01/01/2026
HERI YA MWAKA MPYA 2026 WATANZANIA WENZANGU.
KWA MWAKA 2026 NITAJIKITA KWENYE AGENDA ZIFUATAZO:
1. KUANZISHA HALMASHAURI ZA MIKOA
Utaratibu utakuwa kila halmashauri watachagua mjumbe mmoja katika uchaguzi mkuu ambaye ataungana na Mwenyeviti/Mameya wa halmashauri, Makamu wao pamoja na wabunge wa mkoa husika kuunda Baraza la Wawakilishi la Mkoa. Kiongozi wao atachaguliwa miongozi mwa wajumbe wanaotoka chama chenye wajumbe wengi na ataitwa Gavana wa Mkoa na atasaidiwa na naibu gavana wa mkoa. Mtendaji Mkuu ataitwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mkoa (Regional Exercutive Director). Wawakilishi wa kila halmashauri watalipwa na halmashauri zao, huku mkoani ni posho tu za vikao. Wabunge wataendelea kulipwa na Bunge na Mameya/Wenyeviti/ Makamu/Naibu watalipwa na halmashauri zao na hawataruhusiwa kuwa magavana, naibu gavana wala mwenyeviti wa k**ati bali watabaki kuwa wajumbe tu. Nafasi ya Mkuu wa Mkoa na RAS wake itabaki k**a ilivyo kwa Mkuu wa Wilaya na DAS kwa sasa kushugulikia masuala mahsusi. Hatua hii ni muhimu kusogeza serikali na wananchi. Kwa mfumo wa sasa serikali ipo mbali sana kutoka kwa wananchi na wanakutana kwenye ziara badala ya kuishi nao, kuwa nao, kushinda nao. Changamoto nyingi zinapaswa kumalizwa na mamlaka za mkoa badala ya kusubiri viongozi wa kitaifa pekee.
2. KUANZISHA MAMLAKA HURU (K**A BOT) YA KUSIMAMIA MASHIRIKA NA TAASISI ZA UMMA
Mamlaka hii itakuwa huru kuanzisha, kuuza, kufuta na kuunganisha mashirika yote na Taasisi ambazo zinafanya biashara. Zitabaki zile tu mamlaka, wakala, tume, bodi, na zingine k**a hizo ambazo lengo mama ni kusimamia sekta. Mfano sekta ya maliasili, TFS, Tawa na Bodi ya Utalii ni wasimamizi. Ila Tanapa na Ngorongoro ni wafanyabiashara hivyo watahamishiwa kwenye mamlaka ya usimamizi wa mashirika. Pale uchukuzi, TPA, TRC, ATCL, TRC, TAA, wote ni wafanyabiashara; Latra, Tasac na TCAA ndio wasimamizi. Wasimamizi/mamlaka/ wakala watabaki chini ya Msajili wa Hazina. Watumishi wa mashirika wote hawatakuwa watumishi wa umma tena na watafanya kazi kwa ajira za mkataba. Watumishi wa Umma wanaofanyakazi kwenye mashirika mkataba ukiisha/ukivunjwa wanarudishwa Utumishi ila ambao sio watumishi itakuwa ndio mwisho wa ajira zao.
3.KUANZISHA MFUKO WA UWEKEZAJI WA TAIFA
Nchi zote zenye rasilimali zina mifuko hii ambayo inakusanya faida toka BOT, mashirika mbalimbali, mirabaha ya madini, gesi, misitu na rasilimali zingine na kuziwekeza duniani. Pia hutoa mitaji kwa makampuni binafsi na yale yanayomilikiwa na serikali. Huwa sehemu nzuri kwa serikali kukopa lakini huwezesha miradi mikubwa k**a bandari ya kimataifa ya Bagamoyo, Tanga na Mtwara au miradi k**a LNG Plant nk. Kumbuka rasilimali huisha au hupoteza thamani (k**a ilivyo kwa mafuta/makaa ya mawe) lakini vizazi vinaendelea kuja. Lazima tuendelee kuwekeza ili rasilimali hizo zifaidishe vizazi vijazo pia kuwezesha Tanzania kushiriki uchumi wa Dunia.
4. KUUNGANISHA MIKOA YOTE KWA RELI YA SGR, HALMASHAURI ZOTE PANDE ZOTE KWA LAMI NA KATA ZOTE KWA LAMI/ZEGE AU CHANGARAWE.
Binafsi sio muumini saana wa ujenzi wa reli ya mkoloni. Reli inayowaza zaidi kuhudumia wengine kuliko sisi. Mpango wa reli uboreshwe. Reli ya kati ya SGR inaendelea kujengwa vipi kuhusu reli ya Tanga-Arusha-Musoma- Mwanza? Vipi kuhusu Reli ya Mtwara-Songea- Makambako/ Mbambabay? Vipi kuhusu Reli ya Tanga-Dar-Mtwara? Vipi kuhusu reli ya Arusha-Dodoma-Iringa- Mbeya? na vipi kuhusu reli ya Tabora-Mpanda-Sumbawanga-Mbeya? Mfumo huu wa reli unawezesha Mikoa yote kuunganishwa kwa reli.
Pia katika kila halmashauri ya Wilaya/Mji/ Jiji lazima iunganishwe kwa lami kwa Pande zote kutoka halmashauri nyingine au mkoa mwingine. Na mwisho tuunganishe kata zote kwa changarawe kwa kila upande. Afadhali zile trioni 6 zilizopangwa kupeleka umeme kila Kitongoji zijenge kwanza barabara hizi muhimu. Hakuna haja ya kuwa na umeme kwenye kitongozi wakati barabara ya kwenda wilayani/katani tu haipitiki kwa nusu mwkaka. Kupanga ni kuchagua.
5.FURSA KWA VIJANA
Mwaka huu nitatumia muda wangu kueleza fursa kwa vijana zilizopo Tanzania, nchi jirani na duniani. Fursa katika sekta za kilimo, Madini, Tekinolojia, ajira, masomo, uwekezaji, usafirishaji na zinginezo. Lengo ni kuwafungulia dunia vijana wenzangu na wapambanaji wenzangu.
Ni Mimi MTZ7 (Mpwa wa Tz)