kukushop.com

kukushop.com Page hii kazi yetu ni kutoa elimu ya ufugaji tunapokea oda ya vifarnga aina zote pia tunafanya upembuzi wa mradi wa ufugaj like page hii tufanyekazi.karibu

pata elimu ya ufugaji nunua na uza kuku na mifugo mingine hapa uliza kuhusu kilimo na mifugo utajibiwa haraka hapa kukushop.com

08/09/2025

STAPHYLOCOCCOSIS KWA KUKU 🐓❗
Hivi ndivyo ugonjwa huu unavyoweza kuathiri kuku wako endapo hautatibiwa mapema. Tambua dalili, chukua hatua mapema, linda afya ya kuku wako.

Staphylococcosis kwa Kuku ni maambukizi ya bakteria yanayosababishwa na Staphylococcus aureus. Ni ya kawaida kwenye mashamba ya kuku, hasa pale ambapo kuna majeraha, usafi duni au msongamano.

✓ Jinsi Unavyowaathiri Kuku

Bakteria huingia mwilini kupitia:
~ Majeraha (mikato, mikwaruzo, makato ya kupigana)
~ Vidonda vya miguuni au takataka chafu
~ Majeraha yatokanayo na kushika au vifaa vibaya

Mara tu yakishaingia, huenea kwa haraka zaidi kwa kuku dhaifu au walioko kwenye msongo wa mawazo.

✓ Dalili Kuu na Ishara

~ Viungo kuvimba (arthritis)
~ Kulemaa au ugumu wa kutembea
~ Maambukizi ya mguu (bumblefoot)
~ Majipu kwenye ngozi
~ Kuwahiwa kwa mashavu na pande za kichwa (wattles & comb)
~ Kifo cha ghafla endapo ugonjwa umeenea mwilini (septicemia)

✓ Matibabu

~ Antibiotiki (k**a amoxicillin, tylosin) ila zipewe baada ya ushauri wa daktari au kupimwa usugu wa bakteria
~ Kusafisha na kuua vijidudu kwenye vidonda
~ Kutumia dawa ya juu (antiseptic) kwa maambukizi ya ngozi
~ Kutenga kuku wagonjwa ili kuzuia kuenea

✓ Njia za Kuzuia

~ Kudumisha takataka safi na kavu
~ Kuepuka msongamano na vifaa vyenye ncha kali
~ Kukagua kuku mara kwa mara kwa majeraha
~ Kutunza usafi na biosecurity
~ Kuwapa virutubisho na nyongeza za kinga mwilini

👉 tembelea fb page ya kukushop.com kwa mafunzo zaidi 0714167626whtasp

18/04/2025

Habari wafugaji woote mliofanikiwa na wale ambao bado mnachangamoto karibuni kukusho.com kwa ushauri mzuri

Kwamahitaji ya vifaranga,elimu juu ya ufugaji na ushauri,karibuni sana
03/04/2024

Kwamahitaji ya vifaranga,elimu juu ya ufugaji na ushauri,karibuni sana

11/05/2023

MAMBO KUMI MUHIMU KATIKA UFUGAJI WA KUKU WA KISASA :
1. BANDA BORA:
Banda liwe na sifa zifuatazo: Liweze kupitisha mwanga hewa ya kutosha na vilevile liwe na kinga ya upepo mkali, mvua ya upepo na jua. Banda hili pia lapaswa kujengwa mahali ambapo hapatuamishi maji, panapoweza kufikika kirahisi na mfugaji wakati wa uangalizi, liwe
mbali na mabanda mengine ya kuku na pia liwe mbali na barabara na shughuli zenye kelele nyingi ili kuepuka usumbufu kwa kuku.
2. KUCHAGUA VIFARANGA BORA:
Ni muhimu kwa mfugaji kufahamu mahali pa kupata vifaranga bora wa mayai au nyama. Ni vyema mfugaji akanunua vifaranga kutoka vyanzo vilivyothibitishwa k**a vile Farmers Centre Chicks, Amadori na wengineo. Epuka kununua vifaranga toka vyanzo visivyokuwa vya uhakika ili kuepuka athari mbalimbali wakati ukifuga kuku hawa. Vifaranga bora ni vile vyenye nguvu, visiwe na vilema au magonjwa ya kuambukizwa. Vilevile ni muhimu kuhakikisha kuwa vifaranga hawa wamepewa chanjo dhidi ya magonjwa k**a Mahepe (Marek’s) n.k
3. JOTO LA KUTOSHA:
Joto la wastani ni muhimu sana katika uhai wa kuku, katika juma la kwanza joto linalostahili ni nyuzijoto 35oC na hupimwa kwa kipima joto na kiasi hiki cha joto kipunguzwe kwa nyuzijoto mbili kila juma hadi kufikia nyuzijoto 27oC katika juma la nne. Pamoja na kupima joto unashauriwa uangalie tabia na mwenendo wa vifaranga. K**a vifaranga vikichangamka na kunywa maji vizuri na kutawanyika sehemu zote joto hilo linatosha. Ikiwa joto halitoshi hujikusanya karibu na taa au hujirundika sehemu moja, hivyo unashauriwa kuongeza joto kwa kuongeza idadi ya vifaa au nguvu ya joto kwa mfano taa za umeme. Joto likizidi utaona vifaranga vinakaa mbali na taa vikipanua mabawa yao na kuhema haraka haraka. Hali hii ikizidi husababisha ugonjwa wa joto jingi (heat stroke) na hupelekea vifaranga kuamguka chini.
HALI YA HEWA NA MATOKEO YAKE
4. ULEAJI MZURI WA VIFARANGA:
Mara baada ya vifaranga kuwasili bandani, vikaguliwe vihesabiwe, na kisha viwekwe kwenye sehemu maalum ya kulelea (Brooder). Kisha vipewe maji safi ya uvuguvugu yenye dawa za viubakteria (Antibiotics) k**a vile OTC Plus, Neoxyvital na glucose.
Baada ya wiki nane kuku wawekwe kwa mujibu wa idadi katika banda, kwa mfano:
• Kuku wa nyama wawekwe 9 hadi 10 kwa mita moja mraba.
• Kuku wa mayai wawekwe 5 kwa mita moja mraba.
• Kuku wa mbegu (Parent stock) kuku 3.5 hadi 4.5 kwa mita mraba.
Nafasi katika banda huwafanya kukua haraka, kutaga vizuri na kwa pamoja.
5. MAJI SAFI
Pamoja na chakula hakikisha kuku wako wanapata maji safi na ya kutosha kila siku. Maji safi ni muhimu kwa vile maji yasiyo salama ni njia kuu ya isababishayo magonjwa. Maji husaidia kuyeyusha na kusafi risha chakula mwilini, kutengeneza mayai na kupunguza joto mwilini.
MANYWESHEO
6. CHAKULA:
Chakula hiki hutengenezwa kwa kuzingati a utaalamu wa lishe ya kuku, kwa mfano chakula cha vifaranga huwa laini na proti ni nyingi, chakula cha kuku wakubwa huwa cha chenga na nguvu ya joto zaidi, vilevile, itabidi izingati we kwamba kuku wa mayai asilishwe chakula cha kuku wa nyama kwani atanenepa na kushindwa kutaga. Aidha umri wa utagaji hasa kwa kuku wa mayai na upatikanaji wa aina za nafaka na mashudu yatokanayo na mbegu za mafuta ni muhimu kuzingati wa wakati wa ulishaji au utayarishaji wa chakula cha kuku.
MALISHIO
Wakati ukiwalisha kuku wako, unaweza kutumia malishio (Feeder) za kisasa au vihori ambazo hutengenezwa kwa mbao na vijazwe chakula kufi kia theluthi mbili kwa siku. Ili kuhakikisha kuwa kuku wanakuwa vizuri na kwa pamoja (uniform growth) ni muhimu kuhakikisha kwamba vifaranga wote wanapata nafasi ya kula chakula cha kutosha kila mara.Chakula hiki kiwe kimechanganywa na dawa ya kuzuia magonjwa k**a vile coccidiosis, (Ridocox/Salcox) salmonellosis(Colirid) kati ka kiwango kinachotakiwa.
VICHANGANYIO KATIKA CHAKULA
7. USAFI WA BANDA:
Hakikisha banda lako linasafi shwa na dawa za kuulia vimelea kwa mfano V-RID kila kabla na baada ya kuweka kuku, hii inasaidia kukinga kuku wako na magonjwa yanayoambukiza k**a Marek’s, Gumboro, Koksidiosis (Kikoti ) na kuharisha (Salmonellosis). Vyombo vya chakula, maji pia vioshwe kwa V-RID. Madirisha, milango, waya, kuta na kila kitu kioshwe kwa dawa ya V-RID. Pia Vyombo visafi she na maji na kubadilishwa mara mbili kwa siku.
8. KINGA ZA MAGONJWA:
Ni vema kuhakikisha kwamba kuku wanapati wa chanjo za kuzuia magonjwa mbalimbali k**a Newcastle, Gumboro, Marek’s. wakiwa na umri kuanzia wanapozaliwa hadi wiki ya tatu. Kinga hizi lazima zihifadhiwe na zitumiwe k**a inavyoshauriwa na wataalamu. Mfano wa dawa za kinga zinazoshauriwa kitaalamu ni k**a Thermostable 1, Newcasle lasota, Gumboro, Ndui na nyinginezo.
9. KUKINGA MAGONJWA SUGU
Magonjwa sugu ambayo huuwa au kudumaza kuku katika umri wote ni k**a
(a) Coccidiosis – Inakingwa kwa kuweka dawa mfano RIDOCOX au SALCOX kwenye chakula na inatibiwa na Amprolium na dawa za jamii ya SALFA.
(b) SALMONELLOSIS na E. coli Infections: Hukingwa kwa kutumia kiua bakteria k**a FARMACID Premix au COLIRID katika chakula. Tiba ni kutumia FLUBAN au DOXYCOL
(c) Mafua – Chronic Respiratory diseases, Infectious coryza na mengineyo.
Jitahidi kuzua vumbi katika mabanda,
Tumia TYLOFARM Premix au ANFLOX Feed Premix katika chakula.
(d) Sumu ya fangasi katika chakula:
Sumu hii ina athari kubwa k**a vile kuharisha, inadumaza na kuua. Inaweza kukingwa kwa kutumia MYCOBIND Katika Chakula.
10. FUATA KANUNI ZA UFUGAJI BORA:
Ni muhimu kwa mfugaji kuwa na uelewa wa kutosha wa kanuni za ufugaji bora ili aweze kupata matokeo mazuri. Baadhi ya kanuni hizi ni k**a vile,
• Kuwalea vifaranga vizuri
• Uelewa wa kuyatambua na namna ya kuyadhibiti magonjwa mbalimbali,
• Namna ya kutumia kinga na madawa kwa kiwango na wakati sahihi,
• Vyakula vinavyofaa kwa aina na umri wa kuku na
• Usafi wa banda lake.
Iwapo mfugaji atazingatia kanuni hizi k**a inavyoshauriwa kitaalamu basi hakuna shaka ya kutopata matokeo anayotarajia.
KWA MSAADA ZAIDI
TEMBELEA KURASA HIZI ZA KUKUSHOP. COM

dalasa
17/06/2022

dalasa

Kazi ya jogoo ni kurutubisha yai (kutia mbegu)pasipo na jogoo huwezi pata kifaranga
kuku anaweza taga yai hata k**a jogoo ajampanda ila hilo yai halitakuwa na mbegu mpaka jogoo ampande
ingawa kuna njia ya kupandikiza mbegu kwa kuku lakini ni ya gharama
ushauri wangu k**a unahitaji kuwa na kuku wengi wenye afya basi jali sana aina ya jogoo anaempanda kuku wako
pia k**a unahitaji kupata ushauri juu ya ufugaji njoo kukushop.com tuongee kuhusu mifugo
0714167626

17/06/2022

*JAMANI NIWAIBIE SIRI*
☝️Broiler hawahitaji mambo Mengi kiviile ili wakue ipasavyo zingatia haya *UTANISHUKURU*

🤝Eneo ( weka *kuku 10* Kwa Mita moja mraba), ukizidi Sana weka kuku *11* , Randa hazitaloa Sana, hivo *Coccidiosis* itapungua Kwa sehemu kubwa Ukizidi zaidi ya hapo *Unajitafutia shida za reja reja*

☝️Wape *Chakula Bora,* Starter, Grower na Finisher Kwa mujibu wa maelezo ya Kampuni ulikonunua chakula

👉Wape *chanjo* Kwa muda mwafaka, jitahidi Sana Kuzuia kuku Kuumwa ili *Ratiba ya chanjo isibadilike Sana zaidi ya Siku 3*

🤝 *Vitamins*, Sehemu Muhimu zaidi kwenye ufugaji wa Broiler , Jitahidi kuwapa Kuku wako *Vitamin* Kuliko kuwapa *Madawa*
❗ Mfn: Wiki 2 za mwanzo ukiacha siku za chanjo wape *Vitamin Kwa kubadili badili, au Biospark* Huna haja ya Kutumia saana Booster Wakiwa wadogo ( *Mimi situmii booster yoyote zaidi ya Vitamin Hadi navuna na Kuku wanakua na uzito unoatarajiwa* )

‼️ *UNATAKIWA KUFAULU MALEZI YA VIFARANGA* ‼️
👉Wastani uzito SIKU YA 7 Gram 220-225
👉Siku ya 14 gram 550-600
👉Siku 21 Gram 1100-1200

*ILI UFIKIE UZITO HUU*
👉Uwiano wa Vyombo vya Chakula na Maji inapaswa kuwa Sahihi bila kukosewa.

KARIBUNI TUFUGE BROILER KWA UFANISI
UKIWA NA SWALI
like page

KWA HUDUMA BORA YA UFUGAJI NA KILIMO KARIBUNI KUKUSHOP.COM
08/02/2022

KWA HUDUMA BORA YA UFUGAJI NA KILIMO KARIBUNI KUKUSHOP.COM

ufugaji wa zaman changamoto zilikuwa chache tofauti na ufugaji wa siku hizi changamoto nyingiebu tupeni maoni yenu wadau...
26/02/2021

ufugaji wa zaman changamoto zilikuwa chache tofauti na ufugaji wa siku hizi changamoto nyingi
ebu tupeni maoni yenu wadau ili tupate faida sote

12/11/2020
malezi ya vifarangapata somo la uleji wa vifaranga kupitia group letu la kukushop bila malipo weka namba nikuungesiweki ...
12/11/2020

malezi ya vifaranga
pata somo la uleji wa vifaranga kupitia group letu la kukushop bila malipo weka namba nikuunge
siweki link coz kuna watu hawapo sirius na hili

07/09/2020

NAHITAJI LAYERS WALIO ZEEKA
0688882973

15/06/2020

VIFARANGA BORA MBEGU YA KROILERY WANAPATIKANA KWA BEI YA OFA
1600 KWA KIFARANGA
0714167626

Address

Kinondoni

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when kukushop.com posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to kukushop.com:

Share