Agricultural Seed Agency

Agricultural Seed Agency A leading producer and supplier of high quality agricultural seeds on sustainable basis.

Salam za Pongezi ๐Ÿ‘
01/05/2026

Salam za Pongezi ๐Ÿ‘

Heri ya siku ya Wafanyakazi Duniani.  .
01/05/2026

Heri ya siku ya Wafanyakazi Duniani. .

The Green Voice  /2027
28/04/2026

The Green Voice /2027

27/04/2026

ASA inatekeleza jukumu kuu la kuongeza uzalishaji na usambazaji wa mbegu bora za kilimo kwa wakulima kwa bei nafuu ili kuongeza tija na uzalishaji wa mazao mbalimbali.

Wasiliana Nasi kupata mbegu bora. Piga 0733 455 825 kwa Mawasiliano zaidi. Karibu Sana!

๐ŸŒฑ

Heri ya Miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ
26/04/2026

Heri ya Miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ

ASA YAENDELEA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA TOSCI KATIKA UPATIKANAJI WA MBEGU BORAWakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) Imeendelea...
23/04/2026

ASA YAENDELEA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA TOSCI KATIKA UPATIKANAJI WA MBEGU BORA

Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) Imeendelea kuimarisha ushirikiano wake na Taasisi ya Udhibiti wa Ubora wa Mbegu (TOSCI)) kwa lengo la kuhakikisha upatikanaji wa mbegu bora na zenye viwango vinavyokidhi mahitaji ya wakulima nchini.

Ushirikiano huo unalenga kuongeza ufanisi katika uzalishaji, ukaguzi na uthibiti wa mbegu bora ili kuhakikisha wakulima wanapata mbegu zilizo salama, zenye ubora wa juu na zinazoweza kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao mbalimbali ya kilimo.

Cc

KAMATI YA UKAGUZI ASA YAJIONEA SHUGHURI ZA UDHIBITI UBORA WA MBEGU ZA ASA.Kamati ya Ukaguzi ya Wakala wa Mbegu za Kilimo...
17/04/2026

KAMATI YA UKAGUZI ASA YAJIONEA SHUGHURI ZA UDHIBITI UBORA WA MBEGU ZA ASA.

Kamati ya Ukaguzi ya Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) imefanya kikao cha kumi na tano (15) leo tarehe 17 April 2026, makao makuu ya ASA jijini Morogoro kilichofuatiwa na ziara maalumu ya ukaguzi na kujionea kwa vitendo shughuli za udhibiti ubora wa mbegu zinazozalishwa na ASA, ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha uzalishaji unazingatia viwango vilivyowekwa kitaifa na kimataifa.

Lengo ni kuwawezesha wajumbe wa kamati ya ukaguzi kuielewa ASA na kazi zake kuanzia ngazi ya chini ya uzalishaji. Ziara ilihusisha Wajumbe wote wa Kamati ya ukaguzi, wakiambata na Dkt Basil Mhusa Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara akimwakirisha Mtendaji Mkuu wa ASA, Mkurugenzi wa Uzalishaji Dkt. Justine Ringo na Mkaguzi Mkuu wa ndani CPA Fredrick Haule.

Wajumbe walipata maelezo kutoka kwa wataalamu wa udhibiti ubora kuhusu taratibu zinazotumika kupima ubora wa mbegu, ikiwa ni pamoja na vipimo vya uotaji, usafi wa mbegu na uthibitishaji wa aina ya mbegu kabla ya kusambazwa kwa wakulima.

Ziara hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya Kamati ya Ukaguzi ya ASA ya kuhakikisha uwajibikaji, ufanisi na ubora katika shughuli zote za wakala, ikiwa ni pamoja na uzalishaji na usambazaji wa mbegu bora nchini.

BARAZA LA WAFANYAKAZI ASA LAPITISHA BAJETI YA WAKALA KWA MWAKA WA FEDHA  2026/2027.Baraza la Wafanyakazi la Wakala wa Mb...
13/04/2026

BARAZA LA WAFANYAKAZI ASA LAPITISHA BAJETI YA WAKALA KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027.

Baraza la Wafanyakazi la Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) limepitisha mapendekezo ya Mpango na bajeti kwa mwaka wa fedha 2026/2027, ikiwa ni hatua muhimu katika kuimarisha uzalishaji na upatikanaji wa mbegu bora nchini.

Akiwasilisha mapendekezo hayo Leo tarehe 13 April 2026 jijini Morogoro, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Taasisi, Bi. Mary Machaku, amesema kuwa bajeti hiyo inalenga kugharamia shughuli za Uendeshaji wa Taasisi, Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo pamoja na kuongeza ufanisi wa mapato ya ndani ya Wakala.

โ€œASA imepanga kutekeleza vipaumbele mbalimbali vyenye lengo la kuongeza uzalishaji wa mbegu bora za kilimo kufikia Tani 27,200, kuimarisha usambazaji ili kuwafikia wakulima kwa wakati na ujenzi wa uzio wa kilomita 158.5 katika mashamba mbalimbali ya ASAโ€ amesema Bi. Machaku

Aidha, Akiahirisha kikao hicho kwa niaba ya Mtendaji Mkuu, Bw. Leo Mavika, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara, Dkt. Basili Msuha, amesema ASA itaendelea kushirikiana na wakulima wa mkataba ili kuhakikisha uzalishaji wa mbegu bora unaongezeka kwa kuzingatia viwango vya ubora.

โ€œKupitia bajeti hii, ASA imejipanga kuhakikisha mbegu zinapatikana kwa wakati kwa wakulima ili kuongeza tija katika Sekta ya kilimo na nahimiza watumishi wote kufanya kazi kwa bidii na kujituma ili kufanikisha malengo yaliyowekwa,โ€ amesema Dkt. Msuha.

Baadhi ya wajumbe wa Baraza hilo walichangia na kutoa maoni kupitia bajeti hiyo kwa kueleza kuwa inaonesha mwelekeo chanya katika kukuza uzalishaji wa mbegu bora na kuchangia maendeleo ya sekta ya kilimo nchini.

Katika hatua nyingine, Baraza lilifanya uchaguzi mdogo wa Katibu Msaidizi wa Baraza la Wafanyakazi na kumchagua ndugu Erick Iramba kuwa Katibu Msaidizi wa Baraza la wafanyakazi la ASA, kufuatia kifo cha aliyekuwa Katibu Msaidizi wa Baraza hilo, ndugu Constantine Nzila, kilichotokea mwaka 2025.

09/04/2026

ASA inaendelea kufungua milango ya fursa kwa sekta binafsi kushiriki kikamilifu katika Uzalishaji na Usambazaji wa mbegu bora nchini.

Hadi sasa, zaidi ya Wawekezaji 150 wamejitokeza na kuwekeza katika mashamba ya ASA, hatua muhimu inayochochea ukuaji wa kilimo, kuongeza tija, na kuimarisha usalama wa chakula nchini.

Ushirikiano huu ni chachu ya mapinduzi ya kilimo endelevu nchini.

๐ŸŒฑ

Heri ya kumbukumbu ya kifo cha Hayati Sheikh Abeid Amani Karume, Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la M...
07/04/2026

Heri ya kumbukumbu ya kifo cha Hayati Sheikh Abeid Amani Karume, Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Muasisi wa Muungano.

Address

KITALU NA 50 MTAA WA MAGODORO
Morogoro
255

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00

Telephone

0789260109

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Agricultural Seed Agency posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Agricultural Seed Agency:

Share