Public Figure

Public Figure To share positive thinking with people all around the worldwide. For creditable Health and Safety Updates in Tanzania and Worldwide

22/10/2021

K**a Vijana ambao tunategemewa na serikali yetu katika kusukuma gurudumu la maendeleo, tunaamini kwamba hakuna maendeleo bila yakua na afya bora. Hivyo basi kwa umoja wetu, nguvu zetu na maarifa yetu tumejitolea kushirikiana na na kuhakikisha taarifa sahihi za chanjo ya uviko-19 inawafikia watanzania kwa namna tuliyoibuni sisi na tunaamini tutaungwa mkono katika hili.

The 20th Joint Annual Health Sector Technical Review Meeting.Tukutane Dodoma Kwenye Mkutano wa Wataalam wa kutathmini ut...
07/10/2019

The 20th Joint Annual Health Sector Technical Review Meeting.

Tukutane Dodoma Kwenye Mkutano wa Wataalam wa kutathmini utekelezaji wa Mkakati wa Nne wa Sekta ya Afya “the 20th Joint Annual Health Sector Technical Review Meeting”, Ukumbi wa PSSSF/LAPF.
Kwa maelezo zaidi piga simu namba 0719807219 au 0764976069.

07/10/2019

"Kauli ya serikali juu ya ugonjwa wa ebola.
"Nchi yetu ni salama na hatuna ugonjwa wa Ebola " waziri wa Afya Ummy Mwalimu

"Kabla Rais kuingia madarakani Mkoa wa Songwe ulikua unapokea milioni 450 tu kwa ajili ya dawa kupitia MSDTZ, Rais Maguf...
06/10/2019

"Kabla Rais kuingia madarakani Mkoa wa Songwe ulikua unapokea milioni 450 tu kwa ajili ya dawa kupitia MSDTZ, Rais Magufuli aliahidi kutatua changamoto za Dawa na leo mkoa wa Songwe unapokea Bilioni 1.9 kwa ajili ya dawa kutoka MSDTZ" waziri wa afya Ummy Mwalimu

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania KASSIM MAJALIWA amewataka waajiri kutoa Nafasi kwa maafisa lishe kutoa el...
04/10/2019

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania KASSIM MAJALIWA amewataka waajiri kutoa Nafasi kwa maafisa lishe kutoa elimu kwa wafanyakazi katika maeneo yao ya kazi kwani kutokana na kuwa na vipato vyao wamekuwa wakila hovyo bila kuzingatia lishe bora na kusababisha kuwa na Viribatumbo.

Waziri mkuu MAJALIWA anatoa agizo hilo wakati akifungua mkutano wa mwaka wa kufanya Tathmini ya lishe jijini Dodoma ambapo amesema eneo hilo ni eneo lenye tatizo kubwa zaidi katika suala la lishe huku akiahidi kuanzia 2020 mbio za mwenge zitakuwa zikibeba ujumbe wa lishe.

Aidha mkutano huo pia ulihudhuriwa na Waziri Mkuu Mstaafu MIZENGO PINDA amevishauri vyama vya siasa kuweka suala la lishe kwenye ilani zao za uchaguzi pamoja na kuweka ujumbe kwenye mbio za mwenge ili liweze kuwa la kitaifa na kushirikisha wananchi wote hadi vijijini.
Akizungumza Jijini Dodoma Waziri mkuu mstaafu amesema kuwa suala la lishe linatakiwa kutiliwa mkazo zaidi kwa kupitia njia mbalimbali kwani asilimia 75 ya Watanzania wanaishi vijijini na bado wanaendeleza mila na desturi zilizopitwa na wakati.

Waziri mkuu mstaafu Pinda amesema bado serikali inayo kazi kubwa ya kufanya kuhakikisha inatokomeza tatizo la udumavu kwa kuwaelemisha wananchi wanaoishi vijijini kuondokana na mila potofu zinazozuia wanawake na watoto kula vyakula bora. @ Dodoma, Tanzania

KILIMANJARO YAZINDUA ATM YA KWANZA YA MAZIWA-Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira amezindua ATM ya kwanza ya Maziwa...
04/10/2019

KILIMANJARO YAZINDUA ATM YA KWANZA YA MAZIWA
-
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira amezindua ATM ya kwanza ya Maziwa Nchini katika mji wa Moshi yenye uwezo wa kutoa maziwa kulingana na kiwango chako cha fedha
-
Unaweza kupata maziwa kuanzia kwa Tsh. 50, 100, 400, 600, 1000, 2000, na kuendelea
-
Mradi huu umefadhiliwa na Umoja wa Ulaya na Kusimamiwa na SNV pamoja na Match Maker Associates ambapo wameweza kujenga ATM 3 za kuuza Maziwa
-
ATM zingine zipo Wilaya ya Hai na nyingine ipo Mjini Arusha. Sambamba na hili, RC amezindua Jukwaa la Ubunifu la Maziwa Mkoani humo na amekubali kuwa mlezi wa Jukwaa hilo.
Source•
Credits•

KENYA: WATU 13 WAFARIKI NA 35 KUJERUHIWA KATIKA AJALI‬-Ajali imetokea usiku wa kuamkia leo Oktoba 04 katika barabara ya ...
04/10/2019

KENYA: WATU 13 WAFARIKI NA 35 KUJERUHIWA KATIKA AJALI‬
-
Ajali imetokea usiku wa kuamkia leo Oktoba 04 katika barabara ya Kisumu-Kericho karibu na eneo la Awasi‬ na chanzo chake bado hakijajulikana
-
Basi la abiria la Eldoret Express kutoka Kisumu limegongana uso kwa uso na Lori‬ lililokuwa likielekea Kisumu
-
Majeruhi wamepelekwa katika hospitali ya Rufaa na Ukufunzi ya Jaramogi Oginga Odinga (JOOTRH), Hospitali ya Misheni ya Awasi na Hospitali ya Hope huku waliofariki wakihifadhiwa katika hospitali ya Ahero.
Source•
Credits•

Leo muheshimiwa waziri wa Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,wazee na watoto.,Ummy Mwalimu akitolea ufafanuzi wa ripoti mbal...
03/10/2019

Leo muheshimiwa waziri wa Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,wazee na watoto.,Ummy Mwalimu akitolea ufafanuzi wa ripoti mbali mbali juu ya magonjwa yanayoambukiza, usafi wa mazingira na kampeni ya nyumba ni choo!
Aidha waziri wa Afya amewasisitiza watanzania kua watulivu na kutokua na taharuki juu ya taarifa mbali mbali zinazoendelea kwenye mitandao juu ya ugonjwa wa ebola nchini.
&unsata_taifa.

wizara_afyatzNa WAMJW- DODOMA SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, imezifungia jumla ya maabara 13, ambazo ni sawa na asilim...
03/10/2019

wizara_afyatz
Na WAMJW- DODOMA
SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, imezifungia jumla ya maabara 13, ambazo ni sawa na asilimia 21% kati ya Maabara 61 zilizokaguliwa, huku ikitoa onyo kali kwa Maabara 48 kutokana na baadhi ya Maabara hizo kutokidhi viwango vya kutoa huduma za upimaji.

Hayo yamesemwa na Msajili wa Bodi ya Maabara Binafsi kutoka Wizara ya Afya Bw. Dominic John Fwiling'afu wakati wa ziara ya ukaguzi wa hali ya utoaji huduma za upimaji katika maabara zilizopo Jiji la Dodoma.

Amesema kuwa Bodi ya Maabara Binafsi katika kutekeleza majukumu yake, inaendeleza mpango wake wa kukagua Maabara Binafsi zote nchini ili kuhakikisha zinatoa huduma kulingana na miongozo ili kutoa huduma bora kwa Wananchi.
Aliendelea kusema kuwa zoezi hilo limeanza Jijini Dodoma, huku lengo likiwa kukagua jumla ya Maabara 106 ili kujiridhisha utoaji huduma sahihi kwa wananchi, ikiwemo kukagua k**a Wataalamu waliopo wanakidhi vigezo kwa mujibu wa Sheria.

Pia, Bw. Dominic Fwiling'afu amesema kuwa licha ya kukagua ili kujiridhisha na ubora wa huduma zinazotolewa na Maabara hizo, Bodi hiyo inajukumu la kuangalia ulipaji wa tozo mbali mbali uliowekwa kwa mujibu wa Sheria na kujiridhisha k**a Maabara hizo zimetimiza masharti wakati wa uanzishwaji wake.

Aidha, Bw. Dominic Fwiling'afu ameongeza kuwa, mbali na kuzifungia baadhi ya Maabara hizo ambazo hazijakidhi vigezo kulingana na Sheria na miongozo, Bodi imeendelea kutoa ushauri kwa wamiliki na Wataalamu wa Maabara ili kutoa huduma bora kwa Wananchi.
@ Dodoma, Tanzania

Address

Dodoma
255653144009

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Public Figure posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Public Figure:

Share