08/09/2019
Ni namna gani watu wanaweza kupika mimea yenye sumu kuwa chakula salama?
Mwaka 1860, Robert Burke na William Wills walifahamika kwa kuongoza msafara wa kwanza barani ulaya ambao ulijulikana Australia yote.
Msafara huo haukwenda vizuri kutokana na uongozi mbaya na mipango isiyokuwa na utaratibu pamoja na mikosi.
Wakati wa kurudi, wasafiri hao walipata changamoto ya chakula na kutokuwa na maji ya kutosha .
Hali hiyo ya kukwama jangwani bila chakula iliwapelekea kutengeneza chakula ambacho walijua ni sumu lakini walikuwa hawana njia nyingine ya kuendelea kuishi.
"Ngamia wote walikiwa wanakufa kwa sababu tulikuwa hatuna chakula cha kuwapa na tulikuwa tunajaribu tuweze kupona iwezekanavyo."
Wanakijiji wa eneo hilo la Yandruwandha walikuwa wanaishi licha ya hali ya eneo hilo.
Wenyeji waliwapa keki ambazo zimetengenezwa na unga wa mhogo .
Njaa za wasafiri hao Burke,Wills na King ziliwafanya kutokua na jinsi zaidi ya kula kwa sababu walikuwa wameishiwa nguvu.
King ndio msafiri pekee aliyetarajiwa atapona baada ya miezi kadhaa ambapo msaada ulifika kutoka ulaya
Chakula kilichowafanya kupona jangwani, kilifanya watu wafanye udadisi.
Chakula hicho hicho cha muhogo,mtu hawezi kusema kuwa ni sumu katika nchi nyingi za Afrika.
Wakulima barani Afrika wanalima zao hilo kwa ajili ya chakula na biashara.
Ingawa hata baadhi ya maeneo nchini Tanzania baadhi ya makabila huwa ni mwiko kwao kula mhogo kwa madai kuwa ni sumu.
Nchini Tanzania , wenyeji wa Kilimanjaro wa kabila la wachaga wamekuwa wakidai kuwa chakula hicho ni sumu na hivyo kuwa na utamaduni wa kutokula mihogo.
Lakini siku za hivi karibuni hali imeanza kubadilika pia.
"Ni sisi wachaga wa mjini hapa Dar es salaam ndio tunakula mihogo lakini asili yetu tangu enzi na enzi huwa hatuli mihogo kwetu kwa sababu tunaamini kuwa ni sumu." Mtanzania mmoja mwenye asili ya uchaga alieleza.
Mihogo ni chakula ambacho kina virutubisho vingi kwa afya ya binadamu k**a vitamini na madini.Kuna mihogo ambayo ni mitamu na ambayo