalimbali.
Pamoja na hayo,je watoto wataweza wenyewe bila wazazi? Kila mzazi ana nafasi ya kumuwezesha mtoto wake. Je mzazi afanye nini katika kizazi hiki na wakati huu tunapoona muda umekuwa changamoto?
Kongamano litakuwa na wazungumzaji wengi,ambao ni pamoja na Joel Nanauka( Mwanafunzi bora-kidato cha Nne 2002 na mhamasishaji maarufu), Lusekelo Kibona-Mwanafunzi Bora kidato cha sita 2002 na Mwanafunzi wa PHD, Rais wa DARUSO-Mlimani , Mchumi Ahobokile Mwaitenda, Dr. Lurakuze kutoka Muhimbili, Mwalimu Mkwachu, Mkufunzi na mtaalamu wa Elimu Adam Mnyavanu, Christopher Andendekisye-mkurugenzi wa Mwanafunzi Clinic, Allen Kimambo- Mkurugenzi na Mwanzilishi wa wa Zaidi Recyclers na Championi wa TakaNi Ajira; pamoja wanafunzi wengine walioongoza Kitaifa na wengineo wengi.
ENDELEA KUSIKILIZA WAPO RADIO.
WAJULISHE NA WENGINE. Kwa maelezo zaidi... 0653234010