Layers Pro

Layers Pro Tunawasaidia Wafugaji wa kuku Kuongeza Kipato Chao Kupitia Mbinu Bora za usimamizi wa mradi

Kuku wanamaliza chakula mapema Nitafanyaje chakula kilo 5.5 kitoshee mpaka siku 60?๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐ŸฝHabari yako, leo nilipa...
24/04/2026

Kuku wanamaliza chakula mapema Nitafanyaje chakula kilo 5.5 kitoshee mpaka siku 60?

๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

Habari yako, leo nilipata ugeni wa mama cheupe [sio jina halisi] huyu ni mteja wangu mzuri wa CFP za kuku wanaokua hapa Dodoma

Leo alikuja dukani na alikuwa ana changamoto yake ambayo ni hii "afanyaje chakula kitoshee mpaka siku 60" nilimpa ushauri wa nini Cha kufanya ili chakula kilo 5.5 kitoshee mpaka siku 60

Inawezekana huelewi hii dhana ya chakula kilo 5.5 imetokea wapi, usiwaze... Iko hivi mfumo wetu wa ulishaji wa kuku chotara umegawanyika sehemu mbili

Sehemu ya kwanza ni kuanzia siku 1 mpaka siku 25 ambapo kuku mmoja anakula chakula kilo 1 sehemu ya pili ni kuanzia siku 25 mpaka siku 60 ambalo kuku mmoja anakula chakula kilo 4.5

Kwahiyo kuanzia siku 1 mpaka siku 60 jumla kuku chotara mmoja anakula chakula kilo 5.5 si tumeelewana?

Sasa Ikiwa na wewe unapata changamoto hiyo ya chakula kilo 5.5 kutofika siku ya 60 Fanya mambo yafuatayo

1.Kwanza pakua hii chati ya kuku wa sasso ambayo utaitumia kujua kiwango cha chakula wanachokula kila siku kuanzia siku 1 mpaka siku 60

Kupakua hiyo chati bofya hii link hapa๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

https://drive.google.com/file/d/1JyGNxKDUKYsQyaQAkHvE0KB-702M1Mhr/view?usp=drivesdk

๐Ÿ‘‰๐ŸฝK**a huwezi kupakua hii chati tafuta mtu akusaidie kuipakua na unaweza kwenda nayo stationery wakakuchapishia ukawa na nakala ngumu [hard copy]

๐Ÿ‘‰๐ŸฝChati hii ni ya sasso na tunaitumia kwa kuku chotara aina zote, hatuna chati za chotara wengine k**a unayo unaweza kuitumia.

2.Jambo la pili Jifunze kutumia hiyo chati kwa kuangalia hii video hapa kwa kubofya hii link ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

https://youtu.be/ssrq3vHNL0o

๐Ÿ‘‰๐ŸฝK**a unapata changamoto kuangalia hii video tafuta mtu akusaidie namna ya kufungua hii video ya YouTube najua tunatofautiana!

3.Jambo la tatu hakikisha unawalisha kuku kwa kipimo kila siku k**a ambavyo hiyo chati inaonesha kiwango husika kwa kila siku

Hapa unahitaji mzani, k**a Bado huna mzani tupigie 0752 912132 kuagiza mzani wa kidijitali bei yake ni 20,000 na unapima kuanzia gram 100 mpaka kilo 50. Pia unaweza kufika ofisini kwetu Moshi Agrovet tunapatikana Dodoma Majengo Sokoni

Zingatia kwamba kiwango cha chakula wanachokula kitakuwa kinabadilika kadri wanavyokua siku kwa siku

4.Ulishaji wa chakula ni asubuhi na mchana utagawa chakula nusu kwa nusu yaani k**a kuku wako chotara wanakula chakula kilo 20 kwa siku utawapa kilo 10 asubuhi na jioni utawapa kilo 10

๐€๐๐†๐€๐‹๐ˆ๐™๐Ž

Jifunze jinsi ya kuwalisha kuku wako kwa kufuata viwango vinavyoelekezwa kupitia hiyo chati

Tafadhali sisi hatutakufanyia hayo mahesabu ndio maana tumeandaa chati na hiyo video ili uweze kujifunza na kufanya wewe mwenyewe kila siku hapo bandani kwako.

Ni rahisi Wala sio ngumu

Asante sana kwa usikivu wako kwenye hili suala ๐Ÿ™๐Ÿฟ

CFP
Ulishaji wa uhakika

Tanbro wamefikisha siku 14 Leo wastani wa uzito wao ni gram 286.13, uzito wa kawaida kwa kifaranga wa siku 14 ni gram 20...
21/04/2026

Tanbro wamefikisha siku 14 Leo wastani wa uzito wao ni gram 286.13, uzito wa kawaida kwa kifaranga wa siku 14 ni gram 204 [narejea performance chart ya sasso- tunaitumia kwa chotara wote]

Mpaka siku 14 vifaranga wote wamekula chakula kilo 115.8 maana yake ulaji wa chakula Uko vizuri

Nitaweka clip ya Hawa vifaranga kwenye comment unaweza kuitazama hapo.

Vifaranga hawa tumewachanganyia chakula kuanzia siku 1 kwa kutumia hii formula, tuliwachanganyia chakula kilo 300 ๐Ÿ‘‡

Mahindi paraza kilo 156
Soya kavu kilo 96
Mashudu ya alizeti kilo 27
Mafuta kilo 6 [tumia alizeti, korie etc]
CFP ya vifaranga kilo 15

Jumla kilo 300

K**a unahitaji CFP tafadhali wasiliana nasi, CFP kwasasa zinapatikana hapa

1.Dodoma, Majengo Sokoni pembeni ya CRDB MAJENGO

Mawasiliano ๐ŸŽ๐Ÿ•๐Ÿ“๐Ÿ๐Ÿ—๐Ÿ๐Ÿ๐Ÿ๐Ÿ‘๐Ÿ ๐š๐ฎ ๐ŸŽ๐Ÿ•๐Ÿ๐Ÿ– ๐Ÿ๐Ÿ—๐Ÿ ๐Ÿ‘๐Ÿ•๐Ÿ–

2.Dar es salaam, Ubungo

Mawasiliano ๐Ÿฌ๐Ÿณ๐Ÿญ๐Ÿฑ๐Ÿฒ๐Ÿฒ๐Ÿฌ๐Ÿณ๐Ÿณ๐Ÿญ

3.Iringa mjini

Mawasiliano ๐ŸŽ๐Ÿ•๐Ÿ”๐Ÿ‘ ๐Ÿ—๐Ÿ‘๐Ÿ• ๐ŸŽ๐Ÿ‘๐Ÿ•

4.Arusha mjini

Mawasiliano ๐ŸŽ๐Ÿ•๐Ÿ—๐ŸŽ ๐Ÿ•๐Ÿ—๐Ÿ— ๐Ÿ•๐Ÿ”๐Ÿ”

haiwezekani kuku ana siku 35 awe hivo ukitembelea mabanda ya wafugaji wengi  kuku k**a hao unakuta wana miez miwil had n...
19/04/2026

haiwezekani kuku ana siku 35 awe hivo ukitembelea mabanda ya wafugaji wengi kuku k**a hao unakuta wana miez miwil had nanusu

๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

Nitaweka picha ya hao kuku wa siku 35 ili uwaone, tuliwapost Alhamisi trh 26 March 2026

Tuendelee kujibu hii hoja...

Iko hivi Ukuaji wa kuku unategemea mambo haya makubwa matatu : aina ya kuku, chakula na mfumo wa ulishaji

1.Aina ya kuku

aina tofauti za kuku chotara zina ukuaji tofauti mfano aina hii kwenye picha huwezi kulinganisha ukuaji wake na chotara wengi wanaofahamika, kiukuaji Hawa ukuaji wao uko juu

Hapa kwenye aina ya kuku ongezea na ubora wa vifaranga, yaani aina inaweza kuwa ile ile ila vifaranga wasiwe na ubora

Kwenye picha Hawa ni kuku wapya kwahiyo bado hawajafamika k**a hao wengine [sitaki kuwataja kwa kuheshimu majina ya biashara za wengine] sisi wenyewe tumewafuga wakati tunafanya majaribio ya formula ya vifaranga kuanzia trh 5 January 2026

2.Chakula kutegemeana na unatumia chakula gani itaathiri ukuaji wa kuku wako hapa hata k**a ni Cha kununua dukani au kuchanganya mwenyewe vyakula havifanani

3.Mfumo wa ulishaji kuanzia kiwango cha chakula, masaa ya mwanga, aina ya ufugaji [k**a ni huria,nusu huria au wanafungiwa bandani] na nafasi bandani hivi vyote vinaathiri ukuaji wa kuku

Kwenye comment nitakuwekea video ya Tanbro, kwa mwaka Jana tumefuga sana Tanbro mpaka wafugaji wakawa wanahisi labda CFP ni kwa ajili ya Tanbro ndio maana tulipoanza kutoa darasa kuhusu formula ya vifaranga mwaka huu tukaamua kutumia vifaranga wa hii kampuni ya SQ ili kuondoa dhana kuwa CFP ni kwa ajili ya Tanbro

๐Ÿ‘‰ Muhimu Post zetu tunaweka picha kwa ajili ya kujifunza sio kwa lengo la kutangaza biashara ya vifaranga wanaonekana kwenye picha kumbuka sisi Hatuuzi vifaranga โŒ [Effect inaweza kuwepo ila hii inaitwa unintended project goal]

Hivyo amua wewe mwenyewe utafuga vifaranga wa chotara wa kampuni gani kulingana na sababu zakoโœ…

๐Ÿ‘‰Kuonesha umri wa kuku kwenye Picha tunaandika hivi k**a hii imeandikwa " DAY 35 " maana yake kuku huyu ana siku 35, k**a hatujaweka umri kwenye picha usitusingizie ๐Ÿ˜Š

Sasa Angalia hii video ya Tanbro wa siku 43 kwenye comment section kwasababu wakati tunawafuga Hawa Tanbro wafugaji walikuwa wanabisha kuhusu umri wao k**a ambavyo Leo baadhi wanakataa kuwa Hawa kwenye picha sio kuku wa siku 35 ๐Ÿ˜ƒ

Tuna formula tatu katika mpangilio ufuatao na kila formula ina CFP yake 1.Chakula Cha vifaranga/starter mash hii formula...
19/04/2026

Tuna formula tatu katika mpangilio ufuatao na kila formula ina CFP yake

1.Chakula Cha vifaranga/starter mash hii formula inatumika kuchanganya chakula cha vifaranga kuanzia siku 1 mpaka siku 25

Mahindi paraza kilo 52
Soya kavu kilo 32
Mashudu ya alizeti kilo 9
Mafuta/oil kilo 2
CFP ya vifaranga kilo 5

Jumla kilo 100

๐Œ๐€๐…๐”๐“๐€ ๐˜๐€๐๐€๐“๐”๐Œ๐ˆ๐Š๐€ ๐Š๐–๐„๐๐˜๐„ ๐‚๐‡๐€๐Š๐”๐‹๐€ ๐‚๐‡๐€ ๐•๐ˆ๐…๐€๐‘๐€๐๐†๐€ ๐“๐”

2.Formula ya kuku wanaokua hii inatumika kuanzia siku 25 mpaka unapowauza au wanapoanza kutaga/ukiona yai la kwanza

Mahindi paraza kilo 45
Mashudu ya alizeti kilo 15
Pumba za mahindi kilo 25
Soya kavu kilo 10
CFP ya kuku wanaokua kilo 5

Jumla kilo 100

Hapa kwenye kuku wanaokua Kuna formula nyingine yenye pumba nyingi

3.Formula kwa ajili ya kuku chotara wanaotaga

Mahindi paraza kilo 45
Pumba za mahindi kilo 16
Mashudu ya alizeti kilo 14
Chokaa kilo 10
Soya kavu kilo 10
CFP ya kuku wanaotaga kilo 5

Jumla kilo 100

Hapa pia Kuna formula nyingine yenye pumba nyingi

Kuanzia siku 25 na kuendelea unaweza kutumia uduvi au dagaa k**a mbadala wa soya kavu kwa vifaranga tumia soya kavu pekee

Bei za CFP hapa Dodoma

1.Starter/vifaranga [kuanzia siku 1 na kuendelea]

Kilo 5 ni 17,000
Kilo 25 ni 75,000

2.Grower/kuku wanaokua [Kuanzia siku 25 na kuendelea]

Kilo 5 ni 14,000
Kilo 25 ni 60,000

3.Kuku wanaotaga[Baada ya kuona yai]
Kilo 5 ni 14,000
Kilo 25 ni 60,000

๐Š๐ข๐ฅ๐จ ๐Ÿ“ ๐ข๐ง๐š๐ญ๐จ๐ฌ๐ก๐š ๐ค๐ฎ๐œ๐ก๐š๐ง๐ ๐š๐ง๐ฒ๐š ๐œ๐ก๐š๐ค๐ฎ๐ฅ๐š ๐ค๐ข๐ฅ๐จ ๐Ÿ๐ŸŽ๐ŸŽ

๐Š๐ข๐ฅ๐จ ๐Ÿ๐Ÿ“ ๐ข๐ง๐š๐ญ๐จ๐ฌ๐ก๐š ๐ค๐ฎ๐œ๐ก๐š๐ง๐ ๐š๐ง๐ฒ๐š ๐œ๐ก๐š๐ค๐ฎ๐ฅ๐š ๐ค๐ข๐ฅ๐จ ๐Ÿ“๐ŸŽ๐ŸŽ

Mawasiliano 0752 912132 au 0718 192 378 kuagiza CFP

Tuwekane sawa kuhusu soya Soya imegawanyika sehemu kuu mbili : soya kavu/soyabean meal na soya mafuta/full fat soyaSoya ...
19/04/2026

Tuwekane sawa kuhusu soya

Soya imegawanyika sehemu kuu mbili : soya kavu/soyabean meal na soya mafuta/full fat soya

Soya ya mafuta hii inakuwa na protini 36% na mafuta 18% uwepo wa mafuta mengi inaifanya iwe na energy nyingi kuliko soya kavu

Soya kavu inakuwa na protini 45% au zaidi na mafuta 0.5-2% kwahiyo soya kavu ina protini nyingi na energy yake Iko chini kuliko soya mafuta

Hapa tunatumia soya kavu kwasababu tunalenga kupata protini ya kutosha kwa ajili ya ukuaji wa kuku

๐’๐จ๐ฒ๐š ๐ค๐ข๐ฅ๐จ ๐Ÿ“๐ŸŽ ๐ง๐ข ๐Ÿ๐ŸŽ๐ŸŽ,๐ŸŽ๐ŸŽ๐ŸŽ, ๐ค๐ข๐ฅ๐จ ๐Ÿ ๐ง๐ข ๐Ÿ๐ŸŽ๐ŸŽ๐ŸŽ ๐ฐ๐š๐ฌ๐ข๐ฅ๐ข๐š๐ง๐š ๐ง๐š๐ฌ๐ข ๐ค๐ฐ๐š ๐ง๐š๐ฆ๐›๐š ๐ก๐ข๐ข ๐ŸŽ๐Ÿ•๐Ÿ“๐Ÿ๐Ÿ—๐Ÿ๐Ÿ๐Ÿ๐Ÿ‘๐Ÿ ๐š๐ฎ ๐ŸŽ๐Ÿ•๐Ÿ๐Ÿ– ๐Ÿ๐Ÿ—๐Ÿ ๐Ÿ‘๐Ÿ•๐Ÿ–

Kuna classifications nyingi za soya ila hii ya kuangalia kiwango cha protini ndio mgawanyo sahihi kwa mfugaji

Mgawanyo/classification nyingine ni zile zinazoangalia mchakato wa uandaji mfano

De oiled cake [Soya Doc] k**a huu mfuko kwenye picha na hii ndio inapatikana masoko mengi inakuwa na protini 42-46%

Dehulled soybean meal hii inakuwa na protini 47-48% mchakato wake unahusisha kukoboa soya kabla ya kui process

Disclaimer

Haya sio maelekezo ya kitaalamu kuhusu namna ya kuandaa soya tunashauri ununue soya iliyoandaliwa.

Kuagiza CFP au soya kavu tupigie 0752912132 au fika ofisini kwetu

Moshi Agrovet tunapatikana Dodoma, Majengo Sokoni pembeni ya CRDB MAJENGO

Mpaka kufikia hapo kuku mmoja ametumia gharama ya TZS 5126.58 , ndio kuanzia kununua kifaranga, chakula, chanjo,dawa,kuw...
23/03/2026

Mpaka kufikia hapo kuku mmoja ametumia gharama ya TZS 5126.58 , ndio kuanzia kununua kifaranga, chakula, chanjo,dawa,kuwapa joto na gharama nyinginezo [magazeti, pumba za mpunga etc...]

Gharama yote 1,537,976 [ Gharama hii haihusishi kujenga Banda, kununua vyombo vya maji na chakula na vifaa vya joto] Miundombinu ya kiufugaji ipo [Banda na vifaa vyake]

Kuku mmoja ametumia 5126.58

Tumewachanganyia chakula kilo 300 kuanzia siku 1 kwa kutumia CFP ya vifaranga, walipomaliza kilo 300 za starter tukakutumia CFP ya kuku wanaokua kuchanganya chakula kilo 400 ambacho wanamalizia leo siku ya 31

Wastani wa uzito wao ni kilo 1, maana yake wapo wenye kilo 1 mpaka 1.25 na wadogo gram 850-900

Umri wao siku 31 leo...

Jumla ya gharama zote 1,537,976
Idadi ya kuku:300

Kuna CFP ya vifaranga, kuku wanaokua na Wanaotaga

Bei za CFP hapa Dodoma

1.Starter/vifaranga [kuanzia siku 1 na kuendelea]

Kilo 5 ni 17,000
Kilo 25 ni 75,000

2.Grower/kuku wanaokua [Kuanzia siku 25 na kuendelea]

Kilo 5 ni 14,000
Kilo 25 ni 60,000

3.Kuku wanaotaga[Baada ya kuona yai]
Kilo 5 ni 14,000
Kilo 25 ni 60,000

๐Š๐ข๐ฅ๐จ ๐Ÿ“ ๐ข๐ง๐š๐ญ๐จ๐ฌ๐ก๐š ๐ค๐ฎ๐œ๐ก๐š๐ง๐ ๐š๐ง๐ฒ๐š ๐œ๐ก๐š๐ค๐ฎ๐ฅ๐š ๐ค๐ข๐ฅ๐จ ๐Ÿ๐ŸŽ๐ŸŽ

๐Š๐ข๐ฅ๐จ ๐Ÿ๐Ÿ“ ๐ข๐ง๐š๐ญ๐จ๐ฌ๐ก๐š ๐ค๐ฎ๐œ๐ก๐š๐ง๐ ๐š๐ง๐ฒ๐š ๐œ๐ก๐š๐ค๐ฎ๐ฅ๐š ๐ค๐ข๐ฅ๐จ ๐Ÿ“๐ŸŽ๐ŸŽ

Mawasiliano 0752912132

Moshi Agrovet tunapatikana Dodoma Majengo Sokoni

๐—ข๐—ธ๐—ผ๐—ฎ ๐˜‡๐—ฎ๐—ถ๐—ฑ๐—ถ ๐˜†๐—ฎ ๐Ÿฎ๐Ÿฌ,๐Ÿฌ๐Ÿฌ๐Ÿฌ ๐—ธ๐˜„๐—ฎ ๐—ธ๐˜‚๐—ฐ๐—ต๐—ฎ๐—ป๐—ด๐—ฎ๐—ป๐˜†๐—ฎ ๐—ฐ๐—ต๐—ฎ๐—ธ๐˜‚๐—น๐—ฎ ๐—ฐ๐—ต๐—ฎ ๐˜ƒ๐—ถ๐—ณ๐—ฎ๐—ฟ๐—ฎ๐—ป๐—ด๐—ฎKwa kawaida vifaranga wa chotara tulikuwa tunaanza kuwalisha c...
12/02/2026

๐—ข๐—ธ๐—ผ๐—ฎ ๐˜‡๐—ฎ๐—ถ๐—ฑ๐—ถ ๐˜†๐—ฎ ๐Ÿฎ๐Ÿฌ,๐Ÿฌ๐Ÿฌ๐Ÿฌ ๐—ธ๐˜„๐—ฎ ๐—ธ๐˜‚๐—ฐ๐—ต๐—ฎ๐—ป๐—ด๐—ฎ๐—ป๐˜†๐—ฎ ๐—ฐ๐—ต๐—ฎ๐—ธ๐˜‚๐—น๐—ฎ ๐—ฐ๐—ต๐—ฎ ๐˜ƒ๐—ถ๐—ณ๐—ฎ๐—ฟ๐—ฎ๐—ป๐—ด๐—ฎ

Kwa kawaida vifaranga wa chotara tulikuwa tunaanza kuwalisha chakula cha dukani kuanzia siku 1 mpaka 25 baada ya hapo tunaanza kuwachanganyia chakula kwa kutumia CFP ya kuku wanaokua

Sasa wafugaji wengi ambao wanatumia CFP wamekuwa wakihitaji CFP ya vifaranga ili wapunguze gharama

Ndio wapunguze gharama na hapa nitakupa ushuhuda huu

Tuliokoa 33,000 kwa kuchanganya chakula cha vifaranga na ukuaji wao uko vizuri sana, tulitumia hii formula ๐Ÿ‘‡

Mahindi paraza kilo 52
Soya kavu kilo 32
Mashudu ya alizeti kilo 9
Mafuta/oil kilo 2
CFP ya vifaranga kilo 5

๐‰๐ฎ๐ฆ๐ฅ๐š ๐ค๐ข๐ฅ๐จ ๐Ÿ๐ŸŽ๐ŸŽ ๐ ๐ก๐š๐ซ๐š๐ฆ๐š ๐ฒ๐š๐ค๐ž ๐ญ๐ฎ๐ฅ๐ข๐ญ๐ฎ๐ฆ๐ข๐š ๐Ÿ๐Ÿ’๐Ÿ”,๐ŸŽ๐ŸŽ๐ŸŽ, ๐ค๐ข๐ฅ๐จ ๐Ÿ๐ŸŽ๐ŸŽ ๐ง๐ข ๐ฌ๐š๐ฐ๐š ๐ง๐š ๐ฆ๐ข๐Ÿ๐ฎ๐ค๐จ ๐Ÿ ๐ฒ๐š ๐ค๐ข๐ฅ๐จ ๐Ÿ“๐ŸŽ

Maana yake mfuko mmoja tumeupata kwa 73,000 wakati tungenunua tungetumia 89,500 kwa mfuko mmoja wa starter

Kwahiyo utaona tumesevu 16,500 kwa kila mfuko mmoja kwa kuchanganya chakula cha dukani vifaranga

Fanya hesabu ya gharama ya hii formula uone unaokoa sh ngapi hapo ulipo?

K**a kikwazo kwako ni bei ya soya kavu unaweza kuagiza tukakutumia mf Kuna mfugaji akaniambia alipo soya ni 2700 kilo moja wakati hapa Dodoma soya kavu kilo 50 ni 95,000 sawa na kilo moja sh 1900

Unaweza kuagiza soya kavu ukatumiwa, na huyu mfugaji hakuwa mbali sana ni wilaya fulani hapo Morogoro!

Mwingine yupo Arusha aliniambia soya kavu kilo moja ni 2500

Niliwahi kupigiwa simu na mama mmoja yupo Mbagala akasema ananunua soya kilo moja sh 3000!

Nataka kusemaje?

๐Š๐ฎ๐ญ๐ž๐ง๐ ๐ž๐ง๐ž๐ณ๐š ๐œ๐ก๐š๐ค๐ฎ๐ฅ๐š ๐๐จ๐ซ๐š ๐ค๐ฐ๐š ๐ ๐ก๐š๐ซ๐š๐ฆ๐š ๐ง๐š๐Ÿ๐ฎ๐ฎ ๐ข๐ง๐š๐ก๐ข๐ญ๐š๐ฃ๐ข ๐ฆ๐š๐š๐ง๐๐š๐ฅ๐ข๐ณ๐ข ๐ฒ๐š ๐ค๐ฎ๐ค๐ฎ๐ฌ๐š๐ง๐ฒ๐š ๐ฆ๐š๐ก๐ข๐ญ๐š๐ฃ๐ข ๐ฒ๐จ๐ญ๐ž ๐ฒ๐š๐ง๐š๐ฒ๐จ๐ญ๐š๐ค๐ข๐ฐ๐š ๐ค๐š๐›๐ฅ๐š ๐ฒ๐š ๐ค๐ฎ๐œ๐ก๐š๐ง๐ ๐š๐ง๐ฒ๐š ๐œ๐ก๐š๐ค๐ฎ๐ฅ๐š ๐ก๐š๐ฌ๐š ๐˜๐š๐ฅ๐ž ๐š๐ฆ๐›๐š๐ฒ๐จ ๐ง๐ข ๐š๐๐ข๐ฆ๐ฎ ๐ง๐๐ข๐จ ๐ฒ๐š๐ง๐ฎ๐ง๐ฎ๐ฅ๐ข๐ฐ๐ž ๐ค๐ฐ๐š๐ง๐ณ๐š.

Chakula kinapanda kila siku, changanya chakula uokoe zaidi ya 20,000 huku ukipata ukuaji mzuri wa vifaranga wako k**a ha...
11/02/2026

Chakula kinapanda kila siku, changanya chakula uokoe zaidi ya 20,000 huku ukipata ukuaji mzuri wa vifaranga wako k**a hawa unaowaona kwenye picha Wana siku 21

Ni rahisi Wala sio kazi na huhitaji vitu vingi kuchanganya chakula cha vifaranga, unahitaji hivi vitu vichache Nikupe mfano wa chakula kilo 100 utaweka

Mahindi paraza kilo 52
Soya kavu kilo 32
Mashudu ya alizeti kilo 9
Mafuta/oil kilo 2
CFP ya vifaranga kilo 5

Jumla kilo 100, kwa gharama za hapa Dodoma utatumia 146,000 kupata starter kilo 100 sawa na mifuko 2 ya chakula ambacho ukinunua sio chini ya 179,000

Mafuta unaweza kutumia ya alizeti, korie, safi etc

Bei za CFP ya vifaranga kwa hapa Dodoma
Kilo 5 ni 17,000 inatosha kuchanganya chakula kilo 100
Kilo 25 ni 75,000 inatosha kuchanganya chakula kilo 500

Tupigie 0752912132

22/01/2026

Leo vifaranga wetu wamefikisha siku ya 21 ๐Ÿ”ฅ ๐Ÿ”ฅ ๐Ÿ”ฅ

Gharama ya chakula kilo 100 tulitumia : ๐Ÿ๐Ÿ’๐Ÿ”,๐ŸŽ๐ŸŽ๐ŸŽ

Formula tunayotumia ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

๐Ÿญ.๐— ๐—ฎ๐—ต๐—ถ๐—ป๐—ฑ๐—ถ ๐—ฝ๐—ฎ๐—ฟ๐—ฎ๐˜‡๐—ฎ ๐—ธ๐—ถ๐—น๐—ผ ๐Ÿฑ๐Ÿฎ
๐Ÿฎ.๐—ฆ๐—ผ๐˜†๐—ฎ ๐—ธ๐—ฎ๐˜ƒ๐˜‚ ๐—ธ๐—ถ๐—น๐—ผ ๐Ÿฏ๐Ÿฎ
๐Ÿฏ.๐— ๐—ฎ๐˜€๐—ต๐˜‚๐—ฑ๐˜‚ ๐˜†๐—ฎ ๐—ฎ๐—น๐—ถ๐˜‡๐—ฒ๐˜๐—ถ ๐—ธ๐—ถ๐—น๐—ผ ๐Ÿต
๐Ÿฐ.๐—ข๐—ถ๐—น/๐— ๐—ฎ๐—ณ๐˜‚๐˜๐—ฎ ๐—ธ๐—ถ๐—น๐—ผ ๐Ÿฎ
๐Ÿฑ.๐—–๐—™๐—ฃ ๐˜†๐—ฎ ๐˜ƒ๐—ถ๐—ณ๐—ฎ๐—ฟ๐—ฎ๐—ป๐—ด๐—ฎ ๐—ธ๐—ถ๐—น๐—ผ ๐Ÿฑ

๐—๐˜‚๐—บ๐—น๐—ฎ ๐—ธ๐—ถ๐—น๐—ผ ๐Ÿญ๐Ÿฌ๐Ÿฌ

1.Ulaji wa chakula / Feed intake - Uko vizuri...mpaka leo siku 21 wameshakula kilo 94 sawa gram 959.2 kwa kila kifaranga

2.Uzito / Body weight gain - wanaongezeka vizuri, daily gain ni above average -

Wastani wao ni gram 720
Uzito wa juu gram 840

Kwa uzoefu wetu vifaranga wa chotara siku 21 wakiwa na uzito wa juu ni gram 540 tulipokuwa tunatumia chakula cha dukani

3.Matatizo ya miguu / Leg problems-Hakuna

4.Choo Cha kuku / faecal dropping- Normal/Kawaida - angalia maranda utaona choo choo kikoje

5.Cannibalism/ Kudonoana -Hakuna

๐Š๐š๐ฆ๐š ๐ฎ๐ฅ๐ข๐ฉ๐จ ๐ฌ๐จ๐ฒ๐š ๐ก๐š๐ข๐ฉ๐š๐ญ๐ข๐ค๐š๐ง๐ข ๐ค๐ข๐ซ๐š๐ก๐ข๐ฌ๐ข, ๐ฎ๐ฌ๐ข๐จ๐ ๐จ๐ฉ๐ž ๐ญ๐ฎ๐ง๐š๐ฅ๐ข๐Ÿ๐š๐ง๐ฒ๐ข๐š ๐ค๐š๐ณ๐ข ๐ข๐ฅ๐ข ๐ญ๐ฎ๐ก๐š๐ค๐ข๐ค๐ข๐ฌ๐ก๐ž ๐ฎ๐ง๐š๐ฉ๐จ๐œ๐ก๐š๐ง๐ ๐š๐ง๐ฒ๐š ๐œ๐ก๐š๐ค๐ฎ๐ฅ๐š ๐ฎ๐ง๐š๐ฉ๐ฎ๐ง๐ ๐ฎ๐ณ๐š ๐ ๐ก๐š๐ซ๐š๐ฆ๐š ๐›๐š๐๐š๐ฅ๐š ๐ฒ๐š ๐ค๐ฎ๐ก๐š๐ง๐ ๐š๐ข๐ค๐š ๐›๐ฎ๐ซ๐ž

16/01/2026

Leo vifaranga wetu wamefikisha siku ya 14 ๐Ÿ”ฅ ๐Ÿ”ฅ ๐Ÿ”ฅ

Gharama ya chakula kilo 100 tulitumia : ๐Ÿ๐Ÿ’๐Ÿ”,๐ŸŽ๐ŸŽ๐ŸŽ

Formula tunayotumia ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ

๐Ÿญ.๐— ๐—ฎ๐—ต๐—ถ๐—ป๐—ฑ๐—ถ ๐—ฝ๐—ฎ๐—ฟ๐—ฎ๐˜‡๐—ฎ ๐—ธ๐—ถ๐—น๐—ผ ๐Ÿฑ๐Ÿฎ
๐Ÿฎ.๐—ฆ๐—ผ๐˜†๐—ฎ ๐—ธ๐—ฎ๐˜ƒ๐˜‚ ๐—ธ๐—ถ๐—น๐—ผ ๐Ÿฏ๐Ÿฎ
๐Ÿฏ.๐— ๐—ฎ๐˜€๐—ต๐˜‚๐—ฑ๐˜‚ ๐˜†๐—ฎ ๐—ฎ๐—น๐—ถ๐˜‡๐—ฒ๐˜๐—ถ ๐—ธ๐—ถ๐—น๐—ผ ๐Ÿต
๐Ÿฐ.๐—ข๐—ถ๐—น/๐— ๐—ฎ๐—ณ๐˜‚๐˜๐—ฎ ๐—ธ๐—ถ๐—น๐—ผ ๐Ÿฎ
๐Ÿฑ.๐—–๐—™๐—ฃ ๐˜†๐—ฎ ๐˜ƒ๐—ถ๐—ณ๐—ฎ๐—ฟ๐—ฎ๐—ป๐—ด๐—ฎ ๐—ธ๐—ถ๐—น๐—ผ ๐Ÿฑ

๐—๐˜‚๐—บ๐—น๐—ฎ ๐—ธ๐—ถ๐—น๐—ผ ๐Ÿญ๐Ÿฌ๐Ÿฌ

1.Ulaji wa chakula / Feed intake - Uko vizuri...mpaka leo siku 14 wameshakula kilo 47 sawa gram 480 kwa kila kifaranga

2.Uzito / Body weight gain - wanaongezeka vizuri, daily gain ni above average -

Wastani wao ni gram 387.75
Uzito wa juu gram 474

Kwa uzoefu wetu vifaranga wa chotara siku 14 wakiwa na uzito wa juu ni gram 335 tulipokuwa tunatumia chakula cha dukani

3.Matatizo ya miguu / Leg problems-Hakuna

4.Choo Cha kuku / faecal dropping- Normal/Kawaida - angalia maranda utaona choo choo kikoje

5.Cannibalism/ Kudonoana -Hakuna

๐Š๐š๐ฆ๐š ๐ฎ๐ฅ๐ข๐ฉ๐จ ๐ฌ๐จ๐ฒ๐š ๐ก๐š๐ข๐ฉ๐š๐ญ๐ข๐ค๐š๐ง๐ข ๐ค๐ข๐ซ๐š๐ก๐ข๐ฌ๐ข, ๐ฎ๐ฌ๐ข๐จ๐ ๐จ๐ฉ๐ž ๐ญ๐ฎ๐ง๐š๐ฅ๐ข๐Ÿ๐š๐ง๐ฒ๐ข๐š ๐ค๐š๐ณ๐ข ๐‡๐ข๐ฅ๐จ ๐ง๐š๐ฅ๐จ ๐ข๐ฅ๐ข ๐ญ๐ฎ๐ก๐š๐ค๐ข๐ค๐ข๐ฌ๐ก๐ž ๐ฎ๐ง๐š๐ฉ๐จ๐œ๐ก๐š๐ง๐ ๐š๐ง๐ฒ๐š ๐œ๐ก๐š๐ค๐ฎ๐ฅ๐š ๐ฎ๐ง๐š๐ฉ๐ฎ๐ง๐ ๐ฎ๐ณ๐š ๐ ๐ก๐š๐ซ๐š๐ฆ๐š ๐›๐š๐๐š๐ฅ๐š ๐ฒ๐š ๐ค๐ฎ๐ก๐š๐ง๐ ๐š๐ข๐ค๐š ๐›๐ฎ๐ซ๐ž

Tupo wazi Jumatatu mpaka Jumamosi karibu tukuhudumie tunauza dawa, chanjo, vitamin na vifaa vya ufugaji wa kuku Sasa tum...
26/09/2025

Tupo wazi Jumatatu mpaka Jumamosi karibu tukuhudumie tunauza dawa, chanjo, vitamin na vifaa vya ufugaji wa kuku

Sasa tumekuletea suluhisho la kuandaa chakula cha kuku chotara kwa kutumia CFP ๐Ÿ”ฅ

Tunapatikana Dodoma Majengo Sokoni karibu na CRDB MAJENGO tupigie 0659632332

Address

Weyula
Dodoma
41201

Opening Hours

Monday 07:30 - 19:00
Tuesday 07:30 - 19:00
Wednesday 07:30 - 19:00
Thursday 07:30 - 19:00
Friday 07:30 - 19:00
Saturday 09:30 - 19:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Layers Pro posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Layers Pro:

Share

Category