08/02/2018
Habari ndugu zangu,
natumaini wazima na tunaendelea kupambana na ujenzi wa taifa. Tukiwa tunapambana kila mtu ana njia zake anazozipitia ili kutimiza ndoto zake, lakini je tushawahi kujiuliza kwa nini tunatumia mda mwingi kutimiza na kupata ufumbuzi?
Bhas zingatia haya...
Usiishie kushangaa mali za mtu aliyefanikiwa au anaye elekea mafanikio, jifunze njia anazopitia kwa kutazama mipango yake, maamuzi yake, uthubutu wake, jitihada zake na jinsi anavyo tatua changamoto anazopitia, ili siku moja utakapoamua kuchukua hatua za kuishi ndoto zako k**a yeye, uwe unajua njia za kupitia,
usimshangae na kumpiga majungu, mfuate na kumuuliza maswali ili kujifunza,
andika unayojifunza ili kujazia pale ambapo ulikua unahitaji kujazia juu ya yale unayojua, au kuweka kumbukumbu zitakazokusaidia wakati wa kuanza kusimama mwenyewe katika mipango yako...
kujifunza ni kila siku na kila mara kwahiyo usiogope,
ila usiishie kujifunza na kuendelea kuota mafanikio bila ya kuchukua hatua...STOP STEARING. LIVE YOUR DREAM