Pata ushauri ili uboresha maisha yako kupitia kilimo, ufugaji au Biashara

Pata ushauri ili uboresha maisha yako kupitia kilimo, ufugaji au Biashara Badilisha maisha yako, tumia teknolojia rahisi ili upate maji kwa matumizi ya nyumbani, mifugo na bustani, nishati ya jua, mbolea asilia, n.k.

Page hii ni kwa ajili ya kuwasaidia wakulima, wafugaji na wafanya biashara kupata ushauri wa kitaalamu kwa bei nafuu kwa kutumia mtandao. Mtu yeyote mwenye uhitaji wa ushauri toka kwa wataalamu atatakiwa kuwasiliana na sisi kwa kutumia simu, facebook au e-mail ili kupewa maelekezo namna ya kupata ushauri huo. Kuandika mchanganuo wa biashara ni Shs. 250,000/=
Ushauri pasipo fika field(Site) ni Shs.

30,000/=

Kwenda site: Nauli na Shs. 80,000/= kwa siku. Unaweza kupiga simu No. 0658152878 kwa maelekezo.

06/11/2014

JE? NI NANI MWENYE KIPATO KIZURI KATI YA MKULIMA NA MFUGAJI? ELEZEA NI KWA NINI, Karibuni wadau tujadili hili ili kutatua changamoto zilizopo kwenye kilimo na ufugaji!

19/06/2014

BEI ZA CHINI ZA MAZAO YA KILIMO ZINAWATIA UMASIKINI WAKULIMA WETU WADOGO NA WA KATI.

Wakulima wadogo na wa kati wamekuwa wakijitahidi sana kulima mazao mbalimbali kila mwaka ili kuweza kujipatia chakula na kujiendeleza kiuchumi. Jambo moja kubwa linalofanya maisha ya mkulima kuwa duni ni kuwepo kwa bei za chini za mazao mengi Nchini hali inayomfanya Mkulima kutopata faida inayomwezesha kubadili maisha yake na kubakia tu akifanya kilimo k**a utamaduni. Ni vizuri Serikali ikaboresha mazingira ya masoko ya mazao ya kilimo nchini kwa kujenga viwanda vya kusindika mazao na pia kupanua wigo wa masoko ya mazao kwa kuwaruhusu wakulima kuuza mazao yao nje ya Nchi pindi inapohitajika k**a wanavyoruhusiwa wataalamu mbalimbali kufanya kazi nje ya Nchi kwa kutafuta malisho yaliyo bora. Kilimo nacho ni ajira, hivyo k**a ni ajira lazima uhuru wa mauzo ya mazao popote utolewe, K**a Serikali inazuia uuzwaji wa mazao nje ya Nchi basi haina budi iyanunue kwa bei nzuri toka kwa wakulima na kuyaweka kwenye bohari ili yasaidie wakati wa njaa, la sivyo mkulima ataendelea kuwa maskini na vijana wengi hasa wasomi watakimbia kilimo kwa kuwa hakina tija, Lakini endapo masoko yataboreshwa, wengi wao watakimbilia kwenye kilimo na tutakuwa tumepunguza tatizo la ajira kwa kiasi kikubwa kwa kuwa Tanzania bado inayo ardhi nzuri na ya kutosha inayofaa kwa kilimo.

Address

SUA
Morogoro
3003

Telephone

0658152878

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Pata ushauri ili uboresha maisha yako kupitia kilimo, ufugaji au Biashara posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Pata ushauri ili uboresha maisha yako kupitia kilimo, ufugaji au Biashara:

Share