28/02/2018
UMUHIMU WA MAJI KATIKA MWILI
Maji huunda zaidi ya theluthi mbili ya miili yetu, lakini wengi wetu huacha kunywa maji na kunywa vinywaji vingine wakisahau kunywa maji ya kutosha.
Takwimu zinaonyesha kuwa mwili wa mwanadamu umejengwa kwa asilimia kati ya 55 na 75 za maji na watu wembamba wana kiasi kikubwa cha maji mwilini kuliko wanene. Kwa sehemu kubwa tumetokana na maji, hii ni sababu zaidi ya asilimia 94 ya damu yetu ni maji, zaidi ya asilimia 85 ya ubongo wetu ni maji.
Asilimia 60 ya uzito wako ni maji na mifumo ya mwili wako hutegemea maji ili kufanya kazi zake kwa ufanisi. Unapoanza kuhisi kiu, mwili unakuwa umepungukiwa na maji. Hata katika upungufu mdogo wa maji mwilini, asilimia moja hadi mbili ya uzito wa mwili hupungua, suala hilo humfanya mtu akose nguvu na ajisikie amechoka.
Upungufu sugu wa maji mwilini (chronic dehydration) ndio chanzo cha magonjwa mengi kwa mwili wa binadamu ambayo kisababishi chake kilikuwa hakijulikani.
Kwa asili, upungufu sugu wa maji mwilini unamaanisha upungufu wa kudumu wa maji ambao umedumu kwa muda fulani. K**a ilivyo kwa maradhi ya upungufu wa kiini lishe fulani, mfano upungufu wa vitamini C kwa ugonjwa wa kiseyeye (scurvy), upungufu wa vitamini B kwa ugonjwa wa beriberi ama upungufu wa madini ya chuma kwa ugonjwa wa anemia, upungufu wa vitamini D kwa ugonjwa wa matege/nyongea na mengine unayoyafahamu; namna mahususi ya kutibu magonjwa hayo ni kurudishia kiasi kilichopungua. Kwa mujibu huu, ikiwa tutaanza kutambua mkanganyiko wa kiafya uletwao na upungufu wa maji, uzuiwaji wake na hata udhibiti wake wa mwanzo utakuwa ni rahisi.
Mwili unahitaji kwa kiasi kikubwa maji ili kufanya kazi zake vema. Kwa mfano, mapafu yako yanahitaji vikombe viwili vya maji hadi vinne kila siku ili kufanikisha kazi yake ya upumuaji kwa ufanisi. Na kiasi hicho huhitajika zaidi wakati wa baridi. Kunywa glasi nane za maji au robo lita kila siku ndio kiwango ambacho kipo akilini mwa wengi, wote wakiwa na imani kwamba ndicho kiwango kinachokubalika kiafya, si kweli!
Mahitaji ya maji yanatofautiana kati ya mtu na mtu. Mambo k**a jinsia, hali ya hewa, kiwango cha joto la mwili, ushiriki wa mazoezi, aina ya kazi, umri na aina ya mlo unaokula kulingana na kundi lako la damu ni mambo ambayo yanapaswa kuzingatiwa.
Ukweli ni kwamba kiwango cha maji ambacho unachopaswa kunywa kinatofautiana baina ya mtu mmoja na mwingine.
Mwenye uzito wa kilogramu 45 mpaka 49 anahitaji kunywa lita 1.9 hadi 2.0, mwenye uzito wa kilogramu 50 hadi 54 anahitaji kunywa lita 2.1 hadi 2.2, hali kadhalika kilogramu 55- 59 kwa lita 2.3 hadi 2.4 na kuendelea.
Maji yanapaswa kubaki ndani ya mwili masaa mawili mpaka mawili na nusu ili kuupa mwili muda wa kutosha kuyatumia maji hayo vizuri.
Ikiwa inakulazimu kukojoa chini ya muda wa masaa mawili tangu unywe maji, pamoja na hatua nyingine muhimu tofauti utalazimika:
• Kuacha kunywa maji matupu, jaribu kunywa juisi (uliyotengeneza mwenyewe) ya chungwa, juisi ya matunda mchanganyiko, ya zabibu au juisi nyingine yeyote kulingana na kundi lako la damu na hali ya mwili wako, isipokuwa kwa watu wanaosumbuliwa na pumu (asthma) ambao hawatakiwi kunywa juisi ya chungwa. Wakati huo huo muhimu kukumbuka kuongeza robo tatu gramu za chumvi katika kila nusu lita ya juisi yako.
• Kuhakikisha unakunywa maji kwa mujibu wa kipimo chako kulingana na uzito wako. kunywa maji mengi zaidi ya kiwango chako husababisha maji kutoka nje ya mwili mapema kabla hayajatumiwa na mwili.
• Achana kwanza na matumizi ya kinywaji chochote cha kutengenezwa kiwandani, acha chai ya rangi na kahawa. vinywaji hivi ni mawakala vikojoshi (diuretics), huyalazimisha maji kutoka nje ya mwili mapema kabla mwili haujayatumia. utarudi kunywa chochote ikiwa utavihitaji tena vinywaji hivyo mara utakapokuwa sawa kwa mara nyingine tena kiafya. Acha pia uvutaji wa sigara na au pombe.
Maji yana faida nyingi katika mwili ikiwa ni pamoja na kusaidia umeng’enyaji wa chakula, huboresha hali ya viungo na misuli, maji yanaweka ubongo katika hali nzuri zaidi ya ufanisi zaidi hivyo kunywa maji ya kutosha kunamuwezesha mtu kufikiria vyema zaidi, husaidia kupunguza uwezekano wa kupata baadhi ya magonjwa k**a mafua na kusaidia kupona haraka ugonjwa huo, mawe ya figo, matatizo ya ini, baadhi ya saratani na magonjwa mengine.
Ikiwa unataka kupunguza unene na uzito, pamoja na taratibu maalum, sahihi na salama, maji pia huchochea kukusaidia kwa kiasi kikubwa kwa kuwa huongeza kasi ya shughuli za kimetaboliki na kufanya mwili kutumia nishati nyingi zaidi, hivyo kupunguza kiasi cha nishati kitakachohifadhiwa mwilini katika hali ya mafuta hivyo kuchangia kupunguza unene na uzito kiujumla.
Nguvu zetu hazitokani na vyakula tunavyokula, bali zinatoka katika maji ambayo yanaiweka atomu ya haidrojeni katika chakula.
Vyakula tulavyo hutupatia vitamini na madini tunayoyahitaji ili kubaki katika afya. Ikiwa mwili haupati maji halisi (glasi 1 au 2) kabla ya kula chakula na kusubiri (robo saa au nusu saa), basi mwili lazima ujikope maji wenyewe.
K**a mwili utakopa maji toka katika damu, basi ateri lazima zipunguze vipenyo vyake na moyo lazima utumie nguvu nyingi ili kusukuma damu ambayo ni nene (nyingi), kitendo hiki tunakiita 'shinikizo la damu' (BP).
Ikiwa mwili utajikopa maji toka katika ubongo, utapatwa na 'kichwa kizito' au kichwa kuuma ambacho kinaweza pelekea maumivu ya kichwa.
Ikiwa unakunywa pombe na inavuta maji toka kwenye ubongo, utapatwa na kutokujisikia vizuri au uchovu (hangover).
Kokote katika ogani au tishu mwili utakakokopa maji, lazima ogani au tishu hiyo iachiwe madhara na hivyo kusababisha maumivu ama ufanyaji kazi wa ogani au tishu hiyo usio wa kawaida .
Kila tunapopumua hewa nje (exhale) tunapoteza maji. Ikiwa utahema juu ya kioo, utauona ukungu (maji). Tunapoteza glasi 4 za maji kwa kupumua tu kila baada ya masaa 24!
K**a mwili utakopa maji toka mapafuni, utapatwa na pumzi fupi itakayopelekea upatwe na pumu (asthma) na matatizo mengine yanayohusiana na mfumo wa upumuaji.
Mapafu na moyo vinauhusiano wa karibu, kwa hiyo k**a mwili utakopa baadhi ya maji toka katika mishipa ya moyo, utapatwa na maumivu ya moyo ambayo yanaweza kurahisisha kutokea kwa shambulio la moyo (heart-attack).
Mishipa inahitaji damu na maji wakati unafanya mazoezi, kwa hiyo k**a unatakiwa kula chakula na kisha kutembea au kupandisha ngazi (za ghorofa) na una upungufu wa maji (dehydrated), unaweza ukapatwa na pumzi fupi, shambulio la pumu, utapatwa na maumivu ya moyo (angina) au kukak**aa kwa mishipa (cramps).
Ndiyo maana tumekuwa tukisikia, kamwe usiende kuogelea mara tu baada ya kumaliza kula kwa sababu mishipa itakak**aa. Mwili unapokuwa katika kazi yake ya umeng'enyaji chakula, huielekeza (diverts) damu toka katika mikono na miguu kwenda katika utumbo mdogo ili kusaidia umeng'enyaji wa chakula. Baadhi ya vyakula ni rahisi kumeng'enywa na huwezeshwa na maji pekee, k**a vile matunda na mboga za majani.
Vinywaji vingine (liquid beverages) k**a vile kahawa, chai, soda , pombe na juisi, si maji kwa mwili. Hivi ni vyakula pia kwa sababu ulimi unaipata ladha ya viongezi (additives) na sio ladha ya maji halisi, na hivyo mwili utakishughulikia kinywaji hicho k**a chakula.
Utafaidika na baadhi ya maji k**a vile katika matunda na mboga za majani kwa masharti ya kinywaji hicho kutokuwa na kafeina (caffeine). Kafeina ni kikojoshi (diuretic), huyalazimisha maji kutoka nje ya mwili.
Kunywa maji masaa 2 hadi 2 na nusu baada ya chakula kunasaidia kumalizia umeng'enyaji wa chakula na kuunywesha mwili maji baada ya kukaukiwa kulikosababishwa na kazi ya umeng'enyaji wa chakula.
Njia bora ya kuupa mwili maji ya kutosha ni kutii kiu chako kila unaposikia kiu inabidi unywe maji ya kutosha. Njia nyingine ni kuchunguza mkojo wako kwa makini kuanzia rangi na harufu yake, ikiwa una rangi nzito na harufu kali hii ina maana mwili hauna maji ya kutosha.
Kwa wale wanaofanya mazoezi, watu wengi hupoteza kati ya lita moja na mbili za jasho kila saa moja la mazoezi ya kawaida. Hivyo mtu anapaswa kurudishia maji yaliyopotea kupitia jasho ingawa kuhisi kiu bado ndio mwongozo wa moja kwa moja wa kunywa maji.
Ripoti ya makubaliano iliyochapishwa na British Journal of Sports Medicine, ilidai wanamichezo wengi wako katika hatari ya kupatwa na ‘Hiponatremia’ (upungufu wa chumvi ya natri katika damu) inayotokana na michezo tatizo linaloweza sababisha mtu kunywa maji mengi hivyo anaweza kusababisha kichefuchefu, kutapika, kuumwa kichwa, uchovu na wakati mwingine huweza kusababisha matatizo makubwa k**a kupoteza fahamu na hata kifo.
Ili kujilinda na kupungukiwa au kutozidisha kiwango cha maji, ni vyema kuusikiliza mwili wako unachotaka. Kunywa maji safi na salama kwa kiasi kinachostahili kiafya kunaweza kuboresha maisha na kuimarisha afya.
Tunaweza kufupisha hapa kuwa, kutokana na mazoea yetu ya kusubiri kiu au mdomo ukauke ndipo tunywe maji, huwa tunaulazimisha mwili kuishi katika mfumo wa mgawo wa maji na hatimaye usambazwaji wake, mfumo huo ndio huleta hatari mwilini kwa kuzalisha ishara mbalimbali za magonjwa ambayo dawa yake pekee ni kubadilika kwetu na kuanza kunywa maji kabla ya kusikia kiu na kujifunza umuhimu wa maji kwa maisha marefu bila magonjwa.
Kuna maajabu zaidi ya milioni katika glasi moja ya maji kuliko dawa yoyote utakayotumia.
ANGALIZO:
• Ili kuhakikisha figo zako zinafanya kazi vizuri, ni lazima kiasi cha maji unachokunywa kiwe karibu sawa na kile unachotoa.
• Wakati huo huo, kwenda chooni mara nyingi kwa siku kunaweza kukusababishia kupoteza vitamini muhimu, madini na elektrolaiti na kukufanya vibaya zaidi ya vizuri.
• Unatakiwa kuwa makini sana unapoanza kuongeza uchukuaji wa maji mwilini, anza pole pole kwa kuongeza glasi 1 kila siku mpaka utakapofikia kiwango cha maji unayohitajika kunywa. Lazima uupe mwili muda wa kujirekebisha badala ya kuzoea vinywaji k**a kahawa, chai na soda, kwa kuwa vinywaji hivi huufanya mwili kujiendesha kwa namna nyingine tofauti na inavyopaswa.
• Unaweza kuumwa na kichwa au unaweza usijisikie vizuri tu siku tatu mpaka wiki moja za kuanza kujizoeza kunywa maji kiwango unachotakiwa, usiache kunywa maji kwa kuwa hayo si madhara bali ni dalili kuwa taka na baadhi ya sumu ambazo zimelundikana ndani ya mwili wako katika mifumo tofauti zimeanza kuvunjwavunjwa mwilini. Zoezi ambalo huhitaji msaada zaidi sambamba na matumizi ya maji katika kufanikisha zoezi hili.