Agricultural Seed Agency

Agricultural Seed Agency A leading producer and supplier of high quality agricultural seeds on sustainable basis.

Salam za Pongezi.
29/08/2026

Salam za Pongezi.

28/08/2026

Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA), unatekeleza mradi wa ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji kupitia Mfuko wa Extended Credit Facility (ECF) unaogharimu jumla ya shilingi 15,797,800, 491.03 kwa hekta 800 kwenye mashamba ya Kilimi (hekta 400), Arusha (hekta 200) na Msimba (hekta 200).

Lengo ni kuongeza uhimilivu (Resilience) katika
upatikanaji wa mbegu za kilimo nchini kwa kuwezesha
shughuli za uzalishaji wa mbegu kufanyika mara mbili kwa mwaka ili kuongeza uzalishaji wa mbegu na kukidhi
mahitaji ya mbegu kwa wakulima.

Aidha, ujenzi wa miundombinu hii ya umwagiliaji utasaidia kuongeza unyevu shambani k**a mbadala
(supplementary irrigation), kupunguza changamoto ya mabadiliko ya tabianchi hasa uhaba wa mvua.

Heri ya siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa Mtume Muhammad (S.a.w)
25/08/2026

Heri ya siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa Mtume Muhammad (S.a.w)

KAMATI.Wajumbe wa Kamati ya  Fedha, Mipango na Utawala pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Uzalishaji na Usambazaji wa Wakala...
22/08/2026

KAMATI.

Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Uzalishaji na Usambazaji wa Wakala wa Mbegu za kilimo (ASA) wamekutana na kujadili taarifa mbalimbali za Idara na Vitengo kwa Robo ya nne ya mwaka 2025/2026 ikiwa ni maandalizi ya kikao cha Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Mbegu za kilimo ASA kitakachofanyika hivi karibuni.

Kikao hicho kimefanyika tarehe 21 Agosti mwaka huu Makao Makuu ya ASA Mkoani Morogoro ambapo Kamati hizo zimekutana kwa nyakati tofauti kwa lengo la kujadili mikakati mbalimbali ya Taasisi.

Kamati ya Uzalishaji na Usambazaji ikiongozwa na Kaimu Mwenyekiti Prof.Martin Julius Chegere wakati huo k**ati ya Fedha, Mipango na Utawala ikiongozwa na Bwn. Vianney Lweyendela.

WAZIRI KABUDI ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA ASA CHINI YA PROGRAMU YA AFDPWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (...
17/08/2026

WAZIRI KABUDI ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA ASA CHINI YA PROGRAMU YA AFDP

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Mhe. Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, ameridhishwa na utekelezaji wa miradi inayotekelezwa na Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA) kupitia Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP), inayofadhiliwa na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD).

Amesema hayo wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi katika Shamba la Mbegu la Kilimi, Nzega–Tabora, Agosti 17, mwaka huu. Amesema utekelezaji wa miradi hiyo umeleta mabadiliko makubwa katika sekta ya kilimo kwenye mashamba ya ASA, hasa kwa kuongeza uzalishaji wa mbegu.

Katika ziara hiyo, Waziri Kabudi amekagua miradi inayotekelezwa na ASA kupitia AFDP ikiwemo Ujenzi wa Jengo la Utawala, Ujenzi wa Jengo la kukaushia Mbegu, Ujenzi wa Nyumba za Watumishi, pamoja na shughuli za uzalishaji wa Mbegu.

Waziri Prof. Kabudi amesema Serikali itaendelea kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo ya AFDP ili kuhakikisha inafanyika vizuri.

Aidha, Waziri Kabudi alipata fursa ya kukagua miundombinu ya umwagiliaji katika shamba hilo na kujionea kilimo cha kisasa cha mifumo ya umwagiliaji ambacho kimebadilisha sura ya uzalishaji wa mbegu.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde, amesema Wizara inaendelea kusimamia vizuri miradi ya ASA inayotekelezwa kupitia AFDP kwa kufuata taratibu zote za Serikali.

Amesema majengo na vifaa vilivyokaguliwa na Prof. Kabudi vimesaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza uzalishaji wa mbegu kwa ASA.

Ameongeza kuwa Wizara itaendelea kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu katika kuhakikisha miradi yote inaleta tija kwa jamii.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA), Mhandisi Innocent Masaka, amesema maoni yote yaliyotolewa yatafanyiwa kazi kwa uzito unaostahili.

Mhandisi Masaka amesema Shamba la Mbegu la Kilimi, kupitia Programu ya AFDP, linaendelea kuwekewa miundombinu mbalimbali ikiwemo ujenzi wa ghala la kuhifadhia mbegu, kusimika mtambo wa kuchakata mbegu, na ununuzi wa vifaa vya karakana, ambapo miradi hiyo itatumia jumla ya Shilingi bilioni 5.5 katika shamba hilo.

Katika kusherehekea siku kuu ya wakulima Nanenane katika Kanda ya Ziwa  Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Nyamhongolo baa...
08/08/2026

Katika kusherehekea siku kuu ya wakulima Nanenane katika Kanda ya Ziwa Mkoani Mwanza katika Viwanja vya Nyamhongolo baadhi ya wakulima wamejitokeza kununua mbegu na kupata Elimu ya Mbegu bora katika banda la Wakala wa mbegu za kilimo, ASA.

Wananchi hao wamejitokeza kwa wingi na kufurahia kununua mbegu za Mahindi, Mpunga,Alizeti na mbogamboga kwa bei ya Ofa ya Nanenane.

Nanenane Dodoma. Blandina Kilema Naibu katibu Mtendaji Biashara na Ubunifu wa Tume ya Taifa ya Mipango ameipongeza Wakal...
08/08/2026

Nanenane Dodoma.

Blandina Kilema Naibu katibu Mtendaji Biashara na Ubunifu wa Tume ya Taifa ya Mipango ameipongeza Wakala wa Mbegu za kilimo (ASA) kwa kutekeleza Dira ya Maendeleo 2050.

Amesema hayo alipotembelea banda la Wakala wa Mbegu za kilimo katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya wakulima Nanenane Kitaifa Jijini Dodoma leo tarehe 8/8/2026

Aidha Naibu katibu Mkuu Bi. Blandina Kilema amepokelewa na Mwenyeji wake Mha.Innocent Masaka Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mbegu za kilimo (ASA).

Katika kusherehekea siku kuu ya wakulima Nanenane katika Kanda ya Kaskazini Mkoani Arusha baadhi ya wakulima wamejitokez...
08/08/2026

Katika kusherehekea siku kuu ya wakulima Nanenane katika Kanda ya Kaskazini Mkoani Arusha baadhi ya wakulima wamejitokeza kununua mbegu na kupata Elimu ya Mbegu bora katika banda la Wakala wa mbegu za kilimo, ASA.

Wananchi hao wametokeza kwa wingi na kufurahia kununua mbegu za Mahindi, Mpunga,Alizeti na mbogamboga kwa bei ya Ofa ya Nanenane.

Nanenane. Wakati maadhimisho ya siku ya wakulima yakiadhimishwa leo 8/8/2026 kitaifa Mkoani Dodoma kanda ya kati, wakuli...
08/08/2026

Nanenane.

Wakati maadhimisho ya siku ya wakulima yakiadhimishwa leo 8/8/2026 kitaifa Mkoani Dodoma kanda ya kati, wakulima wamejitokeza kwa wingi kupata elimu na kununua mbegu bora za kilimo katika Mabanda ya wakala wa mbegu za kilimo ASA katika kanda zote tisa nchini.

Kwa Mkoa wa Dodoma wakulima wengi wameonekana wakinunua Mbegu bora za Mahindi aina ya T105, SITUKA M1, Mbegu ya Mpunga Saro 5 (TXD 306), Alizeti aina ya Record pamoja na mbegu za Mbogamboga.

Mwitikio mkubwa wa wakulima kununua mbegu za ASA unatokana na bei nzuri, elimu inayotolewa pamoja na ufanisi wa vipando vya mbegu hizo katika viwanja vya nane nane mwaka huu.

Wakala kwa upande mwingine umejipanga kuongeza uzalizalishaji mbegu za mahindi, mpunga, alizeti, maharage, ufuta na mbogamboga ili kukidhi mahitaji makubwa yanayoendelea kujitokeza kutokana na wakulima kupata mwamko wa kupanda mbegu bora.

Address

KITALU NA 50 MTAA WA MAGODORO
Morogoro
255

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00

Telephone

0789260109

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Agricultural Seed Agency posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Agricultural Seed Agency:

Shortcuts

Share