Usindikaji Na Utunzaji Wa Chakula Kupata Bidhaa Bora

Usindikaji Na Utunzaji Wa Chakula Kupata Bidhaa Bora My purpose is just to educate All Tanzanian about Food Processing, handling in order to get the Quality products

22/11/2018

Habari wasindikaji na mnaoendelea kujifunza k**a kuna mtu ana shida yeyote kwenye maswala ya Usindikaji ususani ubora wa malighafi, utunzaji, jinsi ya namna ya utekelezaji wa kanuni bora za Usindikaji na ubora wa bidhaa kwa ujumla karibu nitakusaidia.

Kwa wale mliokuwa mnanifuatilia kuanzia mwanzo wa masomo haya k**a umejifunza kitu karibu ushare na wenzio.

Wale ambao wanapata shinda ya kupata vibali kutoka TFDA na TBS k**a unachangamoto yeyote kuhusu hilo karibu tutakusaidia . Tuijenge inchi yetu kwa kuongeza thamani ya mazao. Niwatakie utendaji mwema 0685295391 Karibu kwa maswali na ushauri

24/10/2018

Baada ya kujifunza kwa kina kanuni bora za uzalishaji/Usindikaji naamini watu wanaelewa na nashauri uzitumie vizuri hizo kanuni wewe k**a msindikaji zitakusaidia. Leo tujifunze kuhusu uhifadhi/ jinsi ya kuhifadhi mafuta ya Alizeti baada ya kukamuliwa .

Kwa kawaida bidhaa yeyote inayotokana na mafuta ya kupikia k**a vile Alizeti ikiharibika/kuoza ni vigumu kugundua kwani huchukua mda mrefu kuonyesha athari ama mtumiaji anaweza asitambue kabisa. Kiuharisia bidhaa yeyote ya chakula iliyosindikwa au kutokusindikwa ina mda wake wa kuishi kwa lugha nyingine inaitwa shelf life. Mojawapo ya faida ya kusindika ni kuongeza uwezo wa bidhaa kukaa mda mrefu / kuishi kwa baadhi ya vyakula ambavyo huharibika kwa mda mfupi baada ya kuvunwa.

Kwa maana hiyo mzalishaji au msindikaji yeyote anapofunga(pack) bidhaa yake ni lazima aonyeshe itakaa kwa mda gani kuanzia siku iliposindikwa(Manufacturing date and expire date). Hii ni kwa ajili ya usalama wa mtumiaji, bidhaa ikikaa zaidi ya mda wake huharibika na kusababisha madhara kwa mtumiaji.

Mafuta ya Alizeti yaliyokamuliwa na kuchujwa yanamuonekano ufuatao.

Rangi yake ni njano iliyokolea sana hii hutofautiana kutokana na uwezo wa chujio za mashine husika. Yana harufu ya mbegu yenyewe.

Mafuta ya Alizeti yaliyokamuliwa na kuchujwa kawaida yanaweza kutumika kwa mda wa miezi 6-12 endapo yatahifadhiwa katika mazingira mazuri. Mafuta haya yasipotunzwa vizuri huweza kuharibika ndani ya wiki moja, na madhara ya mafuta haya kwa mtumiaji ni makubwa ikiwemo ugonjwa wa kansa. Mafuta haya yanatabia ya kuharibika haraka yanapohifadhiwa kwenye joto Kali, mwanga au kuachwa bila kufunikwa. Kitaalamu inaonyesha hewa(oksijeni), mwanga wa jua ni vitu ambavyo hiharibu ubora wa mafuta haya na kuyafanya yakae mda mfupi lakini pia yanaleta athali kubwa kwa mlaji.

Wasindikaji wetu wengi pamoja na wauzaji wana tamaduni za kuuza mafuta kwa kuyaweza juani, na wengine wakimaliza kukamua hawafuniki, ni hatari sana, wasindikaji mnashauriwa kufunika mafuta yenu pundenapomaliza kuchuja, kwa wauzaji pia hakikisheni mafuta hayapati mwanga wa jua k**a unauzia barabarani jitahidi kuweka hata trubai, tujali afya za watumiaji kunusuru nguvu kazi ya taifa LA leo na kesho.

Kuna namna ya kupima mafuta yako kujua k**a yana ubora au yameharibika, tafuta mtaalam wa mambo ya chakula atakusaidia. Karibuni

Kwa ushauri, maswali na mapendekezo 0685295391 Juliana Kitinde whatsup

04/08/2018

Usafi

Habari za saa hizi wasindikaji na wajasiriamali Leo nakumbusha kuhusu usafi kwenye maeneo ya uzalishaji
Usafi n muhimi sana kabla na baada ya uzalishaji ili kupata bidhaa bora hivyo zingatia usafi kwa afya zetu na wateja wetu .
Hata hivyo usafi unaongeza thamani ya tunacho zalisha na kuongeza imani kwa wateja karibu tuwasiliane MTU mwenye maoni au tatizo tuwasiliane.

08/06/2018

Usalama wa chakula kwa afya ya mtumiaji/mlaji.

Tunaendelea na somo letu LA kanuni bora za usindikaji/uzalishaji.

UNUNUZI WA MALIGHAFI.
Ateuliwe mtaalamu maalumu wa kutayarisha orodha ya malighafi na vifungashio kulingana na ubora unaohitajika.

Malighafi zinuniliwe kwa wafanyabiashara au wakulima wanaotambilika ikiwezekana kuwepo na mkataba kati ya mkulima na msindikaji.

Kuwepo na mfumo utakaohakiki ubora na viwango vya malighafi Mara tu malighafi inapofika kiwandani mfano Kipimia unyevu kwa wasindikaji wa nafaka ni mhimu, kifaa cha kupima maji kwa wasindikaji wa maziwa nk.

Malighafi zitakazokuwa zimeharibika zitolewe Mara moja ili kuepuka uharibifu wa malighafi zingine. Ni mhimu sana , wasindikaji wengi wamekuwa wakipata hasara kwa sababu ya kutofahamu kwamba malighafi mbovu zinaweza kuharibu malighafi zingine.

USAFIRISHAJI WA MALIGHAFI.

Unahitaji uangalifu mkubwa wakati wa usafirishaji kuepusha uharibifu wa chakula.

Wazalishaji/wasindikaji wapo wa aina nyingi, kuna wasindikaji/wazalishaji ambao hununua malighafi shambani au sokoni na kusindika kwa kutumia vitendea kazi vyao yaani mashine nk. Kuna wale ambao hununua bidhaa ambazo tayari zimeshasindikwa mfano Mchele, unga, maziwa ya unga nk na kufungasha(kupack) wenyewe, kuna wale wanunuzi na wasambazaji wa malighafi. Makundi haya yanapaswa kuzingatia kwa kina namna ya usafirishaji wa malighafi kwenda kwenye eneo la uzalishaji.

SIFA YA VIFAA VYA KUBEBEA MALIGHAFI.
Vifaa vya kubebea vyakula(magari) yakaguliwe kabla hayajapakia ili kuhakikisha usalama wa vyakula. Hii ni kwa wale wasindikaji wanaonunua mzigo mkubwa. Kwa wale wasindikaji wanaosafirisha mizigo kutumia maroli au mabus ya abiria(gari lisilo rasimi kwa usafirishaji wa chakula) mnatakiwa kuhakikisha vifungashio vya malighafi viko vizuri kwa ajili ya usalama wa chakula.

Pia vifaa vya kubebea vyakula(gari) vitumike kubeba vyakula tuu na si vinginevyo kwa ajili ya usalama wa vyakula . Mfano gari linalosafirisha nyama, samaki , maziwa nk haliruhusiwi kubeba mchanga, mbolea , kemikali nk hii ni kwa ajili ya kulinda afya ya mlaji/ mtumiaji. Vifaa hivyo pia vinapaswa visafishwe pindi vinapomaliza kutumika kuzuia maambukizi ya vimelea na uchafu mwingine.

Malighafi nyingi kwa asilimia kubwa zinahitaji uthibiti joto kipindi cha usafirishaji. Uthibiti joto..ni joto ambalo linafanya malighafi isipoteze ubora wake kuanzia0°C-25°C hii hutegemea na aina ya malighafi. Kwenye kiwango hiki cha joto vimelea Vingi( micro.organisms) ambavyo hatuvioni kwa macho mfana bakteria, fungus, virusi haviwezi kukua kwenye joto dogo na hii inasaidia kusafirisha malighafi yako katika khali ya ubora.

Malighafi mfano nyama, Samaki, maziwa vinapaswa kusafirishwa vikiwa vimeganda katika vyombo vinavyozuia visiyeyuke.

HATUA ZA USINDIKAJI.

1. Kupokea na kukagua(receiving).
Kwa wasindikaji wanaonunua shambani au sokoni hakikisha malighafi imetunzwa vizuri, iliyovunwa kwa wakati baada ya kufikia kiwango cha kukomaa.

Kwa wasindikaji ambao wanalima wenyewe hakikisha uvunaji, ukaushaji, usafirishaji na uhifadhi vifanyike kwa uangalifu kwa kuzingatia ushauri wa kitaalamu.

Kwa hiyo malighafi inapopokelewa kwa ajili ya usindikaji zingatia mambo yafuatayo

1.Hakikisha malighafi imekauka kwa kiwango kinachofaa kwa upande wa nafaka ikiwezekana tumia kifaa maalumu cha kupimia unyevu.

2. Isiwe ya kuharibiwa na wadudu kwa malighafi zote mfano Matunda nk

3.Iwe imekomaa katika kiwango kinachotakiwa.

4.Isiwe na uchafu au mchanganyiko wa mbegu zingine( kwa upande wa nafaka).

5.Isiwe na ukungu mfano mahindi, mihogo, viazi nk

2.UHIFADHI WA MALIGHAFI.(Storage)

Ni mhimu malighafi ihifadhiwe vizuri kwenye ghala au stoo kabla ya kutumika. Kwa upande wa nafaka magunia yenye malighafi yapangwe juu ya chaga(Pallet) au Trubai ili kuzuia unyevu.
Hakikisha ghala/stoo ya kuhifadhia malighafi ni safi, isiwe inavuja na kuruhusu wadudu mfano panya kuingia ndani. Kwa wasindikaji wa nafaka ni mhimu kutenga malighafi kiasi itakayotumika kwa mda usiozidi miezi mitatu kwani mashambulizi ya wadudu huwa ni ya kiwango chini sana na hivyo hushauriwi kutumia viuatilifu(pesticides).

3.Maandalizi(preparation).
Katika hatua hii malighafi zote hutengenezwa kwa kuongezewa thamani ya chakula mfano mbegu za alizeti husagwa na kutoa mafuta, Matunda k**a vile maembe huoshwa, hukatwakatwa na kusagwa kuwa juisi nk.

Hivyo unashauriwa kuanza kutengeneza/kusindik**alighafi uliotangulia kuhifadhi stoo.

4. Ufungashaji na kuweka lebo(Packaging and labeling).
Katika hatua hii bidhaa iliyozalishwa kwenye malighafi husika hufungashwa kwenye vifungashio safi na vilivyokidhi viwango kwa ajili ya bidhaa husika na kubandikwa lebo inayoitambulisha bidhaa hiyo.

Nitoe angalizo katika swala vifungashio...kabla haujaanza kusindika/ kununua bidhaa yako kwa ajili ya kufungasha hakikisha umefanya tafiti juu ya vifungashio vya bidhaa yako ni mhimu sana..k**a unapata shida jitahidi hata kuonana na wataalamu wanaofahamu vifungashio bora. Kila bidhaa ina vifungashio vyake kutokana na sheria ya chakula ili kuepuka hasara ya kukataliwa kwa vifungashio vyako na mamlaka husika(TFDA/TBS) zingatia hilo. Lakini pia vifungashio vizuri huvutia wateja na pia hutunza ubora wa bidhaa yako. Kwa upande wa lebo kuna vitu vya kuzingatia ambavyo kabla haujatengeneza unatakiwa kuwaona TFDA kwa ajili ya maelezo kutokana na viwango(standards) inavyosema.

5.UHIFADHI WA BIDHAA(storage)
Bidhaa iliyotengenezwa inatakiwa ihifadhiwe kwenye sehemu safi . pia bidhaa inatakiwa ikaguliwe Mara kwa Mara na kugeuzwa ili kuzuia kuharibika kutokana na joto nk

6.USAMBAZAJI(distribution).
Hatua hii ni ya usambazaji wa bidhaa yako kwenda kwa mlaji, vifaa vinavyotumika kusafirishia bidhaa vinatakiwa viwe visafi k**a nilivyoeleza kwa upande wa malighafi. Hizi ndio hatua za usindikaji.(processing steps).
Karibuni kwa maswali, mapendekezo, ushauri napatikana 0685295391 Juliana Kitinde mtaalamu wa maswala ya usindikaji wa vyakula na vinywaji....itaendelea

19/05/2018

Malighafi bora-bidhaa bora, upatikanaji wa masoko kwa urahisi. Tunahimizwa kutengeneza bidhaa zilizo bora kwa kufuata kanuni bora za usindikaji wa chakula.

Leo tutaangalia ubora wa malighafi na bidhaa.

Malighafi ni vyakula ambavyo havijasindikwa mfano matunda, nafaka nk.

SIFA ZA MALIGHAFI BORA

Yawe ni mazao yaliyovunwa kwa wakati na kutunzwa.

Yasiwe yamesinyaa

Yasiwe na ukungu na kuharibiwa na wadudu

Yawe yamekauka vizuri kwa kiwango kinacho takiwa

Yasiwe na uchafu

Punje zilizopasuka kwa upande wa nafaka zisitumike kwa kusindikwa.

BIDHAA BORA

Isiwe na uchafu
Iwe na harufu nzuri na ladha ya asili.

STOO
Iwe safi na isafishwe mara kwa Mara

Lazima iwe mzunguko wa kutosha wa hewa(ventilation).

Malighafi/bidhaa iliyohifadhiwa mwanzo ndiyo itumike kwanza.

Stoo ya bidhaa zilizosindikwa itenganishwe na stoo ya malighafi na vitu vingine.

Nafaka ziwekwe juu ya chaga(pallets) na zisigusane na ukuta

Zingatia matumizi ya viuwatilifu(pesticides) na kemikali zilizoruhusiwa katika hifadhi ya chakula ili kuzuia kusibikwa(contamination) kwa malighafi au vifungashio, weka malighafi yako kwenye ubaridi nyuzi joto 25°C.

Bidhaa zilizosindikwa, vifungashio na viambaupishi vihifadhiwe katika stop safi na kavu katika mashelfu

VIFUNGASHIO

Vihifadhiwe sehemu kavu na safi

Visiathiri au kuharibu ubora wa bidhaa

Vikidhi mahitaji ya bidhaa na matakwa ya soko

Viwe safi, visiingize unyevu, vumbi au wadudu

Visipoteze au kuchukua harufu.

NINI KINATAKIWA KUWA KWENYE VIFUNGASHIO.

Jina la bidhaa husika

Orodha ya malighafi

Uzito kamili wa bidhaa

Maelezo ya namna ya utumiaji yaonyeshwe kwa vielelezo

Jina kamili na anwani ya mzalishaji

Nchi ilipotengenezwa bidhaa yako

Lugha ya kiswahili au kiingereza kutegemea na solo

Tarehe iliyotengenezwa na mwisho wa matumizi

Nambari ya bachi/loti

Taarifa za kilishe ziwe ambazo hazipotoshi

Alama ya ubora iwapo bidhaa imekidhi vigezo vya kiwango husika

Maelezo ya matumizi yawe kulingana na kipimo maalumu.

Wasindikaji wanashauriwa kuzingatia ubora wa malighafi wanayotimia baada ya kuvuna na hata kipindi cha kuhifadhi kuepuka uharibifu wa malighafi na upatikanaji wa bidhaa iliyo chini ya kiwango baada ya kusindika.

Kwa upande wa eneo la kuhifadhia yaani stoo, usafi ni mhimu sana ili kuepusha maambukizi kati ya malighafi moja na nyingine hivyo unashauriwa baada ya kutoa malighafi, usafi ufanyike kwa kina ili kuweza kuhifadhi malighafi nyingine.

Kwa upande wa bidhaa, zingatia sana swala la usafi, kwani linaweza kuharibu ubora wa bidhaa yako na kupunguza soko la bidhaa. hiyo.

Labda nitoe angalizo katika hili.

Asilimia kubwa ya wasindikaji wa Tanzania, wanasindika majumbani, hill siyo tatizo kwa kuanza unachotakiwa kufahamu ni ule mchoro wa usindikaji unatakiwa uweje( production flow chart), hii itakusaidia kugawanya sehemu uliyo nayo na kuepusha changamoto za kuzalisha bidhaa isiyo kidhi viwango has a katika swala la ubora na masoko. Kwenye huu mchoro kuna taratibu za kufuata kutofautisha eneo la kupokelea malighafi, eneo la uzalishaji, na eneo la uhifadhi(stoo).
Wasindikaji wengi wanapata changamoto katika hili na wengine wameshindwa kupata vibali mfano TFDA kwa sababu ya kutofahamu mchoro wa usindikaji.

Kwenye swala vifungashio, unashauriwa kuweka bidhaa yako kwenye vifungashio vizuri na vinavyokidhi viwango, vifungashio vizuri ni vivutio kwa wateja hivyo vinaongeza soko la bidhaa yako.

Lebo inayowekwa kwenye bidhaa yako hakikisha ina taarifa zinazoeleweka na kwa kufuata kanuni za uandishi kamili wa lebo hiyo.
Itaendelea...nakaribisha maswali, ushauri mapendekezo kwa mawasiliano zaidi ili upate huduma za usindikaji , ushauri, uchoraji michoro kwa ajili ya usindikaji piga 0685295391 what's up napatikana ..Juliana Kitinde mtaalamu wa maswala ya usindikaji vyakula na vinywaji

13/04/2018

Tunaendelea na kanuni bora za usindikaji. Kipindi cha nyuma tuliweza kujifunza kanuni bora ya uzalishaji(Good Manufacturing Practices) , kanuni bora ya usafi(Good Hygiene Practice) pamoja na HACCP(Hazard Analysis and Critical Control Points) kwa mtu yeyote anayemiliki au anayetarajia kuanzisha kiwanda. Kanuni au nyezo hizi hutumika katika sehemu zote za maswala ya usindikaji. Tulijifunza pia kuwa msindikaji ni nani na anatakiwa kufanya nini. Leo tutajifunza

ENEO LA USINDIKAJI NA MAZINGIRA YA ENEO LA USINDIKAJI.

Eneo la usindikaji ni jengo linalotumika katika usindikaji na mazingira yanayozunguka. Eneo hilo linatakiwa kuwa na sifa zifuatazo

°Sakafu na ukuta viwe vya kusafishika na paa lisiwe linapitisha maji. Sakafu isiwe inateleza ili kuepusha ajali kwa wafanya kazi. Mfano tiles(marumaru) unayoweka hakikisha isiwe na mtelezo.

°Madirisha yawe na nyavu kuzuia wadudu na uchafu kupenya.

°Eneo(jengo) lisafishwe kabla na baada ya kusindika.

°Sehemu ya usindikaji kusiwe na wanyama wa aina yeyote.

°Maji ya taka yamwagwe kwa uangalifu bila kuchafua mazingira.

°Mazingira yawe safi na takataka zihifadhiwe nje ya jengo.

°Pawe na maji safi na salama

°Hakikisha kuna choo, kuwe na maji na kisafishwe mara kwa mara. Choo kinatakiwa kuwa na umbali kidogo na jengo la usindikaji kwa ajili ya usalama wa bidhaa.

°Kuwe na eneo(chumba) cha kubadilishia nguo wafanya kazi.

°Eneo(chumba )cha kuhifadhia malighafi kitofautishwe na chumba cha kuhifadhia bidhaa baada ya kusindika

°Kuwe na mitaro ya kupitisha maji(drainage system) kuepusha maji kutuama.

°Eneo la usindikaji lazima liwe na vyombo vya kuhifadhia taka(dustbin) kwa mda mfupi usindikaji ukiwa unaendelea.

°Eneo la usindikaji linatakiwa kuwa na hewa ya kutosha( ventilation) kwa ajili ya usalama wa wafanya kazi , malighafi na bidhaa pia.

Kuna vifaa mbalimbali vinavyotumika kwenye usindikaji k**a vile mashine, bomba(pipes), masink nk. Vifaa hivyo vinatakiwa kuwa na Sifa zifuatazo.

Vinatakiwa kuwa na vyuma vya pua( stainless steel), plastic, udongo, aluminiamu, kioo, karatasi nk. Vifaa visivyofaa ni vile vya risasi , chuma na shaba.

K**a unazalisha bidhaa mbili tofauti vyombo vinavyotumika visafishwe kabla ya kusindika bidhaa zingine.

Vyombo vya kuwekea taka viwe na mfuniko.

Tumia sabuni, dawa na brushi kusafisha.

Itaendelea, karibuni kwa maswali, mapendekezo, ushauri, maelekezo

Juliana Kitinde Mtaalamu wa maswala ya usindikaji wa vyakula na vinywaji(Food Scientist) kutoka Chuo Kikuu Cha Sokoine...0685295391/ 0623946883 whatsup karibuni

11/04/2018

Tusindike mazao yetu ili kuepusha upotevu wa mazao baada ya kuvuna. Tanzania ya viwanda tunaweza.

Kipindi kilichopita tulijifunza usindikaji wa unga wa lishe. Kabla sijaendelea na masomo ya usindikaji ningependa tujifunze kwanza kuhusu

KANUNI BORA ZA USINDIKAJI WA VYAKULA NA VINYWAJI

Kuna nyenzo kuu tatu ambazo msindikaji wa vyakula na vinywaji lazima azifuate wakati wa kusindika.

1.Kanuni bora ya uzalishaji(Good Manufacturing Practices {GMP})
2.Kanuni bora ya usafi(Good Hygiene Practices {GHP})
3.Hazard Analysis and Critical Control Point( HACCP) nyenzo hii hubeba nyenzo mbili zilizotangulia.

Nyenzo hizi humsaidia msindikaji kutengeneza bidhaa bora na pia kupata nembo ya ubora (TBS mark) kwa ajili ya bidhaa yako. Inashauriwa kutumia kanuni(nyenzo) hizi mda wote wa usindikaji kwa wasindikaji wote kuanzia majumbani na viwandani pia.

Kanuni bora za usindikaji zinahusisha makundi yafuatayo, msindikaji, eneo/ mazingira ya usindikaji,ubora wa malighafi na bidhaa, uhifadhi malighafi pamoja na usafirishaji wa malighafi.

Msindikaji(mzalishaji) ni mtu yeyote anayehusika na maswala ya usindikaji / MTU yeyote anayefanya kazi kwenye eneo la uzalishaji k**a vile kupokea malighafi, kusindika malighafi na kufunga(packing).

Msindikaji anatakiwa
°Kuwa na sare husika k**a vile Viatu(safety boot), overol, kofia na vitu vingine ambavyo hutegemea aina ya malighafi inayosindikwa.

°Apime afya kabla ya kuanza usindikaji kwa ajili ya usalama wa bidhaa

°Afunike nywele , pua na mdomo mda wote wa usindikaji kwa ajili ya usalama wa bidhaa.

° Anawe mikono kabla ya kusindika na baada ya kutoka chooni

°Akate kucha na asizipake rangi

° Asijishikeshike na ajizuie kupiga chafya wakati wa usindikaji

°Asitumie marashi

Hizi ni kanuni na taratibu kwa wanaofanya kazi kwenye eneo la usindikaji. Kuna baadhi ya makundi ya vyakula mfano vyakula asili ya wanyama k**a vile nyama, samaki, maziwa, pia mboga na matunda , msindikaji anatakiwa kutumia kanuni hizi kwa uangalifu sana kuanzia kwenye upokeaji wa malighafi, usindikaji na uhifadhi wa bidhaa kwani aina hizi za malighafi hushambuliwa virahisi na vimelea(microbes) na kupelekea kupoteza ubora wa chakula kabla ya kusindikwa

Kanuni bora ya uzalishaji(Good Manufacturing Practices), Na Kanuni bora ya usafi(Good Hygiene Practices) ni kwa ajili ya bidhaa bora hivyo hazina budi kutekelezwa ipasavyo.

Kuna wasindikaji ambao wanapata shida kuhusu nembo kupata ya ubora(Tbs Mark) tukimaliza somo hili utatambua ni sehemu gani hukufuata kanuni hizi. Lakini ukipata shida zaidi wasiliana na mtaalamu wa maswala ya usindikaji wa vyakula na vinywaji tupo kwa ajili yako kukusaidia

Kwa wasindikaji wanaotarajia kuanza jaribu kujifunza kwa kina kuhusu hizi kanuni pia unaweza ukawasiliana na mtaalamu kwa ajili ya maelekezo zaidi. Msipate shida tupo kwa ajili yenu kuwasaidia..itaendelea

Juliana kitinde Mtaalamu wa usindikaji wa vyakula (mhitimu kutoka chuo kikuu cha kilimo Sokoine(Sua)...0685295391
K**a una shida, ushauri ,mapendekezo, maswali karibu unaweza wasiliana, na mimi kwa what's up kwenye hiyo namba

20/01/2018

Kwenye kipindi kilichopita tuliona ni kwa jinsi gani nafaka hasa mahindi inavyoweza kushambuliwa na kuvu(aflatoxin) ambao huzalisha sumu kuvu na kuhatarisha afya ya mtumiaji. Tuliweza pia kujifunza jinsi ya kuthibiti kuvu kwenye nafaka, kwa kukausha mahindi vizuri kabla ya kuyahifadhi.
Leo tutajifunza

USINDIKAJI WA MAHINDI

Kusindika ni kitendo cha kubadili malighafi za kilimo kiumbo na kikemikali kwenda kwenye chakula. Usindikaji huongeza thamani ya zao.

Mahindi husindikwa kupata punje kwa ajili ya makande na unga, bidhaa zingine zinazotokana na mahindi ni mafuta na wanga.

USINDIKAJI WA MAHINDI KUPATA UNGA.

Aina za unga
1. Unga wa mahindi yasiyokobolewa(Dona)
2.Unga wa mahindi yaliyokobolewa(sembe)

Unga wa mahindi yasiyokobolewa(Dona).
Vifaa.
Machine ya kusaga, ungo, dumu au ndoo, mifuko na chekeche la nafaka.

Jinsi ya kusindika.
Pepeta mahindi ili kuondoa vumbi na takataka nyingine, tumia Sinia, ungo au chekeche.

Unaweza ukayaosha k**a mahindi yana sumu ambayo inaweza kumdhuru mtumiaji kwa maji safi na kuanika sehemu safi hadi yakauke vizuri.

Saga mahindi na hifadhi kwenye vifungashio vya kuhifadhia unga. Hakikisha sehemu unayotumia kuweka unga wako ni safi.
Unashuriwa kutumia Vifungashio(packaging materials) ambavyo vinauzuia unyevu mfano karatasi isiyopitisha unyevu( paper bags ) pamba nk.
Hushauriwi kutumia nailoni kwa sababu inatengeneza joto ambalo husababisha kuota kwa vimelea aina ya mould na hivy kupelekea kuharibika kwa unga.

Vifungashio vinatakiwa viwe na muonekano mzuri ili watumiaji waweze kununua bidhaa yako kwa wingi.
Zingatia sana swala la unyevu kwenye mahindi kabla ya kusaga na vifungashio unavyotumia kwa sababu unyevu ni moja ya sababu kubwa inayoharibu unga kwa asilimia kubwa.

Unga wa dona una virutubisho vyote vinavyopatikana kwenye mahindi mfano madini ya chuma(iron) vitamin, fats(mafuta) nk. ni mzuri kwa afya ya mtumiaji.

Matumizi ya unga
Hutumika kutengeza ugali, uji, togwa na pia huchanganywa na shairi kutengeneza via. Itaendelea karibuni wajasiriamali na wengine wote kwa maswali na ushauri...0685295391/0757186435

Mahindi yaliyoshambuliwa na kuvu/fangasi(aflatoxin).
02/11/2017

Mahindi yaliyoshambuliwa na kuvu/fangasi(aflatoxin).

Address

4292 Nkuhungu
Dodoma

Telephone

0685295391

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Usindikaji Na Utunzaji Wa Chakula Kupata Bidhaa Bora posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Usindikaji Na Utunzaji Wa Chakula Kupata Bidhaa Bora:

Share