Mr. Atugoli

Mr. Atugoli This page covers consultant services on job analysis. it is the division of EMC Company deals with

This page provide to you motivational notes and quotes, consultations, business idea and development dialogue. it also share success stories and stories from others on life challenges and business opportunity and challenges. it is designed to cover a wide range of individuals, companies, politicians, humani right and governance activist, corporate society, it inclusive of age that is from children

to adult people as content in this page is closely administered. Please share what you think others will get helped and make you happy.

28/03/2024

As we explore Julius Nyerere's profound insights from his visionary 1963 piece on "A United State of Africa," where he declared unity our "new struggle," it's crucial to reflect on our journey towards this lofty ideal. 🌍✨ How far have we come? Are we moving closer to unity or drifting further apart?

In light of the ongoing complexities in the Democratic Republic of Congo (DRC), the Haiti question, and the enduring sovereignty debates over Western Sahara, we find ourselves at a crossroads. 🤔💡 These situations offer us a mirror, reflecting our strides toward solidarity and the fissures that still need mending.

Where do we truly stand in this struggle for unity? Are these challenges merely hurdles on the path to unity, or are they revealing deeper divides we must address? 🌱💬

This conversation is more than a reflection; it's a call to action. It's about reimagining the pan-African dream in the context of today's global and continental intricacies. Let's engage, debate, and envision a united Africa that aligns with the realities of our time. 🚀🌍

Your thoughts and insights are invaluable as we engage in this journey together.

Jamii yetu inaanza kurudi nyuma kwa speed sana. Tatizo ni nini. Yaani mtu anatoa maoni yake tunanza kuangalia nani kakwa...
01/01/2023

Jamii yetu inaanza kurudi nyuma kwa speed sana. Tatizo ni nini. Yaani mtu anatoa maoni yake tunanza kuangalia nani kakwazwa, nani apakwe pakwe mafuta, tunafumbia macho mqmbo yasiyotupendeza.

03/06/2021

R**e is used as weapon of war in . What is missing in the UNSCR 1325?

25TH MAY: African Liberation Day.African Liberation Day is a day of reflection, thinking and rethinking on issues affect...
25/05/2020

25TH MAY: African Liberation Day.

African Liberation Day is a day of reflection, thinking and rethinking on issues affected and still affecting Africans in Africa and Diaspora. It is also a day of passing over knowledge and history of Africa from past, present and future generation. Bringing to the present the evils of the past (colonialism, slave trade, racism, injustices, torture) and the blood of our fore-further in the struggle to put to an end all the evils of the past. Project the future of our community - Humanity, dignity, justice and prosperity.

We can bring the past to the present and teach our generation history and bad thing our brothers and sister went through. But how far are we capable of creating a critical mass of support in the struggle against the remnants of colonialism, imperialism, and Neo-liberal evils? What means and instruments we can use?

21/01/2019

Organization development Concepts: , and

There is a difference between communication, coordination of work/working Style and Hierarchies in an organization.

Communication stands for means of reaching one another, and may not means power and authority, therefore, it may be top -down or bottom - up,

Coordination is just a means in which work may be or can be supervised to ensure production reached, again coordination does not means someone has power over-someone, but just a facilitation role. Coordinator may be appointed by either organ of the organization such as management team,or any other organization decision making body,or by virtue of ones' office may act as coordinator eg administration office in an organization can perform this role. This also does not means reporting systems.

Hierarchies this means relationship with power and authority, that if someone is above an individual in organization hierarchies it means such a person has power and authority of other. for example sales manager and sales officer. this means also reporting systems. One need to report to his or her immediate person in organization hierarchies.

31/08/2018

CCM HAIWEZI KUIMARIKA K**A HAITAKUWA NA UPINZANI IMARA.
HISTORIA ya vyama vingi vya siasa nchini si ya muda mfupi k**a wengi wanavyofikiri, historia yake inaanzia katika harakati za kudai uhuru miaka ya 1950. Wakati huo vyama vya upinzani vilianzishwa kwa malengo ya kufanya siasa kwanza za kudai uhuru, na pia kutetea maslahi ya makundi ya watu ndani ya jamii k**a wafanyakazi na wakulima. Vyama vya siasa vilivyokuwapo wakati wa kudai uhuru ni pamoja na chama cha ‘Tanganyika African Association’ (TAA) ambacho kilianzishwa mwaka 1929 kikuundwa na wafanyakazi. Chama hiki lengo lake kubwa lilikuwa kutetea maslahi ya wafanyakazi dhidi ya serikali ya kikoloni. Wapo watu waliokifananisha chama hiki na chama cha wafanyakazi na kuwa kisingeweza kufikia malengo ya uhuru. Chama cha TAA ndicho kilichobadilishwa mwaka 1954 miaka miwili baada ya baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kujiunga nacho, na kuwa Tanganyika African National Union (TANU). Tofauti na TAA, TANU ilikuwa chama cha kisiasa moja kwa moja ambacho malengo yake yalikuwa mapambano ya kudai na kuleta uhuru, chama hiki kiliungwa mkono na karibia wananchi wote wa Tanganyika wakati huo.
Vyama vingine vilikuwa ni United People Party (UTP), African National Congress (ANC), na All Muslim National Union of Tanzania (AMNUT). Tofauti na vyama vingine vyote vilivyokuwepo wakati huo chama cha ANC kilionekana k**a chama cha vibaraka wa serikali ya ukoloni, hakikuwa na upinzani kwa kiwango cha kutosha kwa serikali. Chama cha AMNUT achilia mbali jina lake kuwa la kidini bado chama hiki kilifanya siasa za kitaifa kwa lengo la kuleta uhuru. Lengo hapa si kueleza historia bali kuonyesha kwa jinsi gani siasa za upinzani nchini mwetu sio za leo k**a wengi hasa wanasiasa vijana wanavyoamini. Labda tujikumbushe baadhi ya kesi na makatazo yaliyotolewa na serikali ya kikoloni wakati huo ili tuweze kuona picha ya ukoloni wakati huo. Mtakumbuka miaka ya 1958 Mwalimu Nyerere akiwa ndiye kiongozi wa TANU alifunguliwa kesi na kukutwa na tuhuma ya kumkashifu mkuu wa Wilaya (Bwana – DC) mkutanoni, kesi ambayo hadi leo inazungumzwa katika siasa za Tanzania. Kisa kingine cha kujikumbusha ni vile Mwalimu Nyerere alivyochaguliwa kuwa mjumbe wa Baraza la kutunga sheria (LEGCO) na Kujiudhuru nafasi hiyo kwa sababu ya kutaka kutetea haki za raia na kuleta uhuru kamili.
Mpaka tunapata uhuru utaona vyama vya upinzani wakati huo vilisaidia sana kuishawishi na kuisukuma serikali ya mkoloni kuweza kuachia nchi yetu. Kwa mantiki hiyo Chama Cha Mapinduzi kinapo tenda matendo yanayoonyesha wazi wazi kuwa ni kufisha upinzani na kuweza kubakia chenyewe, kinajipotezea fursa ya kujitazama na kujitathimini na pengine kupanga mikakati ya kukiwezesha kuwa imara zaidi.
Mara baada ya kupata uhuru wananchama wa TANU wakiongozwa na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere waliona ni vyema kuwa na chama kimoja, k**a nyenzo ya kuungaisha nchi. Uhamuzi wao huo ulidumu kwa kipindi mpaka mwaka 1992. Lakini kutokana na msukumo na mivutano ndani ya chama Mwalimu Nyerere akiwa sio rais wa Tanzania tena yeye mwenyewe alipendekeza mfumo wa vyama vingi. Pendekezo lake halikutokana na kuwa yeye akuwa Rais wakati huo bali lilitokana na ukweli kwamba Mwalimu Nyerere aliona kabisa ugumu wa kuendelea na chama kimoja. Aliona kabisa kuwa chama kimoja kisingeweza kuimiri ushindani na msukumo uliokuwamo ndani ya chama chenyewe.
Mwaka 1995 ulipofanyika uchaguzi wa vyama vingi wa kwanza, mgombea aliyeleta upinzani mkali alikuwa Ndg. Augustine Ryatonga Mlema akiwa na chama cha NCCR – Mageuzi ambaye alikuwa amejiengua kutoka chama cha Mapinduzi. Mgombea huyo alileta upinzani mkubwa kwa chama cha Mapinduzi kiasi cha kufanya Mwalimu Nyerere mwenyewe kuamua kurudi katika majukwaa ya siasa kukinusuru chama chake. Jambo hili tafsiri yake ilikuwa ni kwamba wakati huo uchafu na udhaifu uliokuwepo ndani ya chama cha Mapinduzi ulionekana wazi. Hivyo chama kilipata fursa kutoka upinzani kuweza kujipima na kujitathimini hasa mfumo wa siasa zake wakati huo.
Kwa sasa zipo jitihada ambazo zinaonekana kupitia matendo na matamshi kuwa vyama vya upinzani ama viondolewe au vidhoofishwe. Wapo viongozi wakubwa na makada wa chama cha Mapinduzi wa ngazi za juu, ambao wamekuwa wakitamka wazi wazi kuwa upinzani kufikia mwaka 2020 hautakuwepo. Wengine wamediriki kuwatamkia wananchi kuwa hawatapata maendeleo k**a watachagua upinzani. Matamko ya aina hii kwanza yanatufanya tufikirie zaidi juu ya dhamira ya viongozi wetu, k**a kweli wanahitaji siasa za vyama vingi, na k**a wanaouvumilivu wa siasa za vyama vingi. Lakini tafsiri ya pili ni kwamba wananchi wanatishwa na kushawishiwa kuwa hawawezi kuendelea endapo watachagua upinzani. Lakini zaidi ni kuwambaia kuwa wasijaribu kuchagua upinzania. Je wasipochagua upinzani, vyama ambavyo viko upinzani vitasalia salama? Jibu ni kwama havitakuwa salama, je CCM yenyewe itakuwa salama? Jibu ni kwamba hautakuwa salama kwani itakuwa imechaguliwa kwa hira na vitisho sio kwa utashi na upendo kutoka kwa wananchi. Kwa lugha ya kisayansi ni kwamba itakuwa serikali halali kisheria lakini haitakuwa na mamlaka kisiasa.
Ziko pia mbinu nyingine ambazo zinaonekana kuwa tishio sana dhidi ya vyama vya upinzani ambazo ni pamoja na kuhama hama kwa wanasiasa na viongozi. Jambo la kuhama hama japo wahamaji wenyewe wamekuwa wakijitetea katika majukwaa ya kisiasa kuwa wanahama kuunga mkono juhudi na jitihada zinazofanywa na serikali kuwaletea maendeleo. Sababu yao hii hajitoshelezi hata kidogo ni sababu ya kishika uchumba. Wapo wachambuzi wengi ambao wanaona hii hama hama k**a ni matokeo ya rushwa za kisiasa. Jambo hili kadiri linavyozidi kukua linaweka mazingira ya vyama vya upinzani kuwa na kazi ngumu na nzito ya kutengeneza viongozi wa kushika nafasi mbali mbali ndani ya vyama vyao na kuendeleza siasa kulingana na imani za vyama hivyo.
Njia nyingine inayotumika kudhoofisha upinzani ni k**ata k**ata na kuwafungulia kesi mbali mbali viongozi wa vyama vya upinzani. Kiongozi wa chama cha siasa ni taswira kwa wale wanaomfuata, hivyo anapoonekana mahak**ani kila kukicha si picha nzuri kwa wale wanaomfuata. Na kwa mara nyingi hali hiyo uchochea wafuasi wake kukatamaa kwani kiongozi wao hayuko nao muda mrefu. Ziko mbinu nyingi k**a hizo ambazo zinajaribu kudhoofisha upinzani. Lakini lengo la andiko hili sio kujadili mbinu hizo bali jinsi gani CCM haiwezi kuwa imara kwa kufisha upinzani.
Taadhari hii ya chama cha Mapinduzi kukosa uimara k**a hakitakuwa na upinzani imara si hoja mpya Mwalimu Nyerere katika hotuba zake aliwahi kutoa taahdhari k**a hii kwa chama cha Mapinduzi. Kwa sasa inaonekana chama cha Mapinduzi hakikumbuki au kimejisahurisha kabisa kuhusu tahadhari. Uwepo wa upinzani ni mtaji kwa chama cha Mapinduzi kwani upinzani ndio unaofanya kazi ya kuhoji sera na mipango ya chama cha Mapinduzi. Jambo hili unaweza usilione kwa haraka haraka kutokana kuwa mara nyingi vyama vya upinzani huwa havihoji wazi wazi kuwa vinahoji sera na mipnao ya CCM. Lakini kimsingi chama cha Mapinduzi huwa kinapata mchango mkubwa kutoka katika hoja za upinzani. Moja ni sera ya elimu bila malipo ambayo inatekelezwa sasa, sera hii ilitajwa kwa muda mrefu na vyama vya upinzani, vikiwa na hoja kuwa serikali ya Tanzania inao uwezo wa kusomesha watoto wake kutoka darasa la kwanza mpaka kidato cha nne bila malipo kutokana na rasilimali zake. Kwa sasa serikali kupitia chama cha Mapinduzi wanatekeleza hiyo sera. Hivyo chama cha Mapinduzi kufisha upinzani kinafanya kupoteza kipimo na pengine chimbuko la sera zake.
Kukosa mamlaka kisiasa, Mamlaka ya kisiasa haitokani na sheria bali ridhaa ya wananchi kupitia uchaguzi, wananchi wanapiga kura baada ya kusikiliza hoja za wagombea kutoka vyama vyote na wao kuona kipi kinawafaa na kukichagua. Kupitia uchaguzi wenye uchaguzi maana yake ni kwamba wananchi wanakubali kuongozwa na chama fulani. Uchaguzi wa kufikia hatua hii ni lazima uwe na washindani ambao kwa kiwango fulani wana karibiana au wako sawa kiushawishi, sio ushindani wa simba na swala. Sasa k**a vyama vya upinzani vitakuwa havina watu madhubuti wanao weza kueleza sera zao zikaeleweka kwa wananchi basi watakaoshinda katika chaguzi husika watakuwa kwa kweli wamepita si kwa hoja na sera nzuri bali kwa kukosa upinzani imara. Kutokana na kupita kwa namna hiyo basi hata heshima yao ni kidogo kwa wananchi wanao waongoza.
MWISHO.

Ma - k**arade wa siku hizi wanafurahisha sana,Uk**arade sio rangi za nguo,Uk**arade sio kadi ya usajili.Uk**arade sio mj...
17/08/2018

Ma - k**arade wa siku hizi wanafurahisha sana,

Uk**arade sio rangi za nguo,
Uk**arade sio kadi ya usajili.
Uk**arade sio mjumuiko,
Uk**arade sio kuunga mkono,
Uk**arade sio utengano,
Uk**arade sio kuhudhuria ofisi moja,

Umakarade ni mapambano
Mapambano ya jasho,
Mapambano ya damu na tafakuri
Mapambano ya Ukweli
Mapambano ya Utu
Mapambano ya Haki na Usawa
Mapambano dhidi ya udhalimu, ukandamizaji na unyonyaji
Mapambano yasiyotazama uso wa mtu, wala cheo chake.

Uk**arade sio unachama wa chama cha siasa,

Mak**arade wa leo mnachekesha sana,
Mnatafuta vyama ili mjibatize uk**arade?
Wizi huo
Mnabagua wenzenu,
Hamtaki kabisa kukosolewa.
Sio tabia ya Uk**arade
Hiyo ni tabia ya mabwenyenye
Tena bwenyenye mwenye sura ya ukatili, japo wote ni makatiri
Hamjali kabisa haki za watu,
Hamjali Utu wao,

Uk**arade umewakataa
Mmejibatiza lakini mmenajisi jina,

Mak**arade hatutasita kuwadai
kuwalazimisha, na kuwasukuma
Muachane kabisa na jina tukufu (uk**arade)

Uk**arade ni Utu, Udugu, Usawa na Haki, sio Fitina, Ukandamizaji na Udhalimu

HOJA ZA WENZETU WANAOHAMA CHAMA KIMOJA KWENDA KINGINE HAZIJITOSHELEZI.Na Ndg. Eliud KabamanyaWAKATI tukielekea katika si...
17/08/2018

HOJA ZA WENZETU WANAOHAMA CHAMA KIMOJA KWENDA KINGINE HAZIJITOSHELEZI.
Na Ndg. Eliud Kabamanya
WAKATI tukielekea katika siasa za ushindani nchini kwa maana ya kuwa na vyama vingi vyenye kuwa na sera mbadala na zaidi kuongoza katika kuchochea maendeleo ya nchi, taifa limekumbwa na zimwi la hama hama. Siasa za ushindani na vyama vingi ndiyo vichocheo vya maendeleo endelevu, kwa kuwa kupitia siasa hizo wananchi upata fursa ya kueleza, kuchangia, na kushirikisha wengine mawazo na mapendekezo yao juu ya maendeleo ya taifa husika. Na utaratibu huo uchagia kwa kiwango kikubwa kufikia maendeleo ya watu kwa ajili ya watu wenyewe. Kupitia mfumo huo wa siasa haijalishi chama ambacho mwananchi anakuwemo, bado anayo nafasi kubwa ya kuchagia katika maendeleo ya nchi yake.
Kwa siku hizi za karibuni tumeshuhudia wimbi la wanasiasa hasa wale wenye nyadhifa za uwakilishi k**a vile wabunge, madiwani na wenyeviti wa serikali za mitaa au wenyeviti wa vyama vya siasa katika ngazi za wilaya na mikoa, wakihama kutoka chama kimoja kwenda chama kingine. Pamoja na kuwa wapo waliohama kutoka CCM kwenda upinzani, wimbi hili la uhamiaji limewakumba hasa wanachama wa vyama vya upinzani wakitoka kwenye vyama vyao kwenda Chama Cha Mapinduzi. Hoja yao kubwa ni kuunga mkono jitihada za rais Dkt John Pombe Magufuli, kuwa ameonesha nia na uwezo mkubwa wa kutekeleza malengo na matamanio ya Watanzania kwa kiwango kikubwa.
Hoja yao ya pili ni kwamba katika vyama vyao hasa huko upinzani kuwa utawala wa vyama hivyo havizingatii misingi na kanuni za utawala wa sheria pamoja na misingi ya uanzishwaji wa vyama hivyo. Wapo wanao sema kuwa vyama vyao vimekuwa vikiongozwa kwa upendeleo na ukabaila, lakini pia wengine wemedai kuwa vyama vyao vimekuwa na ubadhirifu wa mali za vyama husika. Hoja hizi kwa kweli ni dhaifu hatuwezi kuzitumia kuthibitisha kuhama kwao. Na kwa maana nyingine tunaweza kusema ipo hoja zaidi ya hizo wanazozitaja
Pamoja na kuwa hizi hoja hazijitoshelezi hatukatai kuwa ni haki ya kikatiba ya kujiunga chama anachokitaka mtu ilimradi chama hicho kimesajiliwa halali na kinafanya shughuli za kisiasa kwa mujibu wa sheria na kanuni. Na ndio maana wakati wowote hatukuwahi kuhoji uhamiaji wa wanasiasa kutoka chama kimoja kwenda kingine. Lakini kwa sasa tunalazimika kuhoji hilo kwa sababu uhamaji wake ni sawa na safari ya nyumbu kutoka sehemu moja ya kwenda sehemu nyingine. Ziko sababu kadhaa ambazo tunaweza kuzitumia kujiridhisha kabisa kuwa hoja zinazotolewa na wanaohama vyama si za msingi bali ni zaidi ya wanachosema machoni pa wananchi kupitia vyombo vya habari.
Hoja ya kumuunga mkono Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa kile anachokifanya, wahamaji wengi wanasema kuwa hii ndio sababu ya wao kuhamia Chama Cha Mapinduzi, kwa kuwa Rais huyo anatokana na chama hicho. Hoja hii ni mfu, kwa sababu nyingi mno, moja ni Rais Magufuli hatokani na Chama Cha Mapinduzi k**a wengi wanavyodhani. Rais wa Jamhuri ya Muungano anapatikana kwa njia ya kugombea na kupigiwa kura na wananchi wote. Pamoja na kuwa anatakiwa awe na chama cha kupitia lakini bado anapigiwa kura na wananchi wote. Kwa lugha Rais ni mwananchama wa chama fulani aliyekubaliwa na wananchi kusaidiana nao kwa wakati wa kipindi cha miaka mitano kutekeleza malengo na matamanio ya wananchi. Kwa hiyo ni jukumu la watanzania wote wapenda maendeleo walioko ndani ya chama chake au nje ya chama chake kumuunga mkono. Tuelewane jambo moja kumuunga mkono Rais haina maana kwamba umshangilie anapofanya jambo jema. Hata kumkosoa anapokosea ni kumuunga mkono, mfano Tanzania wakati fulani ilikuwa na mjadala juu ya kusaini mkataba wa kushirikiana na Umoja wa Ulaya katika biashara (EPA) Watanzania wote walijaribu kutoa hoja zao na mawazo yao juu ya waonavyo kuhusu jambo hilo. Kwa muundo huo walikuwa wanamuunga mkono kiongozi wao katika utekelezaji wa shughuli zake. Mfano mwingine ni pale wanapohoji kutoheshimu katiba, jambo hili halifanyiki kwa maana ya kumpinga Rais bali ni kumkumbusha makubaliano ya Watanzania kwa ujumla, Kazi hii haikutaki uhamie kwenye chama chake bali umakini na ufundi wa kueleza jambo ambalo unafikiri linaweza kufanyika kwa maslahi mapana ya taifa.
Jambo la pili ni la kitakwimu, sote tunakumbuka kuwa Mheshimiwa Rais Magufuli amepatikana kwa kupata kura zaidi ya 58% ya wapiga kura wote, waliokuwa wamejiandikisha kupiga kura mwaka 2015. Waliojindikisha ni ni zaidi ya milioni sita mpaka nane ambazo ndizo zilikuwa zinakadiriwa kuwa wananchama wa Chama Cha Mapinduzi wakati huo. Viwango hivyo vinakuonyesha kabisa kuwa Mheshimiwa Rais Magufuli ametokana na wananchi kupitia chama cha siasa, maana yake haikulazimu mwanasiasa kujiunga na chama chake ndo useme unamuunga mkono wakati pengine ulimpingia kura ili awe rais wa Jamhuri ya Muungano.
Tatu, wakati Rais Magufuli ametembelea chuo kikuu cha Dar es Salaam mapema mwaka 2016 nakumbuka alimtaja Dkt (Prof) Kitila kuwa ni mwanasiasa wa mfano kwa maana anaweza kueleza mapungufu na mema ya serikali hata k**a hayuko ndani ya chama chake. Maneno hayo ya Mheshimiwa Rais yanatosha kuthibitishia kuwa hatuhitaji kujiunga na chama chake ili kumuunga mkono. Yanaonyesha wazi wazi kuwa bado mtu ang’e weza kummunga mkono akiwa nje ya chama chake, na bado mambo yakaenda sawa.
Nne ni kuhusu itikadi za chama na utamaduni wa chama, wote tunajua kuwa chama cha siasa kwa namna yoyote hile lazima kiwe na itikadi na utamaduni unaokiendesha. Mfano Chama Cha Mapinduzi itikadi yao hadi sasa wanajinasibisha na siasa za kijamaa na Kujitegemea. Vyama vingine navyo vinaitikadi zake. Mtu anapotaka kujiunga chama cha siasa kwa malengo ya kukisaidia chama husika kwanza ni lazima akubali itikadi ya chama anachotaka kuhamia. Kwa maana, k**a ameikubali na kuielewa itikadi ya chama hicho basi atakuwa mfuasi na mtetezi mzuri wa itikadi husika. Jambo ambalo ni nadra sana kulisikia katika hotuba za wanaohama vyama. Kila anayehama utasikia anasema ana muunga mkono Rais kwa juhudi zake za kusimamia uwajibikaji, na kujitahidi kuleta maendeleo. Hakuna anayetaja kuwa amevutiwa na itikadi anayosimamia Mheshimiwa Rais na chama chake. Hali hiyo inaweza kutufanya kufikiri ama wanayemuunga mkono hana itikadi au wao wenyewe hajajishughulisha kujua itikadi ya chama wanachohamia. Na k**a hivyo ndivyo basi hatuna budi kuwaona watu hao wakihama chama hicho kwenda vyama vingine, kwa kuwa hawana wanachoamini.
Tano, Urais na nchi hizi ni taasisi zinazotakiwa kujisimamia sio kutegemea mtu, mfano mtu anayepewa wajibu wa kusimamia taasisi ya Urais muda wake ni vipindi viwili vya miaka mitano tu k**a ataweza kuchaguliwa katika vipindi hivyo. Kwa upande wa pili nchi ni taasisi inayodumu kwa manufaa ya wananchi kwa muda wote. Kwa mantiki hiyo hatutakiwa kujiunga na chama chochote kwa kumuunga mkono kiongozi wa chama husika. Tunachotakiwa kuunga mkono ni maendeleo na Ustawi wa nchi kwa ujumla. Rais awezi kukaa madarakani milele anakaa kipindi chake kikiisha anatakiwa kurudia nafasi yake ya uraia mwenye sifa ya kuwa Rais Mstaafu. Hivyo si kazi yetu kuunga mkono pale anapokuwa anatekeleza wajibu wake. Lakini pia k**a tunamuunga mkono k**a yeye bila kujua jukumu lake ni nini, maana yake hatujifikirishi kujua je k**a atamaliza muda wake je tutahama chama chake kwa kuwa hatuna wa kumuunga mkono, au tutafuta namna ya kuondokana na nchi yetu. Kwa maana tumejikita katika kuunga mkono mtu binafsi sio nchi au Urais.
Hoja ya ukabila na kutozingatia utawala wa sheria katika vyama walivyokuwemo, hoja hii pia inaweza kupingwa kwa sababu za kihistoria na kisiasa. Hoja ya kihistoria inatuonyesha kuwa waliohama wengi si tu walikuwa ndani ya vyama hivyo awali bali pia walitoka katika chama wanachorudi leo. K**a hivyo ndivyo je huko waliko kuwa awali kulikuwako ukabila na utawala usiozingatia misingi? Je leo kumebadiliaka? Tukiachilia hilo utaona kuwa wote wanaosema ukabila na kutozingatia utawala wa sheria, watu hao waliowengi wamepata ubunge wakiwa huko, wamepata udiwani wakiwa huko na mengine mengi yaliyowanufaisha sana. Sasa wakati huo wanapata nyadhifa na vyeo ukabila huo na utawala usiozingatia taratibu hakuwepo? Na k**a ulikuwepo ni Jitihada zipi walifanya kuhakikisha jambo hilo linaodolewa? K**a hawakufanya jitihada je wanaweza kuturidhisha kuwa wamechangia katika kututengenezea bomu linaloweza kulipuka hapo baadae? Kwa sababu k**a sehemu kuna siasa za ukabila na wewe umeziacha ziendelee kuchanua maana yake umeacha siku moja taifa ligawanyike kwa misingi hiyo ya kikabila.
Si jambo la afya hata kidogo kwa siasa zetu tuapohama vyama vyetu kwa hoja ya kuunga mkono Rais, tunadidimiza itikadi na ukuwaji wa vyama vya saisa.
Mwisho.

09/08/2018

Utii wa Sheria bila Shuruti si Kulazimishana ni Kuheshimiana

Ni ukweli kabisa kuwa ni muhimu sana tukatii sheria bila shuruti. Hiyo ndio sura ya Usta-Afrika wa binadamu, yaani sheria unaifanya kuwa ndio asili ya maisha yako. Si kitu cha lazima. Utii wa sheria bila shuruti ili uweze kutokea, lazima sheria ijisimamie yenyewe. Iwe msumeno, iweze kukata mbele na nyuma. Na hapo ndipo italeta heshima na utu kwa pande zote. Italeta uwajibikaji wa kila mmoja. Kila mwanajamii hatajua anawajibika kwa sheria waliojiwekea.

Tofauti na msingi huo siku hizi kumekuwepo uhamasishaji wa kiwango cha juu kutii sheria bila shuruti, kwa hili nawapongeza sana jeshi la polisi na vyombo vya habari kwa uhamasishaji. Pamoja na pongezi zangu si vyema kufumbia macho pale sheria inapoonekana kuhimizwa upande mmoja na kuacha upande wa pili. Mfano sheria inaruhusu watu kukusanyika na kujadiliana, hii sio utashi wa mtu mmoja ni sheria. Na msingi wake ni kuheshimiana, k**a unaniheshimu utanisikiliza utakuja tujadili, na mimi nitafanya hivyo kwa kuwa nakuheshimu. K**a uniheshimu utaniamrisha nifanye na mimi nitagoma kwa kuwa sikuheshimu.

Pamoja na tukio la viongozi wa vyama vya upinzani huko Tarime kuvutana na askari polisi mpaka kuhumizana si tukio linaloleta heshima katika jamii. Pengine hatuwezi kusema aliyekuwa na kosa ni nani, labda ni wapinzani au polisi, lakini heshima ya watu hao k**a watu ni muhimu sana. Maana yake ni kwamba wang'e heshimiwa labda wang'e tii pila shuruti.

Address

Kinondoni
15885

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mr. Atugoli posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mr. Atugoli:

Share